< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Аллилуия. Славьте Господа, ибо Он благ, ибо вовек милость Его!
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Так да скажут избавленные Господом, которых избавил Он от руки врага,
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
и собрал от стран, от востока и запада, от севера и моря.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
Они блуждали в пустыне по безлюдному пути и не находили населенного города;
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
терпели голод и жажду, душа их истаевала в них.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он избавил их от бедствий их,
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
и повел их прямым путем, чтобы они шли к населенному городу.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих:
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
ибо Он насытил душу жаждущую и душу алчущую исполнил благами.
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Они сидели во тьме и тени смертной, окованные скорбью и железом;
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
ибо не покорялись словам Божиим и небрегли о воле Всевышнего.
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
Он смирил сердце их работами; они преткнулись, и не было помогающего.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он спас их от бедствий их;
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
вывел их из тьмы и тени смертной, и расторгнул узы их.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих:
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
ибо Он сокрушил врата медные и вереи железные сломил.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Безрассудные страдали за беззаконные пути свои и за неправды свои;
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
от всякой пищи отвращалась душа их, и они приближались ко вратам смерти.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он спас их от бедствий их;
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
послал слово Свое и исцелил их, и избавил их от могил их.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих!
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
Да приносят Ему жертву хвалы и да возвещают о делах Его с пением!
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Отправляющиеся на кораблях в море, производящие дела на больших водах,
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
видят дела Господа и чудеса Его в пучине:
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
Он речет, - и восстанет бурный ветер и высоко поднимает волны его:
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
восходят до небес, нисходят до бездны; душа их истаевает в бедствии;
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
они кружатся и шатаются, как пьяные, и вся мудрость их исчезает.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он вывел их из бедствия их.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
Он превращает бурю в тишину, и волны умолкают.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
И веселятся, что они утихли, и Он приводит их к желаемой пристани.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих!
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Да превозносят Его в собрании народном и да славят Его в сонме старейшин!
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
Он превращает реки в пустыню и источники вод - в сушу,
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
землю плодородную - в солончатую, за нечестие живущих на ней.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Он превращает пустыню в озеро, и землю иссохшую - в источники вод;
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
и поселяет там алчущих, и они строят город для обитания;
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
засевают поля, насаждают виноградники, которые приносят им обильные плоды.
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
Он благословляет их, и они весьма размножаются, и скота их не умаляет.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Уменьшились они и упали от угнетения, бедствия и скорби,
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
Он изливает бесчестие на князей и оставляет их блуждать в пустыне, где нет путей.
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
Бедного же извлекает из бедствия и умножает род его, как стада овец.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Праведники видят сие и радуются, а всякое нечестие заграждает уста свои.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Кто мудр, тот заметит сие и уразумеет милость Господа.