< Mithali 20 >

1 Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
Wiyn is a letcherouse thing and drunkenesse is ful of noise; who euere delitith in these, schal not be wijs.
2 Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
As the roryng of a lioun, so and the drede of the kyng; he that territh hym to ire, synneth ayens his owne lijf.
3 Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
It is onour to a man that departith hym silf fro stryuyngis; but fonned men ben medlid with dispisyngis.
4 Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
A slow man nolde ere for coold; therfor he schal begge in somer, and me schal not yyue to hym.
5 Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
As deep watir, so counsel is in the herte of a man; but a wijs man schal drawe it out.
6 Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
Many men ben clepid merciful; but who schal fynde a feithful man?
7 Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
Forsothe a iust man that goith in his simplenesse, schal leeue blessid sones aftir hym.
8 Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
A king that sittith in the seete of doom, distrieth al yuel bi his lokyng.
9 Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
Who may seie, Myn herte is clene; Y am clene of synne?
10 Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
A weiyte and a weiyte, a mesure and a mesure, euer eithir is abhomynable at God.
11 Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
A child is vndurstondun bi hise studies, yf his werkis ben riytful and cleene.
12 Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
An eere heringe, and an iye seynge, God made euere eithir.
13 Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
Nyle thou loue sleep, lest nedynesse oppresse thee; opene thin iyen, and be thou fillid with looues.
14 “Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
Ech biere seith, It is yuel, it is yuel; and whanne he hath go awey, thanne he schal haue glorie.
15 Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
Gold, and the multitude of iemmes, and a preciouse vessel, ben the lippis of kunnyng.
16 Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
Take thou awei the cloth of hym, that was borewe of an othere man; and for straungeris take thou awei a wed fro hym.
17 Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
The breed of a leesing is sweet to a man; and aftirward his mouth schal be fillid with rikenyng.
18 Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
Thouytis ben maad strong bi counselis; and bateils schulen be tretid bi gouernals.
19 Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
Be thou not medlid with him that schewith pryuetees, and goith gylefulli, and alargith hise lippis.
20 Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
The liyt of hym that cursith his fadir and modir, schal be quenchid in the myddis of derknessis.
21 Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
Eritage to which me haastith in the bigynnyng, schal wante blessing in the laste tyme.
22 Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
Seie thou not, Y schal yelde yuel for yuel; abide thou the Lord, and he schal delyuere thee.
23 Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
Abhomynacioun at God is weiyte and weiyte; a gileful balaunce is not good.
24 Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
The steppis of man ben dressid of the Lord; who forsothe of men mai vndurstonde his weie?
25 Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
Falling of man is to make auow to seyntis, and aftirward to withdrawe the vowis.
26 Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
A wijs kyng scaterith wickid men; and bowith a bouwe of victorie ouer hem.
27 Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
The lanterne of the Lord is the spirit of man, that sekith out alle the priuetees of the wombe.
28 Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
Merci and treuthe kepen a kyng; and his trone is maad strong bi mekenesse.
29 Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
The ful out ioiyng of yonge men is the strengthe of hem; and the dignyte of elde men is hoornesse.
30 Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.
The wannesse of wounde schal wipe aweie yuels, and woundis in the priuyere thingis of the wombe.

< Mithali 20 >