< Marko 8 >

1 Katika siku hizo, kulikuwa tena na umati mkubwa, na hawakuwa na chakula. Yesu akawaita wanafunzi wake akawaambia,
Around this time there was another large crowd that had nothing to eat. Jesus called the disciples together and told them,
2 “Ninauhurumia umati huu, wameendelea kuwa nami kwa siku tatu na hawana chakula.
“I feel for the crowd because they have already stayed with me for three days and they have nothing to eat.
3 Nikiwatawanya warudi majumbani kwao bila kula wanaweza wakazimia njiani kwa njaa. Na baadhi yao wametoka mbali sana.”
If I send them home without food, they'll faint on the way. Some have come from a long way away.”
4 Wanafunzi wake wakamjibu, “Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?”
“Where could anybody find enough bread to feed them here in this wilderness?” answered his disciples.
5 Akawauliza, “mna vipande vingapi vya mikate?” Wakasema, “Saba”.
“How many loaves do you have?” he asked. “Seven,” they replied.
6 Aliuamuru umati ukae chini. Akachukua mikate saba, akamshukuru Mungu, na kuivunja. Akawapa wanafunzi wake waiweke mbele yao, nao wakaiweka mbele ya umati.
He told the crowd to sit down on the ground. Then he took the seven loaves of bread, and gave thanks. He broke the bread and handed the pieces to his disciples to give to the crowd.
7 Pia walikuwa na samaki wadogo wachache, na baada ya kushukuru, aliwaamuru wanafunzi wake wawagawie hivi pia.
They had a few fish as well, so having blessed them, he said, “Take these and share them too.”
8 Walikula na wakatosheka. Na walikusanya vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba.
They ate until they were full, and then collected up seven baskets of leftovers.
9 Walikaribia watu elfu nne. Na aliwaacha waende.
There were four thousand people there. After sending them on their way,
10 Mara aliingia kwenye mashua na wanafunzi wake, na wakaenda katika ukanda ya Dalmanuta.
Jesus climbed into a boat with his disciples and went to the region of Dalmanutha.
11 Kisha Mafarisayo walitoka nje na kuanza kubishana naye. Walitaka awape ishara kutoka mbinguni, kwa kumjaribu.
The Pharisees arrived and began to argue with him, wanting him to give them a miraculous sign from heaven, trying to get him to prove himself.
12 Akatafakari kwa kina moyoni mwake akasema, “Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara? Nawaambia ninyi kweli, hakuna ishara itakayotolewa kwa kizazi hiki.”
Jesus sighed deeply, and asked, “Why do you people want a sign? I tell you the truth: I will not give you a sign.”
13 Kisha akawaacha, akaingia ndani ya mashua tena, akaondoka kuelekea upande mwingine.
So he left them behind, climbed into the boat, and went back across the lake.
14 Wakati huo wanafunzi walisahau kuchukua mikate. Hawakuwa na mikate zaidi ya kipande kimoja kilichokuwa kwenye mashua.
But the disciples had forgotten to bring bread with them. All they had in the boat was one loaf.
15 Aliwaonya na kusema, “Muwe macho na mjilinde dhidi ya chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
“Watch out—beware of the yeast of the Pharisees and of Herod!” he warned them.
16 Wanafunzi wakasemezana wao kwa wao, “Ni kwa sababu hatuna mikate.”
“He's saying that because we don't have any bread,” they concluded.
17 Yesu alilitambua hili, na akawaambia, “Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate? Hamjajua bado? Hamuelewi? Mioyo yenu imekuwa miepesi?
Jesus knew what they were saying, and said, “Why are you talking about not having any bread? Are you still not thinking and not understanding? Have you closed your minds?
18 Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?
You've got eyes to see, haven't you? And ears to hear?
19 Nilipoigawanya mikate mitano kwa watu elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?” Wakamjibu, “kumi na mbili.”
Don't you remember when I shared five loaves among five thousand? How many basketfuls of leftovers did you pick up?” “Twelve,” they replied.
20 “Na nilipoigawanya mikate saba kwa watu elfu nne, mlichukua vikapu vingapi?”
“And the seven loaves divided among four thousand. How many basketfuls of leftovers did you pick up?” “Seven,” they answered.
21 Wakasema, “Saba.” Akawaambia, “Bado hamuelewi?”
“Do you still not understand?” he asked them.
22 Wakaja Bethsaida. Watu hao walimleta kwa Yesu mtu kipofu na wakamsihi Yesu amguse.
They went to Bethsaida where some people brought a blind man to Jesus. They begged Jesus to touch him and heal him.
23 Yesu akamshika kwa mkono yule kipofu, na kumwongoza nje ya kijiji. Alipotema mate juu ya macho yake na kunyosha mikono yake juu yake, alimuuliza, “Unaona chochote?”
Jesus took the blind man by the hand and took him outside the village. Jesus spat on the man's eyes and touched him with his hands. Then Jesus asked him, “Can you see anything?”
24 Alitazama juu na kusema, “Naona watu wanaonekana kama miti inatembea.”
The man looked around, and said, “I can see people, but they look like trees walking.”
25 Ndipo akanyosha tena mikono yake juu ya macho yake, mtu yule akafungua macho yake, aliona tena, na akaona kila kitu vizuri.
So Jesus touched the man's eyes again. He could see properly—he was cured and his sight was clear.
26 Yesu alimwacha aende nyumbani na akamwambia, “Usiingie mjini.”
Jesus sent the man home, and told him, “Don't go back through the village.”
27 Yesu aliondoka na wanafunzi wake kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi. Wakiwa njiani aliwauliza wanafunzi, “Watu wanasema mimi ni nani?”
Jesus and his disciples left to go to the villages of Caesarea Philippi. On the way he asked his disciples, “Who do people say I am?”
28 Wakamjibu wakasema, “Yohana mbatizaji. Wengine wanasema, 'Eliya' na wengine, 'Mmoja wa Manabii.”
“Some say John the Baptist, some say Elijah, others say one of the prophets,” they replied.
29 Akawauliza, “Lakini ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro kamwambia, “Wewe ni Kristo.”
“But who do you say I am?” he asked them. “You are the Messiah!” Peter answered.
30 Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.
Jesus warned them not to tell anybody about him.
31 Na akaanza kuwafundisha ya kuwa Mwana wa Adamu lazima ateseke kwa mambo mengi, na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.
Then Jesus began to explain to them that the Son of man would suffer many things and be rejected by the elders, chief priests, and religious teachers. He would be killed, but three days later would rise again.
32 Alisema haya kwa uwazi. Ndipo Petro akamchukua pembeni na akaanza kumkemea.
Jesus explained this to them very clearly. But Peter took Jesus aside and started to reprimand him for what he said.
33 Lakini Yesu aligeuka na kuwatazama wanafunzi wake na akamkemea Petro na kusema, “Pita nyuma yangu Shetani! Hujali mambo ya Mungu, isipokuwa mambo ya watu.”
Jesus turned around and looking at his disciples, reprimanded Peter. “Get away from me, Satan,” he said. “You're not thinking as God thinks, but as human beings do.”
34 Kisha akauita umati na wanafunzi wake pamoja, na kuwaambia, “Kama kuna mtu anataka kunifuata, ajikane mwenyewe, achukue msalaba wake, na anifuate.
Jesus called the crowd and his disciples over to him, and told them, “If you want to follow me, you must give up on yourselves, pick up your cross and follow me.
35 Kwa kuwa yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote atakayepoteza maisha yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya injili, atayaokoa.
If you want to save your life you will lose it, but if you lose your life because of me and the good news you will save it.
36 Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?
What use is it for you to gain everything in the whole world, and lose your life?
37 Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?
What would you give in exchange for your life?
38 Yeyote anioneaye aibu na maneno yangu katika kizazi hiki cha wazinzi na kizazi cha wenye dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea aibu atakapokuja katika ufalme wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
If you're ashamed to acknowledge me and what I say among this unfaithful and sinful people, then the Son of man will be ashamed to acknowledge you when he comes with his Father's glory with the holy angels.”

< Marko 8 >