< Mithali 16 >

1 Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
It perteyneth to man to make redi the soule; and it perteyneth to the Lord to gouerne the tunge.
2 Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
Alle the weies of men ben opyn to the iyen of God; the Lord is a weiere of spiritis.
3 Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
Schewe thi werkys to the Lord; and thi thouytis schulen be dressid.
4 Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
The Lord wrouyte alle thingis for hym silf; and he made redi a wickid man to the yuel dai.
5 Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
Abhomynacioun of the Lord is ech proude man; yhe, thouy the hond is to the hond, he schal not be innocent. The bigynnyng of good weie is to do riytwisnesse; forsothe it is more acceptable at God, than to offre sacrifices.
6 Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
Wickidnesse is ayen bouyt bi merci and treuthe; and me bowith awei fro yuel bi the drede of the Lord.
7 Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
Whanne the weyes of man plesen the Lord, he schal conuerte, yhe, hise enemyes to pees.
8 Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
Betere is a litil with riytfulnesse, than many fruytis with wickidnesse.
9 Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
The herte of a man schal dispose his weie; but it perteyneth to the Lord to dresse hise steppis.
10 Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
Dyuynyng is in the lippis of a king; his mouth schal not erre in doom.
11 Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
The domes of the Lord ben weiyte and a balaunce; and hise werkis ben alle the stoonys of the world.
12 Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
Thei that don wickidli ben abhomynable to the king; for the trone of the rewme is maad stidfast bi riytfulnesse.
13 Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
The wille of kyngis is iust lippis; he that spekith riytful thingis, schal be dressid.
14 Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
Indignacioun of the kyng is messangeris of deth; and a wijs man schal plese him.
15 Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
Lijf is in the gladnesse of the `cheer of the king; and his merci is as a reyn comynge late.
16 Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
Welde thou wisdom, for it is betere than gold; and gete thou prudence, for it is precyousere than siluer.
17 Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
The path of iust men bowith awei yuelis; the kepere of his soule kepith his weie.
18 Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
Pride goith bifore sorewe; and the spirit schal be enhaunsid byfor fallyng.
19 Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
It is betere to be maad meke with mylde men, than to departe spuylis with proude men.
20 Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
A lerned man in word schal fynde goodis; and he that hopith in the Lord is blessid.
21 Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
He that is wijs in herte, schal be clepid prudent; and he that is swete in speche, schal fynde grettere thingis.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
The welle of lijf is the lernyng of him that weldith; the techyng of foolis is foli.
23 Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
The herte of a wijs man schal teche his mouth; and schal encreesse grace to hise lippis.
24 Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
Wordis wel set togidere is a coomb of hony; helthe of boonys is the swetnesse of soule.
25 Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
A weye is that semeth riytful to a man; and the laste thingis therof leden to deth.
26 Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
The soule of a man trauelinge trauelith to hym silf; for his mouth compellide hym.
27 Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
An vnwijs man diggith yuel; and fier brenneth in hise lippis.
28 Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
A weiward man reisith stryues; and a man ful of wordis departith princis.
29 Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
A wickid man flaterith his frend; and ledith hym bi a weie not good.
30 Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
He that thenkith schrewid thingis with iyen astonyed, bitith hise lippis, and parformeth yuel.
31 Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
A coroun of dignyte is eelde, that schal be foundun in the weies of riytfulnesse.
32 Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
A pacient man is betere than a stronge man; and he that `is lord of his soule, is betere than an ouercomere of citees.
33 Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.
Lottis ben sent into the bosum; but tho ben temperid of the Lord.

< Mithali 16 >