< Mathayo 24 >
1 Yesu alitoka hekaluni na kwenda zake. Wanafunzi wake walimwendea na kumuonesha majengo ya hekalu.
A vyšed Ježíš, bral se z chrámu. I přistoupili učedlníci jeho, aby ukázali jemu stavení chrámové.
2 Laikni aliwajibu na kuwaambia, “Je, hamuyaoni mambo haya yote? Kweli nawaambia, hakuna jiwe litalobaki juu ya lingine bila kubomolewa.”
Ježíš pak řekl jim: Vidíte-liž tyto všecky věci? Amen pravím vám: Nebude zůstaven tuto kámen na kameni, kterýž by nebyl zbořen.
3 Na alipokaa katika Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake walimwendea kwa faragha na kusema, “Tuambie, mambo haya yatatokea lini? Kitu gani kitakuwa dalili ya kuja kwako na mwisho wa ulimwengu?” (aiōn )
A když se posadil na hoře Olivetské, přistoupili k němu učedlníci soukromí, řkouce: Pověz nám, kdy to bude, a které znamení příchodu tvého a skonání světa? (aiōn )
4 Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Iweni makini kwamba asije mtu akawapotosha.
I odpověděv Ježíš, řekl jim: Vizte, aby vás někdo nesvedl.
5 Kwa kuwa wengi watakuja kwa jina langu. Watasema, 'Mimi ndiye Kristo', na watawapotosha wengi.
Nebo mnozí přijdou pod jménem mým, řkouce: Jáť jsem Kristus, a svedouť mnohé.
6 Mtasikia vita na taarifa za vita. Angalieni msije mkawa na wasiwasi, kwa kuwa mambo haya hayabudi kutokea; lakini ule mwisho utakuwa bado.
Budete slýchati zajisté boje a pověsti bojů. Hleďtež, abyste se nekormoutili; nebo musí to všecko býti; ale ne i hned bude konec.
7 Kwa kuwa taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi katika sehemu mbalimbali.
Nebo povstane národ proti národu a království proti království, a budou hladové a morové a země třesení po místech.
8 Lakini mambo haya yote ni mwanzo tu wa uchungu wa kujifungua.
Ale tyto všecky věci jsou počátkové bolestí.
9 Ndipo watawatoa kwa ajili ya mateso na kuwaua. Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.
A tehdy vydadí vás v ssoužení, a budou vás mordovati, a budete v nenávisti u všech národů pro jméno mé.
10 Ndipo wengi watajikwaa na kusalitiana na watachukiana wenyewe kwa wenyewe.
A tehdyť se zhorší mnozí, a vespolek se budou zrazovati, a jedni druhých nenáviděti.
11 Manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi.
A mnozí falešní proroci povstanou, a svedou mnohé.
12 Kwa sababu uovu utaongezeka, upendo wa wengi utapoa.
A že rozmnožena bude nepravost, ustydne láska mnohých.
13 Lakini atakaye vumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
Ale kdož by setrval až do konce, ten spasen bude.
14 Hii Injili ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu mzima kama ushuhuda kwa mataifa yote. Na ndipo ule mwisho utafika.
A bude kázáno toto evangelium království po všem světě, na svědectví všechněm národům, a tehdáž přijde skonání.
15 Kwa hiyo, mtakapoona chukizo la uharibifu, lililosemwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu [asomaye na afahamu],
Protož když uzříte ohavnost zpuštění, předpověděnou od Daniele proroka, ana stojí na místě svatém, (kdo čte, rozuměj, )
16 ndipo walioko Yuda wakimbilie milimani.
Tehdáž ti, kteříž by byli v Judstvu, nechť utekou na hory.
17 Na yule aliyeko juu ya paa la nyumba asiweze kuteremka chini kuchukua kitu chochote kutoka ndani ya nyumba yake,
A kdo na střeše, nesstupuj, aby něco vzal z domu svého.
18 naye aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
A kdo na poli, nevracuj se zase, aby vzal roucha svá.
19 Lakini ole wao ambao wana mtoto na wale ambao wananyonyesha katika siku hizo!
Běda pak těhotným a těm, kteréž kojí v těch dnech.
20 Ombeni kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
Protož modlte se, aby utíkání vaše nebylo v zimě aneb v svátek.
21 Kwa kuwa kutakuwa na dhiki kuu, ambayo haijawahi kuwapo tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, na wala haitakuwapo tena.
Nebo bude tehdáž ssoužení veliké, jakéhož nebylo od počátku světa až do té chvíle, aniž kdy potom bude.
22 Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna ambaye angeokoka. Lakini kwa sababu ya wateule, siku hizo zitafupishwa.
A byť nebyli ukráceni dnové ti, nebyl by spasen žádný člověk. Ale pro vyvolené ukráceni budou ti dnové.
23 Kisha ikiwa mtu yeyote atawaambia 'Tazama, Kristo yuko hapa! au, 'Kristo yuko kule' msiamini maneno hayo.
Tehdy řekl-li by vám kdo: Aj, tutoť jest Kristus, aneb tamto, nevěřte.
24 Kwa kuwa Makristo wa uongo na manabii wa uongo watakuja na kuonesha ishara kubwa na maajabu, kwa kusudi la kupotosha, kama ingewezekana hata na wateule.
Nebo povstanou falešní Kristové a falešní proroci, a činiti budou divy veliké a zázraky, tak že by svedli, (by možné bylo, ) také i vyvolené.
25 Tazameni, nimewatahadharisha kabla ya mambo hayo kutokea.
Aj, předpověděl jsem vám.
26 Kwa hiyo, ikiwa watawaambia, ''Kristo yuko jangwani,' msiende huko jangwani. Au, 'Tazameni, yuko ndani ya nyumba,' msiamini maneno hayo.
Protož řeknou-liť vám: Aj, na poušti jest, nevycházejte. Aj, v skrýších, nevěřte.
27 Kama vile radi inavyomulika kutokea mashariki na kuangaza hadi magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
Nebo jakož blesk vychází od východu slunce, a ukazuje se až na západ, tak bude i příchod Syna člověka.
28 Popote ulipo mzoga, huko ndiko tai wakusanyikapo.
Nebo kdežkoli bude tělo, tuť se shromáždí i orlice.
29 Lakini mara baada ya dhiki kuu ya siku zile, Jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbinguni zitatikisika.
A hned po ssoužení těch dnů slunce se zatmí, a měsíc nedá světla svého, a hvězdy budou padati s nebe, a moci nebeské budou se pohybovati.
30 Ndipo ishara ya Mwana wa Adamu itaonekana angani, na makabila yote ya dunia wataomboleza. Watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani kwa nguvu na utukufu mkuu.
Tehdážť se ukáže znamení Syna člověka na nebi, a tehdyť budou kvíliti všecka pokolení země, a uzříť Syna člověka přicházejícího na oblacích nebeských s mocí a slávou velikou.
31 Atawatuma malaika wake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.
Kterýž pošle anděly své s hlasem velikým trouby, i shromáždíť vyvolené jeho ode čtyř větrů, a od končin nebes až do končin jejich.
32 Jifunzeni somo kutokana na mti mtini. Mara tu tawi linapochipuka na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kinakaribia.
Od stromu pak fíkového naučte se podobenství tomuto: Když již ratolest jeho odmladne, a lístí se pučí, porozumíváte, že blízko jest léto.
33 Hivyo pia, mtakapoona mambo haya yote, mnapaswa kujua kwamba amekaribia, karibu na malango.
Takéž i vy, když byste uzřeli toto všecko, vězte, žeť blízko jest a ve dveřích.
34 Kweli nawaambia, kizazi hiki hakitapita, hadi mambo yote haya yatakuwa yametokea.
Amen pravím vám, že nepomine věk tento, až se tyto všecky věci stanou.
35 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Nebe a země pominou, ale slova má nikoli nepominou.
36 Lakini kuhusu siku ile na saa hakuna mtu ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, bali Baba peke yake.
O tom pak dni a hodině té žádný neví, ani andělé nebeští, jediné sám Otec můj.
37 Kama vile ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
Ale jakož bylo za dnů Noé, takť bude i příchod Syna člověka.
38 Kwa kuwa katika siku hizo kabla ya gharika watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa hadi siku ile ambayo Nuhu aliingia katika safina,
Nebo jakož za dnů těch před potopou žrali a pili, ženili se a vdávaly se, až do toho dne, když Noé všel do korábu,
39 na hawakujua kitu chochote hadi gharika ilipokuja na kuwasomba wote - ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
A nezvěděli, až přišla potopa, a zachvátila všecky: takť bude i příští Syna člověka.
40 Ndipo watu wawili watakuwa shambani- mmoja atachukuliwa, na mmoja ataachwa nyuma.
Tehdyť dva budou na poli; jeden bude vzat, a druhý zanechán.
41 Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja - mmoja atachukuliwa, na mmoja atabaki.
Dvě budou mleti ve mlýně; jedna bude vzata, a druhá zanechána.
42 Kwa hiyo, kuweni macho kwa sababu hamjui ni siku gani ambayo atakuja Bwana wenu.
Bdětež tedy, poněvadž nevíte, v kterou hodinu Pán váš přijíti má.
43 Lakini mjue kwamba, ikiwa bwana mwenye nyumba angejua ni saa ipi ambayo mwizi angekuja, angekesha na asingeruhusu nyumba yake kuvamiwa.
Toto pak vězte, že byť věděl hospodář, v které by bdění zloděj měl přijíti, bděl by zajisté, a nedal by podkopati domu svého.
44 Kwa hiyo, pia mnapaswa kuwa tayari, kwa kuwa Mwana wa Adamu atakuja katika saa msiyoitarajia.
Protož i vy buďte hotovi; nebo v tu hodinu, v kterouž se nenadějete, Syn člověka přijde.
45 Hivyo ni nani aliye mwaminifu, mtumwa mwenye akili, ambaye bwana wake amempa madaraka juu ya walio katika nyumba yake, ili awape chakula kwa wakati unaofaa?
Kdož tedy jest ten služebník věrný a opatrný, kteréhož ustanovil pán jeho nad čeledí svou, aby jim dával pokrm v čas?
46 Amebarikiwa mtumishi huyo, ambaye bwana wake atamkuta akifanya hivyo wakati ajapo.
Blahoslavený služebník ten, kteréhož přijda pán jeho, nalezl by, an tak činí.
47 Kweli nawaambia kwamba bwana atamweka juu ya kila kitu kilicho chake.
Amen pravím vám, že nade vším statkem svým ustanoví jej.
48 Lakini kama mtumwa mwovu akisema moyoni mwake, 'Bwana wangu amekawia,'
Jestliže by pak řekl zlý služebník ten v srdci svém: Prodlívá pán můj přijíti,
49 na akaanza kuwapiga watumishi wake, na akala na kulewa vileo,
I počal by bíti spoluslužebníky, jísti pak a píti s opilci:
50 Bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo haitarajii, na katika saa ambayo haijui.
Přijdeť pán služebníka toho v den, v kterýž se nenaděje, a v hodinu, v kterouž neví.
51 Bwana wake atamkata vipande viwili na kumweka katika nafasi moja sawa na wanafiki, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
I oddělíť jej, a díl jeho položí s pokrytci. Tamť bude pláč a škřipení zubů.