< Mithali 7 >
1 Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
Figlio mio, custodisci le mie parole e fà tesoro dei miei precetti.
2 Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
Osserva i miei precetti e vivrai, il mio insegnamento sia come la pupilla dei tuoi occhi.
3 Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
Lègali alle tue dita, scrivili sulla tavola del tuo cuore.
4 Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
Dì alla sapienza: «Tu sei mia sorella», e chiama amica l'intelligenza,
5 ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
perché ti preservi dalla donna forestiera, dalla straniera che ha parole di lusinga.
6 Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
Mentre dalla finestra della mia casa stavo osservando dietro le grate,
7 Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
ecco vidi fra gli inesperti, scorsi fra i giovani un dissennato.
8 Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
Passava per la piazza, accanto all'angolo della straniera, e s'incamminava verso la casa di lei,
9 Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
all'imbrunire, al declinare del giorno, all'apparir della notte e del buio.
10 Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
Ecco farglisi incontro una donna, in vesti di prostituta e la dissimulazione nel cuore.
11 Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
Essa è audace e insolente, non sa tenere i piedi in casa sua.
12 Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
Ora è per la strada, ora per le piazze, ad ogni angolo sta in agguato.
13 Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
Lo afferra, lo bacia e con sfacciataggine gli dice:
14 leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
«Dovevo offrire sacrifici di comunione; oggi ho sciolto i miei voti;
15 hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
per questo sono uscita incontro a te per cercarti e ti ho trovato.
16 Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
Ho messo coperte soffici sul mio letto, tela fine d'Egitto;
17 Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
ho profumato il mio giaciglio di mirra, di aloè e di cinnamòmo.
18 Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
Vieni, inebriamoci d'amore fino al mattino, godiamoci insieme amorosi piaceri,
19 Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
poiché mio marito non è in casa, è partito per un lungo viaggio,
20 Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
ha portato con sé il sacchetto del denaro, tornerà a casa il giorno del plenilunio».
21 katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
Lo lusinga con tante moine, lo seduce con labbra lascive;
22 Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
egli incauto la segue, come un bue va al macello; come un cervo preso al laccio,
23 mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
finché una freccia non gli lacera il fegato; come un uccello che si precipita nella rete e non sa che è in pericolo la sua vita.
24 Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
Ora, figlio mio, ascoltami, fà attenzione alle parole della mia bocca.
25 Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
Il tuo cuore non si volga verso le sue vie, non aggirarti per i suoi sentieri,
26 Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
perché molti ne ha fatti cadere trafitti ed erano vigorose tutte le sue vittime.
27 Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )
La sua casa è la strada per gli inferi, che scende nelle camere della morte. (Sheol )