< Hesabu 15 >

1 Kisha BWANA akanena na Musa, akasema,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
2 “Sema na wana wa Israeli uwaambie, 'Mtakapoingia katka nchi ambayo mtaishi, ambayo BWANA atawapa,
глаголи сыном Израилевым и речеши к ним: егда внидете в землю вселения вашего, юже Аз даю вам,
3 mtatakiwa kuandaa sadaka kwa moto kwa BWANA, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kukamilisha kiapo au sadaka ya hiari, au sadaka katika sikukuu zenu, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo.
и сотворите принос Господу во всесожжение или жертву, еже возвеличити мольбу, или благовольну, или в праздники вашя в воню благовония Господу, аще убо от волов, или от овец:
4 Utamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
и да принесет приносяй дар свой Господу жертву, муки пшеничны десятую часть ефи (меры), вмешены в елей четвертыя части ина (меры):
5 Na tena mtatoa pamoja na sadaka ya kuteketezwa, au kwa sadaka ya divai robo ya hini ya sadaka ya vinywaji kwa kila mwanakondoo.
и вина на возлияние четвертую часть ина сотворите во всесожжение или в жертву: агнцу единому да сотвориши толико, принос воню благовония Господу.
6 Kama unatoa sadaka ya kondoo dume, utaandaa sadaka ya unga ya sehemu za kumi mbili za efa ya unga mwembamba uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya divai.
И овну, егда творите его во всесожжение или в жертву, да сотвориши жертву муки пшеничны две десятины вмешаны в елеи, третию часть ина (меры):
7 Kwa sadaka ya kinywaji, mtatoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ambayo itatoa harufu nzuri kwa BWANA.
и вина на возлияние третию часть ина принесете в воню благовония Господу.
8 Utakapoandaa fahari kwa ajiliy a sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo, au sadaka ya amani kwa BWANA,
Аще же творите от волов во всесожжение или в жертву, еже возвеличити мольбу, или во спасителное Господу,
9 Ndipo utakapotoa sadaka ya fahari pamoja na sadaka ya unga ya sehemu za kumi tatu za unga mwembamba uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
и принесет с телцем принос муки пшеничны три десятины вмешаны в елей, пол ина (меры):
10 Mtatoa sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai, sadaka iloyotengenezwa kwa moto ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
и вина на возлияние пол ина (меры), принос в воню благовония Господу.
11 Itafanyika hivi kwa kila fahari, kwa kila kondoo dume, na kila mwanakondoo dume au mbuzi mchanga.
Тако да сотвориши телцу единому, или овну единому, или агнцу единому от овец или от коз:
12 Kila sdaka utakayoindaa na kuitoa itafanyika kama ilivyoanishwa hapa.
по числу их, яже аще сотворите, тако сотворите единому по числу их.
13 Wazawa wote wa Israeli watafanya mambo haya kwa utaratibu huu, yeyote atakayeleta sadaka iliyotengenezwa kwa moto, ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
Всяк туземец да сотворит тако сицевая принести приношения в воню благовония Господу:
14 Na kama kuna mgeni anayeishi kati yenu, au yeyote atakayeishi na watu wa vizazi vyenu vyote, lazima atengeneze sadaka iliytoengenezwa kwa moto, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Atafanya kama mnavyofanya.
аще же пришлец в вас прибудет в земли вашей, или иже аще будет в вас в родех ваших, и сотворит принос в воню благовония Господу, якоже творите вы, тако да сотворит.
15 Kutakuwa na sheria hiyo hiyo kwa watu wote na kwa mgeni anayeishi kati yenu, sheria ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Ninyi mlivyo, ndivyo atakavyokuwa mgeni aliyeishi kati yenu. Atafanya kama mnavyofanya mbele ya BWANA.
Сонме Господнь, закон един да будет вам и пришелцем прилежащым в вас, закон вечный в роды вашя: якоже вы, (тако) и пришлец да будет пред Господем:
16 Sheria na amri hiyohiyo ndiyo itakayotumika kwa mgeni anayeishi kati yenu.”
закон един да будет и оправдание едино да будет вам и пришелцу прилежащему в вас.
17 Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
18 “Nena wana wa Israeli uwaambie, 'mtakapofika katika nchi ninayowapeleka,
глаголи сыном Израилевым и речеши к ним: егда внидете в землю, в нюже Аз ввожду вас тамо,
19 mtakapokula chakula kinachozalishwa katika nchi hiyo, mtatoa sadaka ya kunipendeza mimi.
и будет егда ясте от хлебов земли (тоя), отложите участие во отделение Господу: начаток теста вашего,
20 Kutoka kwenye mikate yenu ya kwanza mtatoa mkate wa kuinuliwa kama sadaka iliyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka. Mtaiinua kwa jinsi hii.
хлеб отлучите участие оное: якоже участие от гумна,
21 Watu wa uzao wako wote wtanitolea sadaka ya kuinuliwa kutoka kwenye unga wenu wa kwanza.
тако отделите той хлеб, начаток теста вашего, и дадите Господу участие в роды вашя.
22 Wakati mwingine mtafanya dhambi pasipo kukusudia, Kama hamtatii amri zote hizi ambazo nimemwambia Musa
Егда же согрешите и не сотворите всех заповедий сих, ихже глагола Господь Моисею,
23 -kila kitu ambacho nimewaamuru kupitia Musa kuanzia siku ambayo nilianza kuwaamuru na kuendelea kwa watu wote wa uzao wako.
якоже повеле Господь Бог к вам рукою Моисеовою, от дне в оньже повеле Господь к вам, и потом в роды вашя,
24 Kwa swala la dhambi isiyokusudiwa ambayo watu wote hawaijui, basi watu wote watatoa fahari mchanga sadaka ya kuteketezwa ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Pamoja na haya yote, lazima itengenezwe sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji, kama ilivyoagaizwa katika amri, na beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
и будет аще от очес сонма сотворится неволею, и да сотворит весь сонм телца единаго непорочна от волов во всесожжение, в воню благовония Господу, и жертву сего, и возлияние его по уставлению, и козла единаго от коз греха ради:
25 Kuhani atafanya sadaka upatanisho kwa watu wote wa Israeli. Watasemehewa kwa sababu dhambi haikukusudiwa. Wametoa sadaka yao, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili yangu. Wameleta sadaka yao kwangu iliyotengenezwa kwa moto. Wameleta sadaka yao ya uovu mbele yangu kwa ajili ya kosa lao.
и да помолится жрец от всем сонме сынов Израилевых, и оставится им, яко нехотение есть: и сии принесоша дар свой, принесение Господу греха ради своего пред Господем, нехотений ради своих,
26 Ndipo watu wote wa Israeli watasamehewa, pia wageni wote wanaoishi kati yao, kwa sababu watu wote walitenda dhambi pasipo kukusudia.
и оставится всему сонму сынов Израилевых и пришелцу прилежащему в вас, яко всем людем нехотенное.
27 Kama mtu atatenda dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa umri wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
Аще же душа едина не хотящи согрешит, да приведет козу едину единолетну греха ради:
28 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa BWANA kwa ajili ya mtu yule aliyefanya dhambi pasipo kukusudia. Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika.
и да помолится жрец о души нехотевшей и согрешшей нехотением пред Господем, и да помолится о ней, и оставится ей.
29 Mtakuwa na sheria hiyohiyo kwa mtu yeyote anayefanya dhambi hiyo pasipo kukusudia, sheria hiyohiyo hata kwa mzawa wa Isreli na kwa wageni wanaoishi kati yao.
Населнику (земли) сынов Израилевых и пришелцу прилежащему в них, закон един да будет им, иже аще сотворит не хотящь.
30 Lakini mtu afanyaye chochote kwa KUkusudia, awe mzawa au mgeni, ananikufuru mimi. Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake.
И душа яже сотворит рукою гордости от туземец или от пришелцев, Бога сия разгневает, и потребится душа та от людий своих:
31 Kwa sababu atakuwa amedharau neno langu na amevunja neno amri yangu, mtu huyo ataondolewa kabisa. Dhambi yake itakuwa juu yake.'”
яко слово Господне презре и заповеди Его разсыпа, сотрением да сотрется душа та: и грех ея на ней.
32 Wakati wana wa Israeli walipokuwa katika jangwa, wakamuona mwanamume akikusanya kuni sikiu ya Sabato.
И бяху сынове Израилевы в пустыни, и обретоша мужа собирающа дрова в день субботный,
33 Wale waliomwona wakamleta kwa Musa, Haruni na kwa watu wote.
и приведоша его обретшии собирающа дрова в день субботный к Моисею и Аарону и ко всему сонму сынов Израилевых,
34 Wakamweka kifungoni kwa sababu ilikuwa haijaamuliwa atakachotendewa.
и ввергоша его в темницу: не совещаша бо, что сотворят ему.
35 Kisha BWANA akanena na Musa, “Yule mwanamume lazima auawe. Watu wote lazima wampige kwa mawe nje ya kambi.”
И рече Господь к Моисею, глаголя: смертию да умрет человек сей, да побиете его камением весь сонм вне полка.
36 Kwa hiyo watu wote wakamtoa nje ya kambi nao wakampiga kwa mawe mpaka akafa kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
И изведоша его весь сонм вне полка, и побиша его камением весь сонм вне полка, якоже глагола Господь Моисею.
37 BWANA akanena na Musa tena, akasema,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
38 “Waambie wana wa Israeli na uwaamuru wajifanyie vishada wavining'inize katika mapindo ya mavazi yao, wavining'ineze katika ncha zote kwa nyuzi za rangi ya samawi. Watu wote watafanya hivi kwa watu wote wa kizazi chote.
глаголи сыном Израилевым и речеши им: и да сотворят себе рясны на воскрилиих риз своих в роды своя: и возложите на рясны воскрилий прядение синее,
39 Huu utakuwa ukumbusho maalumu kwenu, kila mtakapovitazama, mtakumbuka amri zangu, na kuzishika ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo na macho yenu na kuwa waasherati wa hayo.
и будет вам на ряснах: и узрите их, и воспомянете вся заповеди Господни и сотворите я, и не развратитеся вслед мыслей своих и вслед очес ваших, имиже вы соблудисте вслед их:
40 Fanyeni hivi ili kwamba mweze kukumbuka na kutii amri zangu zote, na ili kwamba mpate kuwa watakatifu, waliotunzwa kwa ajili yangu, Mungu wenu.
яко да помянете и сотворите вся заповеди Моя, и будете святи Богу вашему:
41 Mimi ndimi BWANA Mungu wenu niliyekutoa toka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
Аз Господь Бог ваш, изведый вас из земли Египетския, быти вам Бог: Аз Господь Бог ваш.

< Hesabu 15 >