< Marko 10 >

1 Yesu aliondoka eneo hilo na akaenda katika mkoa wa Uyahudi na eneo la mbele ya Mto Yorodani, na makutano walimfuata tena. Aliwafundisha tena, kama ilivyokuwa kawaida yake kufanya.
And from there having risen up He comes into the region of Judea (and *N(k)O*) (*k*) beyond the Jordan, And come together again crowds to Him, and as He had been accustomed again He was teaching them.
2 Na Mafarisayo walikuja kumjaribu na wakamuuliza, “Ni halali kwa mwanamume kuachana na mke wake?”
And having come to [him] (the *k*) Pharisees (were questioning *N(k)O*) Him if it is lawful for a husband a wife to divorce testing Him.
3 Yesu akawajibu, “Musa aliwaamuru nini?”
And He answering said to them; What you did command Moses?
4 Wakasema, “Musa aliruhusu kuandika cheti cha kuachana na kisha kumfukuza mwanamke.”
And they said; Permitted Moses a roll of divorce to write and to send [her] away.
5 “Ni kwa sababu ya mioyo yenu migumu ndiyo maana aliwaandikia sheria hii,” Yesu aliwaambia.
(and answering *k*) (But *no*) Jesus said to them; Because of the hardness of heart of you He wrote for you commandment this;
6 “Lakini kutoka mwanzo wa uumbaji, 'Mungu aliwaumba mwanamume na mwanamke.'
From however [the] beginning of creation Male and female He made them’ (*k*) (God; *K*)
7 Kwa sababu hii mwanamume atamwacha baba yake na mama yake na ataungana na mke wake,
On account of this will leave a man the father of him and mother and will be joined to wife of him,
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; Kwa kuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
and will be the two for flesh one’ Therefore no longer no longer they are two but one flesh.
9 Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
What therefore God has joined together, man not should separate.
10 Walipokuwa ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamwuliza tena kuhusu hili.
And (in the house *N(k)O*) again the disciples (of it *k*) concerning (the [meaning] of *k*) (this were questioning *N(k)O*) Him.
11 Akawaambia, “Yeyote amwachaye mke wake na kumwoa mwanamke mwingine, anafanya uzinzi dhidi yake.
And He says to them; Who[ever] (maybe *N(k)O*) shall divorce the wife of him and shall marry another, commits adultery against her.
12 Mwanamke naye akimwacha mme wake na kuolewa na mwanamme mwingine, anafanya uzinzi.”
And if (she *N(K)O*) (having divorced *N(k)O*) the husband of her (and *k*) (shall marry another, *N(k)O*) she commits adultery.
13 Nao walimletea watoto wao wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.
And they were bringing to Him little children that them He may touch; But the disciples (rebuked those *N(k)O*) (bringing [them]. *KO*)
14 Lakini Yesu alipotambua hilo, hakufurahishwa nalo kabisa akawaambia, “Waruhusuni watoto wadogo waje kwangu, na msiwazuie, kwa sababu walio kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
Having seen now Jesus was indignant and He said to them; do permit the little children to come to Me, (and *k*) not do hinder them! To the for sof uch belongs the kingdom of God.
15 Ukweli nawaambia, yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hakika hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
Amen I say to you, who[ever] (only *N(k)O*) unless shall receive the kingdom of God as a child, certainly not shall enter into it.
16 Kisha akawachukua watoto mikononi mwake na akawabariki akiwawekea mikono yake juu yao.
And having embraced them (he was greatly blessing *N(k)O*) having laid the hands on them.
17 Na alipoanza safari yake mtu mmoja alimkimbilia na akapiga magoti mbele yake, akamwuliza, “Mwalimu Mwema, nifanye nini ili niweze kurithi uzima ya milele?” (aiōnios g166)
And when is going forth He on [the] journey having run up one and he having knelt down to Him he was asking Him; Teacher good, what shall I do that life eternal I may inherit? (aiōnios g166)
18 Na Yesu akasema, “Kwa nini unaniita mwema? Hakuna aliye mwema, isipokuwa Mungu peke yake.
And Jesus said to him; Why Me you call good? No [one is] good only except one God.
19 Unazijua amri: 'Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, mheshimu baba na mama yako'.”
The commandments you know: Not shall you murder not shall you commit adultery not shall you steal, not shall you bear false witness, not shall you defraud, do honor the father of you and the mother.’
20 Mtu yule akasema, “Mwalimu, haya yote nimeyatii tangu nikiwa kijana.”
And (answering *ko*) (he was saying *N(k)O*) to Him; Teacher, these all I have kept from [the] youth of me.
21 Yesu alimwangalia na kumpenda. Akawambia, “Unapungukiwa kitu kimoja. Unapaswa kuuza vyote ulivyo navyo na uwape masikini, na utakuwa na hazina mbinguni. Ndipo uje unifuate.”
And Jesus having looked upon him He loved him and He said to him; One thing (to you *N(k)O*) is lacking; do go, as much as you have do sell and do give to the poor and you will have treasure in heaven. and come, do follow Me (having taken up cross. *K*)
22 Lakini alikata tamaa kwa sababu ya maelezo haya; aliondoka akiwa mwenye huzuni, kwa kuwa alikuwa na mali nyingi.
And having been sad at the word he went away grieving; he was [one] for having possessions many.
23 Yesu akatazama pande zote na kuwaambia wanafunzi wake, “Ni jinsi gani ilivyo vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu!
And having looked around Jesus says to the disciples of Him; How difficultly those riches having into the kingdom of God will enter!
24 Wanafunzi walishangazwa kwa maneno haya. Lakini Yesu akawaambia tena, “Watoto, ni jinsi gani ilivyo vigumu kuingia katika ufalme wa Mungu!
And the disciples were astonished at the words of Him. But Jesus again answering He says to them; Children, how difficult it is (having trusted upon *KO*) (*K*) (riches *KO*) into the kingdom of God to enter!
25 Ni rahisi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano, kuliko mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”
Easier it is [for] a camel through the eye of the needle (to pass *N(k)O*) than [for] a rich man into the kingdom of God to enter.
26 Walishangazwa sana na wakasemezana, “Hivyo nani ataokoka”
And exceedingly they were astonished saying among (themselves; *NK(O)*) Then who is able to be saved?
27 Yesu akawaangalia na kusema, “Kwa binadamu haiwezekani, lakini sio kwa Mungu. Kwa kuwa katika Mungu yote yanawezekana.”
Having looked (now *k*) on them Jesus says; With men [it is] impossible but not [is impossible] with (*k*) God; all things for [are] possible (is *k*) with God.
28 “Petro akaanza kuzungumza naye, “Angalia tumeacha vyote na tumekufuata.”
(and *k*) Began to say Peter to Him; Behold we ourselves left all and (have followed *N(k)O*) You.
29 Yesu akasema, “Ukweli nawaambia ninyi, hakuna aliyeacha nyumba, au kaka, au dada, au mama, au baba, au watoto, au ardhi, kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Injili,
(answering *ko*) (now *k*) (Was saying *N(k)O*) Jesus; Amen I say to you, no [one] there is who has left house or brothers or sisters or mother or father (or wife *K*) or children or lands because of me and (because *no*) of the gospel,
30 ambaye hatapokea mara mia zaidi ya sasa hapa duniani: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, na ardhi, kwa mateso, na ulimwengu ujao, uzima wa milele. (aiōn g165, aiōnios g166)
only unless shall take a hundredfold now in time this — houses and brothers and sisters and (mothers *NK(o)*) and children and lands with persecutions — and in the age which is coming life eternal. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
Many however will be first last and the last first.
32 Walipokuwa njiani, kwenda Yerusalemu, Yesu alikuwa amewatangulia mbele yao. Wanafunzi walishangaa, na wale waliokuwa wanafuata nyuma waliogopa. Ndipo Yesu akawatoa pembeni tena wale kumi na wawili na akaanza kuwaambia ambacho kitamtokea hivi karibuni:
They were then on the way going up to Jerusalem, and was going on before them Jesus, and they were astonished; (those *no*) (then *N(k)O*) following were afraid. And having brought to [Himself] again the Twelve He began them to tell the [things] are being soon to Him to happen
33 “Tazama, tunakwenda mpaka Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atafikishwa kwa makuhani wakuu na waandishi. Watamhukumu afe na watamtoa kwa watu wa Mataifa.
that Behold we go up to Jerusalem, and the Son of Man will be betrayed to the chief priests and to the scribes, and they will condemn Him to death and will betray Him to the Gentiles
34 Watamdhihaki, watamtemea mate, watampiga fimbo, na watamwua. Lakini baada ya siku tatu atafufuka.”
And they will mock Him and will spit upon Him and will flog Him and will kill (him *ko*) and (on [the] third day *N(k)O*) He will rise again.
35 Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walikuja kwake na kusema, “Mwalimu, tunakuhitaji utufanyie chochote tukuombacho.”
And come up to Him James and John, the (two *O*) sons of Zebedee, saying (to Him; *no*) Teacher, we desire that whatever if we shall ask (you *no*) You shall do for us.
36 Aliwaambia, “Mnataka niwatendee nini?”
And He said to them; What do you desire Me (I may do *N(k)O*) for you?
37 Wakasema, “Turuhusu tukae nawe katika utukufu wako, mmoja katika mkono wako wa kuume na mwingine mkono wako wa kushoto.”
And they said to Him; do grant to us that one of [us] at right [hand] and one at (left [hand] *N(k)O*) (of you *k*) let us sit in the glory of You.
38 Lakini Yesu aliwajibu, “Hamjui mnachoomba. Mnaweza kukinywea kikombe ambacho nitakiywea au kustahimili ubatizo ambao nitabatizwa?”
And Jesus said to them; Not you know what you ask. Are you able to drink the cup which I myself drink (or *N(k)O*) the baptism which I myself am baptized to be baptized [with]?
39 Wakamwambia, “Tunaweza” Yesu akawaambia, “Kikombe nitakachokinywea, mtakinywea. Na ubatizo ambao kwao nimebatizwa, mtaustahimili.
And they said to Him; We are able. And Jesus said to them; The (indeed *k*) cup which I myself drink you will drink, and the baptism which I myself am baptized you will be baptized [with];
40 Lakini atakayekaa mkono wangu wa kuume au mkono wangu wa kushoto sio mimi wa kutoa, lakini ni kwa wale ambao kwao imekwisha andaliwa.”
but to sit at [the] right hand of Me (or *N(k)O*) at [the] left hand (of me *k*) not is Mine to give but [to those] for whom it has been prepared.
41 Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia haya, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
And having heard [this] the ten began to be indignant about James and John.
42 Yesu akawaita kwake na kusema, “Mnajua kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala, na watu wao mashuhuri huwaonyesha mamlaka juu yao.”
(*k*) (And *no*) (now *k*) having called near them Jesus says to them; You know that those being accounted to rule over the Gentiles exercise lordship over them, and those great ones of them exercise authority over them.
43 Lakini haipaswi kuwa hivi kati yenu. Yeyote atakaye kuwa mkubwa kati yenu lazima awatumikie,
Not thus however (is it *N(k)O*) among you, Instead who[ever] (maybe *N(k)O*) shall desire great to become among you, will be your servant;
44 na yeyote atakaye kuwa wa kwanza kati yenu ni lazima awe mtumwa wa wote.
and who[ever] (maybe *NK(o)*) shall desire (among *no*) (you to become *N(k)O*) first, will be of all slave.
45 Kwa kuwa Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa bali kutumika, na kuyatoa maisha yake kuwa fidia kwa wengi.”
Even for the Son of Man not came to be served but to serve and to give the life of Him [as] a ransom for many.
46 Wakaja Yeriko. Alipokuwa akiondoka Yeriko na wanafunzi wake na kundi kubwa, mwana wa Timayo, Batimayo, kipofu mwombaji, alikaa kando ya barabara.
And they come to Jericho. And when was going out He from Jericho — and the disciples of Him and a crowd large — (the *no*) son of Timaeus Bartimaeus, (the *k*) blind (beggar, *N(k)O*) was sitting beside the road.
47 Aliposikia kuwa ni Yesu Mnazareti, alianza kupiga kelele na kusema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And having heard that Jesus (of Nazareth *N(k)O*) it is, he began to cry out and to say; (O *k*) Son of David Jesus, do have mercy on me.
48 Wengi walimkemea yule kipofu, wakimwambia anyamaze. Lakini alilia kwa sauti zaidi, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
And were rebuking him many that he may be silent. but much more he was crying out; Son of David, do have mercy on me.
49 Yesu alisimama na kuamuru aitwe. Walimwita yule kipofu, wakisema, “Kuwa shujaa! Inuka! Yesu anakuita.”
And having stopped Jesus commanded: (do call *N(k)O*) him. And they call the blind [man] saying to him; take courage! (do rise up *N(k)O*) He calls you.
50 Akalitupa pembeni koti lake, akakimbia zaidi, na kuja kwa Yesu.
And having cast away the cloak of him (having jumped up *N(k)O*) he came to Jesus.
51 Yesu akamjibu na kusema, “Unataka nikufanyie nini?” Yule mwanaume kipofu akamjibu, “Mwalimu, ninataka kuona.”
And answering to him Jesus (said; *N(k)O*) What to you do you desire I may do And the blind [man] said to Him; Rabboni, that I may receive sight.
52 Yesu akamwambia, “Nenda. Imani yako imekuponya.” Hapo hapo macho yake yakaona; na akamfuata Yesu barabarani.
(And *no*) (now *ko*) Jesus said to him; do go, the faith of you has healed you. And immediately he received sight and he was following (Him *N(k)O*) (Jesus *k*) on the way.

< Marko 10 >