< Hesabu 2 >

1 BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia,
And Jehovah spoke to Moses and to Aaron, saying,
2 Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
The sons of Israel shall encamp every man by his own standard, with the ensigns of their fathers' houses. They shall encamp round about opposite the tent of meeting.
3 Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda.
And those who encamp on the east side toward the sunrise shall be those of the standard of the camp of Judah, according to their armies. And the ruler of the sons of Judah shall be Nahshon the son of Amminadab.
4 Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
And his army, and those who were numbered of them, were seventy-four thousand and six hundred.
5 Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari.
And those who encamp next to him shall be the tribe of Issachar. And the ruler of the sons of Issachar shall be Nethanel the son of Zuar.
6 Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
And his army, and those who were numbered of it, were fifty-four thousand and four hundred.
7 Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni.
Then the tribe of Zebulun. And the ruler of the sons of Zebulun shall be Eliab the son of Helon.
8 Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
And his army, and those who were numbered of it, were fifty-seven thousand and four hundred.
9 Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
All who were numbered of the camp of Judah were a hundred eighty-six thousand and four hundred, according to their armies. They shall set forth first.
10 Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri.
On the south side shall be the standard of the camp of Reuben according to their armies. And the ruler of the sons of Reuben shall be Elizur the son of Shedeur.
11 Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
And his army, and those who were numbered of it, were forty-six thousand and five hundred.
12 Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai.
And those who encamp next to him shall be the tribe of Simeon. And the ruler of the sons of Simeon shall be Shelumiel the son of Zurishaddai.
13 Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
And his army, and those who were numbered of them, were fifty-nine thousand and three hundred.
14 Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli.
Then the tribe of Gad. And the ruler of the sons of Gad shall be Eliasaph the son of Reuel.
15 Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
And his army, and those who were numbered of them, were forty-five thousand and six hundred and fifty.
16 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
All who were numbered of the camp of Reuben were a hundred fifty-one thousand and four hundred and fifty, according to their armies. And they shall set forth second.
17 Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
Then the tent of meeting shall set forward, with the camp of the Levites in the midst of the camps. As they encamp, so shall they set forward, every man in his place, by their standards.
18 Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
On the west side shall be the standard of the camp of Ephraim according to their armies. And the ruler of the sons of Ephraim shall be Elishama the son of Ammihud.
19 Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
And his army, and those who were numbered of them, were forty thousand and five hundred.
20 Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri.
And next to him shall be the tribe of Manasseh. And the ruler of the sons of Manasseh shall be Gamaliel the son of Pedahzur.
21 Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
And his army, and those who were numbered of them, were thirty-two thousand and two hundred.
22 Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni.
Then the tribe of Benjamin. And the ruler of the sons of Benjamin shall be Abidan the son of Gideoni.
23 Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
And his army, and those who were numbered of them, were thirty-five thousand and four hundred.
24 Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
All who were numbered of the camp of Ephraim were a hundred eight thousand and a hundred, according to their armies. And they shall set forth third.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
On the north side shall be the standard of the camp of Dan according to their armies. And the ruler of the sons of Dan shall be Ahiezer the son of Ammishaddai.
26 Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
And his army, and those who were numbered of them, were sixty-two thousand and seven hundred.
27 Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani.
And those who encamp next to him shall be the tribe of Asher. And the ruler of the sons of Asher shall be Pagiel the son of Ochran.
28 Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
And his army, and those who were numbered of them, were forty-one thousand and five hundred.
29 Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
Then the tribe of Naphtali. And the ruler of the sons of Naphtali shall be Ahira the son of Enan.
30 Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
And his army, and those who were numbered of them, were fifty-three thousand and four hundred.
31 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
All that were numbered of the camp of Dan were a hundred fifty-seven thousand and six hundred. They shall set forth rearmost by their standards.
32 Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550.
These are those who were numbered of the sons of Israel by their fathers' houses. All who were numbered of the camps according to their armies were six hundred three thousand and five hundred and fifty.
33 Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
But the Levites were not numbered among the sons of Israel, as Jehovah commanded Moses.
34 Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.
Thus did the sons of Israel. According to all that Jehovah commanded Moses, so they encamped by their standards, and so they set forward, everyone by their families, according to their fathers' houses.

< Hesabu 2 >