< Marko 14 >

1 Ilikuwa siku mbili tu baada ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na waandishi walikuwa wakitafuta namna ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
It was now two days before Passover and the Feast of Unleavened Bread. The chief priests and the religious leaders were trying to find a surreptitious way to arrest Jesus and have him killed.
2 Kwa kuwa walisema, “Sio wakati huu wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
“But not during Passover,” they said to themselves, “otherwise the people may riot.”
3 Wakati Yesu alipokuwa Bethania nyumbani kwa Simoni mkoma, na alipokuwa akielekea mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa na chupa ya marashi ya nardo safi yenye gharama kubwa sana, aliivunja chupa na kuimimina juu ya kichwa chake.
Meanwhile Jesus was in Bethany, eating a meal at Simon the leper's home. A woman came in with an alabaster jar of very expensive pure nard perfume. She broke the jar open and poured the perfume on Jesus' head.
4 Lakini kulikuwa na baadhi yao waliokasirika. Waliambiana wao kwa wao wakisema, “Ni nini sababu ya upotevu huu?
Some of those who were there became annoyed and said, “Why waste this perfume?
5 Manukato haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari mia tatu, na wakapewa maskini.” Nao walimkemea.
It could've been sold for a year's wages and the money given to the poor.” They were angry with her.
6 Lakini Yesu alisema, “Mwacheni peke yake. Kwa nini mnamsumbua? Amefanya jambo zuri kwangu.
But Jesus replied, “Leave her alone! Why are you criticizing her for doing something beautiful to me?
7 Siku zote maskini mnao, na wakati wowote mnapotamani mnaweza kufanya mazuri kwao, lakini hamtakuwa nami wakati wote.
You'll always have the poor with you, and you can help them whenever you want. But you won't always have me with you.
8 Amefanya kile anachoweza: ameupaka mwili wangu mafuta kwa ajili ya maziko.
She did what she could: she anointed my body in anticipation of my burial.
9 Kweli nawaambia, kila mahali injili inapohubiriwa katika ulimwengu wote, kile alichofanya mwanamke huyu kitazungumzwa kwa ukumbusho wake.
I tell you the truth: wherever the good news is spread in the world, people will remember what she did.”
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale kumi na wawili, alikwenda kwa wakuu wa makuhani ili kwamba apate kumkabidhi kwao.
Then Judas Iscariot, one of the twelve disciples, went to the chief priests and arranged to betray Jesus to them.
11 Wakati wakuu wa Makuhani waliposikia hivyo, walifurahi na wakaahidi kumpa fedha. Alianza kutafuta nafasi ya kumkabidhi kwao.
When they heard this, they were delighted, and promised to pay him. So Judas began to look for an opportunity to betray Jesus.
12 Katika siku ya kwanza ya mkate usiotiwa chachu, wakati walipotoa mwanakondoo wa pasaka, wanafunzi wake walimwambia, “Unataka twende wapi tukaandae ili upate kula mlo wa Pasaka?”
On the first day of the Feast of Unleavened Bread, the time when the Passover lamb is sacrificed, Jesus' disciples asked him, “Where do you want us to go and prepare the Passover meal for you?”
13 Aliwatuma wanafuzi wake wawili na kuwaambia, “Nendeni mjini, na mwanamume ambaye amebeba mtungi ataonana nanyi. Mfuateni.
He sent two of his disciples, telling them, “Go into the city and there you'll meet a man carrying a water pot. Follow him,
14 Nyumba atakayoingia, mfuateni na mmwambie mwenye nyumba hiyo, 'Mwalimu asema, “Kiko wapi chumba cha wageni mahali nitakapokula Pasaka na wanafunzi wangu?”
and when he goes into a house, ask the owner where I and my disciples can celebrate the Passover.
15 Atawaonesha chumba cha juu kikubwa chenye samani ambacho kiko tayari. Fanyeni maandalizi kwa ajili yetu pale.”
He will take you to a large upstairs room that is furnished and ready. You can make preparations for us there.”
16 Wanafunzi waliondoka wakaenda mjini; walikuta kila kitu kama alivyokuwa amewaambia, na wakaandaa mlo wa Pasaka.
The disciples went into the city, and found things just as he'd described them. They prepared the Passover meal.
17 Wakati ilipokuwa jioni, alikuja na wale Kumi na wawili.
In the evening Jesus went there with the twelve disciples.
18 Na walipokuwa wakiikaribia meza na kula, Yesu alisema, “Kweli nawaambia, mmoja kati yenu anayekula pamoja nami atanisaliti.”
While they were sitting eating, Jesus said, “I tell you the truth: one of you is going to betray me; one who is eating with me now.”
19 Wote walisikitika, na mmoja baada ya mwingine walimwambia, “Hakika siyo mimi?”
They were shocked, and they each asked, “It's not me, is it?”
20 Yesu alijibu na kuwaambia, “Ni mmoja wa Kumi na wawili kati yenu, mmoja ambaye sasa anachovya tonge katika bakuli pamoja nami.
“It's one of the Twelve, one of you sharing this food with me,” he replied.
21 Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakwenda kama vile maandiko yasemavyo juu yake. Lakini ole wake mtu yule ambaye kupitia yeye Mwana wa Adamu atasalitiwa! Ingekuwa vizuri zaidi kwake kama mtu yule asingezaliwa.”
“The Son of man will die, just as the Scriptures predicted. But how terrible it will be for the man who betrays the Son of man! It would be better for that man if he'd never been born.”
22 Na walipokuwa wakila, Yesu alichukua mkate, akaubariki, na kuumega. Aliwapa akisema, “Chukueni. Huu ni mwili wangu.”
As they were eating, Jesus picked up some bread. He blessed it, and gave it to them. “Take it. This is my body,” he told them.
23 Alichukua kikombe, akashukuru, na akawapatia, na wote wakakinywea.
Then he picked up the cup. He blessed it, and gave it to them. They all drank from it.
24 Aliwaambia, “Hii ni damu yangu ya agano, damu imwagikayo kwa ajili ya wengi.
“This is my blood,” he told them, “the agreement that's being poured out for many.
25 Kweli nawaambia, sitakunywa tena katika zao hili la mzabibu mpaka siku ile nitakapokunywa mpya katika ufalme wa Mungu.”
I tell you the truth, I won't drink of the fruit of the vine until the day I drink it fresh in God's kingdom.”
26 Walipokwisha kuimba wimbo, walikwenda nje katika Mlima wa Mizeituni.
After they had sung a psalm, they left for the Mount of Olives.
27 Yesu aliwaaambia, “Ninyi nyote mtajitenga mbali kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, 'Nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika.'
“All of you will abandon me,” Jesus told them. “For as the Scriptures say, ‘I will attack the shepherd, and the sheep will be completely scattered.’
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia mbele yenu Galilaya.”
But after I have risen from the dead, I will go before you to Galilee.”
29 Petro alimwambia, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
“I won't abandon you even if everyone else does,” Peter replied.
30 Yesu alimwambia, “Kweli nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utakuwa umenikana mara tatu.”
Jesus answered him, “I tell you the truth that today, this very night, before the rooster crows twice, you will deny that you even know me three times.”
31 Lakini Petro alisema, “Hata itanilazimu kufa pamoja nawe, sitakukana.” Wote walitoa ahadi ile ile.
But Peter was totally adamant, saying, “Even if I have to die with you, I will never deny you.” All of them said the same.
32 Walikuja kwenye eneo lililoitwa Gethsemane, na Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nasali.”
They arrived at a place called Gethsemane, where Jesus told his disciples, “Sit here while I go and pray.”
33 Aliwachukua Petro, Yakobo, na Yohana pamoja naye, akaanza kuhuzunika na kutaabika sana.
He took Peter, James, and John with him. He began to be very disturbed and troubled.
34 Aliwaambia, “Nafsi yangu ina huzuni sana, hata kufa. Bakini hapa na mkeshe.”
Jesus told them, “My agony is so painful it feels like I'm dying. Please, remain here and stay awake.”
35 Yesu alienda mbele kidogo, akaanguka chini, akaomba, kama ingewezekana, kwamba saa hii ingemwepuka.
He went a little farther on and then fell to the ground. He prayed, asking to be spared the time that was coming, if it were possible.
36 Alisema, “Aba, Baba, Mambo yote kwako yanawezekana. Niondolee kikombe hiki. Lakini siyo kwa mapenzi yangu, bali mapenzi yako.”
“Abba, Father! You can do everything,” he said. “Please, take this cup of suffering away from me. Yet it's not what I want, but what you want.”
37 Alirudi na kuwakuta wamelala, na akamwambia Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?
Then Jesus returned and found the disciples asleep. “Simon, are you sleeping?” he asked Peter. “Couldn't you stay awake for just an hour?
38 Kesheni na muombe kwamba msije mkaingia katika majaribu. Hakika roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Stay awake, and pray so you won't fall into temptation. The spirit is willing, but the body is weak.”
39 Alienda tena na kuomba, na alitumia maneno yaleyale.
He left them once more, and prayed, saying the same things.
40 Alikuja tena akawakuta wamelala, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito na hawakujua nini cha kumwambia.
Then he returned, and again he found them sleeping because they couldn't keep their eyes open. They didn't know what to say!
41 Alikuja mara ya tatu na kuwaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Yatosha! Saa imefika. Tazama! Mwana wa Adamu atasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
He returned a third time, and asked them, “Are you still asleep? Are you still resting? Well that's enough, because the time has come! Look, the Son of man is about to be betrayed into the hands of sinners.
42 Amkeni, twendeni. Tazama, yule anayenisaliti yuko karibu.”
Get up! Let's go! See, here comes my betrayer.”
43 Mara tu alipokuwa bado anaongea, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, alifika, na kundi kubwa kutoka kwa wakuu wa makuhani, waandishi na wazee wenye mapanga na marungu.
Just as he was saying this, Judas—one of the twelve disciples—arrived with a mob carrying swords and clubs, sent by the chief priests, religious leaders, and elders.
44 Wakati huo msaliti wake alikuwa amewapa ishara, akisema, Yule nitakayembusu, ndiye. Mkamateni na kumpeleka chini ya ulinzi.”
Now the betrayer had arranged a sign with them: “He's the one that I kiss. Arrest him, and take him away under guard.”
45 Wakati Yuda alipofika, moja kwa moja alienda kwa Yesu na kusema, “Mwalimu!” Na akambusu.
Judas went right up to Jesus. “Rabbi,” he said, and kissed him affectionately.
46 Kisha wakumtia chini ya ulinzi na kumkamata.
So they grabbed hold of Jesus and arrested him.
47 Lakini mmoja kati yao aliyesimama karibu naye alichomoa upanga wake akampiga mtumishi wa kuhani mkuu na kumkata sikio.
But one of those standing there pulled out his sword and struck the high priest's servant, cutting off his ear.
48 Yesu aliwaambia, “Mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama mnyang'anyi?
“Am I some kind of rebel that you have come to arrest me with swords and clubs?” Jesus asked them.
49 Wakati kila siku nilikuwa nanyi na nikifundisha hekaluni, hamkunikamata. Lakini hili limefanyika ili maandiko yatimie.
“I was there with you, teaching in the Temple every day. Why didn't you arrest me then? But this is happening to fulfill the Scriptures.”
50 Na wale wote waliokuwa na Yesu walimwacha na kukimbia.
Then all Jesus' disciples deserted him and ran away.
51 Kijana mmoja alimfuata, aliyekuwa amevaa shuka tu aliyokuwa amejifunika kumzunguka; walimkamata lakini
(One of his followers was a young man who was wearing only a linen garment.
52 aliwaponyoka akaiacha shuka pale akakimbia uchi.
They seized hold of him, but he ran off naked, leaving the garment behind.)
53 Walimwongoza Yesu kwa kuhani mkuu. Pale walikusanyika pamoja naye makuhani wakuu wote, wazee, na waandishi.
They took Jesus to the high priest's house where all the chief priests, elders, and religious teachers had gathered.
54 Petro naye alimfuata Yesu kwa mbali, kuelekea kwenye ua wa kuhani mkuu. Aliketi pamoja na walinzi, waliokuwa karibu na moto wakiota ili kupata joto.
Peter followed him at a distance, and went into the courtyard of the high priest's house. He sat down with the guards and warmed himself by the fire.
55 Wakati huo makuhani wakuu wote na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumwua. Lakini hawakuupata.
Inside the chief priests and the whole governing council were trying to find some evidence to have Jesus put to death, but they couldn't find anything.
56 Kwa kuwa watu wengi walileta ushuhuda wa uongo dhidi yake, lakini hata ushahidi wao haukufanana.
Many were giving false testimony against him, but their statements didn't agree.
57 Baadhi walisimama na kuleta ushahidi wa uongo dhidi yake; wakisema,
Some of them got up to speak falsely against Jesus.
58 “Tulimsikia akisema, 'Nitaliharibu hekalu hili lililotengenezwa kwa mikono, na ndani siku tatu nitajenga lingine lisilotengenezwa kwa mikono.'”
“We heard him say, ‘I will destroy this Temple that human hands built, and in three days I will build another without hands.’”
59 Lakini hata ushahidi wao haukufanana.
But even so their testimony didn't agree.
60 Kuhani mkuu alisimama katikati yao na akamwuliza Yesu, “Je, huna jibu? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
Then the high priest stood up in front of the council, and asked Jesus, “Have you nothing to say in response to these charges made against you?”
61 Lakini alikaa kimya na hakujibu chochote. Mara Kuhani mkuu alimwuliza tena, “Je wewe ni Kristo, mwana wa Mbarikiwa?”
But Jesus remained silent and didn't answer. So the high priest asked again, “Are you the Messiah, the Son of the Blessed One?”
62 Yesu alisema, “Mimi ndiye. Na utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wa nguvu akija na mawingu ya mbinguni.”
“I am,” Jesus replied, “and you will see the Son of man sitting on the right of the Mighty One, and coming with the clouds of heaven.”
63 Kuhani mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Je, bado tunahitaji mashahidi?
The high priest tore his clothes and asked, “Why do we need any more witnesses?
64 Mmesikia kufuru. Uamuzi wenu ni upi?” Na wote walimhukumu kama mmoja aliyestahili kifo.
You have heard the blasphemy! What's your reaction?” They all found him guilty and condemned him to death.
65 Baadhi wakaanza kumtemea mate na kumfunika uso na kumpiga na kumwambia, “Tabiri!” Maafisa walimchukua na kumpiga.
Then some of them began to spit on him. They blindfolded him, hit him with their fists, and said, “Why don't you prophesy then, you ‘Prophet’!” The guards took him away and beat him up.
66 Na Petro alipokuwa bado yuko chini uani, mtumishi mmoja wa wasichana wa kuhani mkuu alikuja kwake.
Meanwhile Peter was down below in the courtyard. One of the high priest's servant-girls passed by,
67 Alimwona Petro alipokuwa amesimama akiota moto, na alimtazama kwa kumkaribia. Kisha alisema, “Nawe pia ulikuwa na Mnazareti, Yesu”.
and seeing Peter warming himself, looked straight at him and said, “You were with Jesus of Nazareth too!”
68 Lakini alikataa, akisema, “Sijui wala sielewi kuhusu kile unachosema!” Kisha alitoka akaenda nje uani. (Zingatia; Mstari huu, “Na jogoo akawika” haumo kwenye nakala za kale).
But he denied it. “I don't know what you're talking about or what you mean,” he replied. Then he went out to the forecourt, and a rooster crowed.
69 Lakini mtumishi wa kike pale, alimwona na alianza kuwaambia tena wale ambao walikuwa wamesimama pale, “Mtu huyu ni mmoja wao!”
Seeing him there, the servant girl repeated to those standing around, “This man is one of them!”
70 Lakini alikana tena. Baadaye kidogo wale waliokuwa wamesimama pale walikuwa wakimwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya.”
Once more Peter denied it. A little while later they said to Peter again, “You're definitely one of them because you're a Galilean too!”
71 Lakini alianza kujiweka mwenyewe chini ya laana na kuapa, “Simjui mtu huyu mnayemsema.”
Peter began calling down curses on himself and he swore, “I don't know this man who you're talking about.”
72 Kisha jogoo aliwika mara ya pili. Kisha Petro alikumbuka maneno ambayo Yesu aliyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Na alianguka chini na kulia.
Immediately the rooster crowed the second time. Then Peter remembered what Jesus had said to him: “Before the rooster crows twice, you will deny me three times.” When he realized what he'd done, he burst into tears.

< Marko 14 >