< Mithali 28 >

1 Waovu hukimbia wakati hakuna mtu anayewafukuza, bali wale watendao haki ni thabiti kama simba kijana.
A wickid man fleeth, whanne no man pursueth; but a iust man as a lioun tristynge schal be with out ferdfulnesse.
2 Kwa sababu ya uhalifu wa nchi, kuna wakuu wengi, bali kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa, itadumu kwa muda mrefu.
For the synnes of the lond ben many princis therof; and for the wisdom of a man, and for the kunnyng of these thingis that ben seid, the lijf of the duyk schal be lengere.
3 Mtu masikini mwenye kukandamiza watu wengine masikini ni kama mvua inayopiga ambayo haisazi chakula.
A pore man falsli calengynge pore men, is lijk a grete reyn, wherynne hungur is maad redi.
4 Wale wanaokataa sheria huwatukuza watu waovu, bali wale wenye kuitunza sheria hupigana dhidi yao.
Thei that forsaken the lawe, preisen a wickid man; thei that kepen `the lawe, ben kyndlid ayens hym.
5 Watu wabaya hawafahamu haki, bali wale wanaomtafuta Yehova wanafahamu kila kitu.
Wickid men thenken not doom; but thei that seken the Lord, perseyuen alle thingis.
6 Ni bora mtu masikini ambaye anatembea katika uadilifu, kuliko mtu tajiri ambaye ni mdanganyifu katika njia zake.
Betere is a pore man goynge in his sympilnesse, than a riche man in schrewid weies.
7 Yeye anayetunza sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali mwenye ushirika na walafi humwaibisha baba yake.
He that kepith the lawe, is a wijs sone; but he that fedith glotouns, schendith his fadir.
8 Anayepata mafanikio kwa kutoza riba kubwa anakusanya utajiri wake kwa ajili ya mwingine ambaye atakuwa na huruma kwa watu masikini.
He that gaderith togidere richessis bi vsuris, and fre encrees, gaderith tho togidere ayens pore men.
9 Kama mtu atageuzia mbali sikio lake kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
His preyer schal be maad cursid, that bowith awei his eere; that he here not the lawe.
10 Yeye anayempotosha mwenye uadilifu katika njia ya uovu ataangukia kwenye shimo lake mwenyewe, bali wakamilifu watapata urithi mwema.
He that disseyueth iust men in an yuel weye, schal falle in his perisching; and iuste men schulen welde hise goodis.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu masikini mwenye ufahamu atamtafuta.
A ryche man semeth wijs to him silf; but a pore man prudent schal serche him.
12 Kunapokuwa na ushindi kwa wenye kutenda haki, kunafuraha kuu, bali wanapoinuka waovu, watu hujificha wenyewe.
In enhaunsing of iust men is miche glorie; whanne wickid men regnen, fallyngis of men ben.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali mwenye kutubu na kuziacha ataonyeshwa rehema.
He that hidith hise grete trespassis, schal not be maad riytful; but he that knoulechith and forsakith tho, schal gete merci.
14 Anafuraha ambaye huishi kwa unyenyekevu, bali anayeufanya moyo wake ataanguka katika taabu.
Blessid is the man, which is euere dredeful; but he that is `harde of soule, schal falle in to yuel.
15 Kama simba anayeunguruma au dubu anayeshabulia ni kama mtawala mwovu juu ya watu masikini.
A rorynge lioun, and an hungry bere, is a wickid prince on a pore puple.
16 Mtawala anayekosa ufahamu ni mkandamizaji katili, bali mwenye kuchukia aibu atadumu katika siku zake.
A duyk nedi of prudence schal oppresse many men bi fals chalenge; but the daies of hym that hatith aueryce, schulen be maad longe.
17 Kama mtu anahatia kwa sababu amemwaga damu ya mtu, atakuwa mkimbizi hadi kifo na hakuna atakayemsaidia.
No man susteyneth a man that falsly chalengith the blood of a man, if he fleeth `til to the lake.
18 Mwenye kuenenda kwa ukaminifu atakuwa salama, bali mwenye njia ya udanganyifu ataanguka ghafla.
He that goith simpli, schal be saaf; he that goith bi weiward weies, schal falle doun onys.
19 Anayefanya kazi kwenye shamba lake atapata chakula kingi, bali afuataye shughuli za upuuzi atapata umasikini mkubwa.
He that worchith his lond, schal be fillid with looues; he that sueth ydelnesse, schal be fillid with nedynesse.
20 Mtu mwaminifu atapata baraka nyingi bali apataye utajiri wa haraka hawezi kukosa adhabu.
A feithful man schal be preisid myche; but he that hastith to be maad riche, schal not be innocent.
21 Siyo vema kuonyesha upendeleo, lakini kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya.
He that knowith a face in doom, doith not wel; this man forsakith treuthe, yhe, for a mussel of breed.
22 Mtu mchoyo huharakisha kwenye utajiri, lakini hajui ni umasikini gani utakuja juu yake.
A man that hastith to be maad riche, and hath enuye to othere men; woot not that nedinesse schal come on hym.
23 Anayemkaripia mtu baadaye atapata fadhila zaidi kutoka kwake kuliko mwenye kumsifia sana kwa ulimi wake.
He that repreueth a man, schal fynde grace aftirward at hym; more than he that disseyueth bi flateryngis of tunge.
24 Yule anayemwibia baba yake na mama yake na kusema, “Hiyo siyo dhambi,” ni mshirika wa mwenye kuharibu.
He that withdrawith ony thing fro his fadir and fro his modir, and seith that this is no synne, is parcener of a manquellere.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea mafarakano, bali anayemtumaini Yehova atafanikiwa.
He that auauntith hym silf, and alargith, reisith stryues; but he that hopith in the Lord, schal be sauyd.
26 Yule anayeutumaini moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, bali anayekwenda kwa hekima atajilinda mbali na hatari.
He that tristith in his herte, is a fool; but he that goith wiseli,
27 Mwenye kuwapa masikini hatapungukiwa kitu, bali anayewafumbia macho atapokea laana nyingi.
schal be preysid. He that yyueth to a pore man, schal not be nedi; he that dispisith `a pore man bisechynge, schal suffre nedynesse.
28 Watu waovu wanapoinuka, watu hujificha wenyewe, lakini watu waovu wataangamia, wale watendao haki wataongezeka.
Whanne vnpitouse men risen, men schulen be hid; whanne tho `vnpitouse men han perischid, iust men schulen be multiplied.

< Mithali 28 >