< Hesabu 1 >

1 Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
And Jehovah spoke to Moses in the wilderness of Sinai, in the tent of meeting, on the first day of the second month, in the second year after they came out of the land of Egypt, saying,
2 'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
Take ye the sum of all the congregation of the sons of Israel, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, every male, by their polls,
3 kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
from twenty years old and upward, all who are able to go forth to war in Israel. Thou and Aaron shall number them by their armies.
4 Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
And with you there shall be a man of every tribe, each one head of his fathers' house.
5 Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
And these are the names of the men who shall stand with you. Of Reuben: Elizur the son of Shedeur.
6 kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
Of Simeon: Shelumiel the son of Zurishaddai.
7 Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
Of Judah: Nahshon the son of Amminadab.
8 Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
Of Issachar: Nethanel the son of Zuar.
9 kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
Of Zebulun: Eliab the son of Helon.
10 kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
Of the sons of Joseph, of Ephraim: Elishama the son of Ammihud; of Manasseh: Gamaliel the son of Pedahzur.
11 kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
Of Benjamin: Abidan the son of Gideoni.
12 Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
Of Dan: Ahiezer the son of Ammishaddai.
13 kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
Of Asher: Pagiel the son of Ochran.
14 kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
Of Gad: Eliasaph the son of Deuel.
15 na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
Of Naphtali: Ahira the son of Enan.
16 Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
These are those who were called from the congregation, the rulers of the tribes of their fathers. They were the heads of the thousands of Israel.
17 Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
And Moses and Aaron took these men who are mentioned by name,
18 na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
and they assembled all the congregation together on the first day of the second month. And they declared their ancestry after their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, by their polls.
19 Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
As Jehovah commanded Moses, so he numbered them in the wilderness of Sinai.
20 Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
And the sons of Reuben, Israel's firstborn, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, by their polls, every male from twenty years old and upward, all who were able to go forth to war,
21 Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
those who were numbered of them, of the tribe of Reuben, were forty-six thousand and five hundred.
22 Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Simeon, their generations, by their families, by their fathers' houses, those who were numbered of it, according to the number of the names, by their polls, every male from twenty years old and upward, all who were able to go forth to war,
23 Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
those who were numbered of them, of the tribe of Simeon, were fifty-nine thousand and three hundred.
24 Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Gad, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
25 Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
those who were numbered of them, of the tribe of Gad, were forty-five thousand six hundred and fifty.
26 Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Judah, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
27 walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
those who were numbered of them, of the tribe of Judah, were seventy-four thousand and six hundred.
28 Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Issachar, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
29 Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
those who were numbered of them, of the tribe of Issachar, were fifty-four thousand and four hundred.
30 Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Zebulun, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
31 Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
those who were numbered of them, of the tribe of Zebulun, were fifty-seven thousand and four hundred.
32 Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Joseph, namely, of the sons of Ephraim, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
33 Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
those who were numbered of them, of the tribe of Ephraim, were forty thousand and five hundred;
34 Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
of the sons of Manasseh, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
35 Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
those who were numbered of them, of the tribe of Manasseh, were thirty-two thousand and two hundred.
36 Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Benjamin, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
37 Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
those who were numbered of them, of the tribe of Benjamin, were thirty-five thousand and four hundred.
38 Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Dan, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
39 Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
those who were numbered of them, of the tribe of Dan, were sixty-two thousand and seven hundred.
40 Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Of the sons of Asher, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
41 Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
those who were numbered of them, of the tribe of Asher, were forty-one thousand and five hundred.
42 Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the sons of Naphtali, their generations, by their families, by their fathers' houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all that were able to go forth to war,
43 Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
those who were numbered of them, of the tribe of Naphtali, were fifty-three thousand and four hundred.
44 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
These are those who were numbered, whom Moses and Aaron numbered, and the rulers of Israel, being twelve men. They were each one for his fathers' house.
45 Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
So all those who were numbered of the sons of Israel by their fathers' houses, from twenty years old and upward, all who were able to go forth to war in Israel,
46 Walihesabu wanaume 603, 550.
even all those who were numbered were six hundred three thousand and five hundred and fifty.
47 Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
But the Levites according to the tribe of their fathers were not numbered among them.
48 Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
For Jehovah spoke to Moses, saying,
49 “usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
Only the tribe of Levi thou shall not number, neither shall thou take the sum of them among the sons of Israel,
50 Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
but appoint thou the Levites over the tabernacle of the testimony, and over all the furniture of it, and over all that belongs to it. They shall bear the tabernacle, and all the furniture of it, and they shall minister to it, and shall encamp round about the tabernacle.
51 Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
And when the tabernacle sets forward, the Levites shall take it down, and when the tabernacle is to be pitched, the Levites shall set it up. And the stranger who comes near shall be put to death.
52 Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
And the sons of Israel shall pitch their tents, every man by his own camp, and every man by his own standard, according to their armies.
53 Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
But the Levites shall encamp round about the tabernacle of the testimony, that there be no wrath upon the congregation of the sons of Israel. And the Levites shall keep the charge of the tabernacle of the testimony.
54 Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.
Thus did the sons of Israel. According to all that Jehovah commanded Moses, so they did.

< Hesabu 1 >