< Marko 11 >

1 Wakati huo walipokuja Yerusalemu, walipokaribia Besthfage na Bethania, katika Mlima wa Mizeituni, Yesu aliwatuma wawili miongoni mwa wanafunzi wake
And when they drew near to Jerusalem to Bethphage and Bethany near the Mount of Olives, He sends two of the disciples of Him
2 na aliwaambia, “Nendeni katika kijiji kinachokabiliana nasi. Mara mtakapoingia humo, mtamkuta mwanapunda ambaye hajapandwa. Mfungueni na mmlete kwangu.
and says to them; do go into the village before you; and immediately entering into it you will find a colt tied upon which no [one] (not yet *NO*) a person (sat; do untie *N(k)O*) it (also *no*) (do lead [it]. *N(k)O*)
3 Na kama yeyote akiwaambia, 'Kwa nini mnafanya hivi'?, mnapaswa kusema, 'Bwana anamhitaji na mara atamrudisha hapa'.”
And if anyone to you may say; Why are you doing this?’ do say (that *ko*) the Lord of it need has, and soon it (He sends *N(k)O*) (back *no*) here.
4 Walikwenda na kumkuta mwanapunda amefungwa nje mlangoni kwenye mtaa ulio wazi, nao walimfungua.
(and *no*) they departed (now *k*) and found (the *k*) colt tied at (the *k*) door outside by the street and they untied it.
5 Na baadhi ya watu walikuwa wamesimama pale na waliwaambia, “Mnafanya nini, kumfungua mwanapunda huyo?”
And some of those there having stood they were saying to them; What are you doing untying the colt?
6 Waliwaambia kama Yesu alivyowaambia, na watu wakawaacha waende.
And they spoke to them even as (had commanded *N(k)O*) Jesus, and they allowed them.
7 Wanafunzi wawili walimleta mwanapunda kwa Yesu na walitandika mavazi yao juu yake ili Yesu aweze kumpanda.
And (they lead *N(k)O*) the colt to Jesus and (they do cast *N(k)O*) upon it the cloaks of them, and He sat on (it. *N(k)O*)
8 Watu wengi wakatandika mavazi yao barabarani, na wengine wakatandika matawi waliyoyakata kutoka mashambani.
(And *no*) many (now *k*) the cloaks of them spread on the road, others then branches (cutting down *N(k)O*) from the (fields *N(K)O*) (and were spreading into way. *K*)
9 Wale waliokwenda mbele yake na wale waliomfuata walipiga kelele, “Hosana! Amebarikiwa anayekuja kwa jina la Bwana.
And those going before and those following were crying out (saying: *k*) Hosanna! Blessed [is] the [One] coming in [the] name of [the] Lord!
10 Ubarikiwe ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi! Hosana kwa aliye juu”
Blessed [is] the coming kingdom (in name of the Lord *K*) of the father of us David! Hosanna in the highest!
11 Ndipo Yesu aliingia Yerusalemu na alikwenda hekaluni na alitazama kila kitu. Sasa, wakati ulikuwa umeenda, alikwenda Bethania pamoja nao kumi na wawili.
And He entered into Jerusalem (Jesus and *k*) into the temple, and having looked around on all things, (when late [evening] *NK(o)*) already being the hour, He went out to Bethany with the Twelve.
12 Siku iliyofuata, wakati walipokuwa wakirudi kutoka Bethania, alikuwa na njaa.
And on the next day when were exiting they from Bethany He was hungry.
13 Na akaona mti wa mtini uliokuwa na majani kwa mbali, alikwenda kutazama kama angeweza kupata chochote juu yake. Na wakati alipokwenda kwa huo, hakupata chochote isipokuwa majani, kwa kuwa haikuwa majira ya mtini.
And having seen a fig tree (from *no*) afar having leaves He went if perhaps anything He will find on it. And having come to it no [thing] He found only except leaves; (the *no*) for season not it was of figs.
14 Aliuambia, “Hakuna yeyote atakayekula tunda kutoka kwako tena”. Na wanafunzi wake wakasikia. (aiōn g165)
And answering (Jesus *k*) He said to it; No more to the age from you no one fruit would eat. And were listening the disciples of Him. (aiōn g165)
15 Walikuja Yerusalemu, naye aliingia hekaluni na kuanza kuwatoa nje wauzaji na wanunuzi ndani ya hekalu. Alizipindua meza za wabadilishaji wa fedha na viti vya wale waliokuwa wakiuza njiwa.
And they come to Jerusalem, And having entered (Jesus *k*) into the temple He began to cast out those selling and (those *no*) buying in the temple, and the tables of the money changers and the seats of those selling the doves He overturned
16 Hakumruhusu yeyote kubeba chochote hekaluni kilichoweza kuuzwa.
And not He was permiting that anyone may carry a vessel through the temple.
17 Aliwafundisha na akasema, “Je haikuandikwa, 'nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote'? Lakini mmeifanya pango la wanyang'anyi”.
And He was teaching (and *no*) (was saying *N(k)O*) to them; Surely it has been written that The house of Mine a house of prayer will be called for all the nations’? You yourselves however (have made *N(k)O*) it a den of robbers.’
18 Makuhani wakuu na waandishi walisikia alivyokuwa amesema, nao walitafuta njia ya kumwua. Hata hivyo walimwogopa kwa sababu umati ulishangazwa na mafundisho yake.
And heard [it] the chief priests and the scribes and they were seeking how Him (they may destroy; *N(k)O*) they were afraid of for Him, all (for *N(k)O*) the crowd was astonished at the teaching of Him.
19 Na kila wakati jioni ilipofika, waliondoka mjini.
And (when *N(k)O*) evening came, (they were going *N(k)O*) out of the city.
20 Walipokuwa wakitembea asubuhi, waliuona mti wa mtini umekauka mpaka kwenye mizizi yake.
And passing by in the morning they saw the fig tree dried up from [the] roots.
21 Petro alikumbuka na kusema, “Rabi! Tazama, mti wa mtini ulioulaani umekauka”.
And having remembered Peter says to Him; Rabbi, look the fig tree that You cursed has been dried up.
22 Yesu aliwajibu, “Muwe na imani katika Mungu.
And answering Jesus says to them; do have faith from God.
23 Amini nawaambia kwamba kila auambiaye mlima huu, 'Ondoka, na ukajitupe mwenyewe baharini, 'na kama hana mashaka moyoni mwake lakini anaamini kwamba alichokisema kitatokea, hivyo ndivyo Mungu atakavyofanya.
Amen (for *ko*) I say to you that who[ever] maybe may say to the mountain this; do be taken away and do be cast into the sea,’ and not may doubt in the heart of him but (may believe *N(k)O*) that (what he says *N(k)O*) takes place, it will be done for him (what maybe he shall say. *K*)
24 Kwa hiyo ninawaambia: kila kitu muombacho na kuuliza kwa ajili yake, aminini kwamba mmepokea, navyo vitakuwa vyenu.
Because of this I say to you; all things as much as (when *k*) (praying *N(k)O*) (and *no*) (you ask, *NK(o)*) do believe that (you receive, *N(k)O*) and it will be to you.
25 Wakati mnaposimama na kuomba, mnapaswa kusamehe chochote mlichonacho dhidi ya yeyote, ili kwamba Baba yenu aliye mbinguni awasamehe pia ninyi makosa yenu.
And when (you stand *N(k)O*) praying, do forgive if anything you have against anyone so that also the Father of you who [is] in the heavens may forgive you the trespasses of you.
26 (Zingatia: Mstari huu, “Lakini msiposamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatasamehe dhambi zenu” haumo kwenye nakala za kale).
(if *KO*) (now you yourselves not do you allow nor the father of you in to the heavens will forgive the trespasses of you *K*)
27 Walikuja Yerusalemu tena. Na Yesu alipokuwa akitembea hekaluni, makuhani wakuu, waandishi na wazee walikuja kwake.
And they come again to Jerusalem; And in the temple when is walking He they come to Him the chief priests and the scribes and the elders
28 Walimwambia, “Kwa mamlaka gani unafanya mambo haya?” Na ni nani aliyekupa mamlaka kuyafanya haya?”
And (they were saying *N(k)O*) to Him; By what authority these things are You doing (Or *N(k)O*) who You gave authority this that these things You may do?
29 Yesu aliwaambia, “Nitawauliza swali moja. Niambieni na mimi nitawaambia kwa mamlaka gani ninayafanya mambo haya.
And Jesus (answering *k*) said to them; I will ask you (I myself also I myself also *KO*) one question, and do answer Me, and I will tell you by what authority these things I do.
30 Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au ulitoka kwa wanadamu? Nijibuni.”
The baptism (*no*) of John from heaven was it or from men? do answer Me.
31 Walijadiliana miongoni mwao na kushindana na kusema, “Kama tukisema, 'Kutoka mbinguni,' atasema, 'Kwa nini basi hamkumwamini?'
And (they were reasoning *N(k)O*) with themselves saying; (What may we say? *O*) If we shall say; From heaven, He will say; Because of why then not did you believe in him?
32 Lakini kama tukisema, 'Kutoka kwa wanadamu,'...” Waliwaogopa watu, kwa kuwa wote walishikilia kwamba Yohana alikuwa Nabii.
But (if *k*) shall we say; From men’, they were afraid of the (crowd; *N(k)O*) all for were holding John truly that a prophet he was.
33 Ndipo walimjibu Yesu na kusema, “Hatujui. Ndipo Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani nayafanya mambo haya.
And answering to Jesus they say: Not do we know. And Jesus (answering *k*) says to them; Neither I myself tell you by what authority these things I do.

< Marko 11 >