< Luka 7 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kila kitu alichokuwa anasema kwa watu waliomsikiliza, akaingia Kapernaumu.
When He completed all His words in the ears of the people, He came into Capernaum.
2 Mtumwa fulani wa akida, aliyekuwa wa thamani sana kwake, alikuwa mgonjwa sana na alikuwa karibu ya kufa.
And the servant of a certain centurion, being sick, was about to die, who was precious to him.
3 Lakini akiwa amesikia kuhusu Yesu, yule Akida alimtuma kiongozi wa kiyahudi, kumwomba aje kumwokoa mtumwa wake ili asife.
And hearing about Jesus, he sent elders of the Jews to Him, asking Him that having come He may save his servant.
4 Walipofika karibu na Yesu, walimsihi kwa bidii na kusema, “anastahili kwamba unapaswa kufanya hivi kwa ajili yake,
And they, having come to Jesus, continued to entreat Him earnestly, saying, That he to whom He will do this is worthy:
5 kwa sababu analipenda taifa letu, na ndiye aliyejenga sinagogi kwa ajili yetu”.
for he loves our race, and himself built for us a synagogue.
6 Yesu akaendelea na safari yake pamoja nao. lakini kabla hajaenda mbali na nyumba, afisa mmoja aliwatuma marafiki zake kuzungumza naye. “Bwana, usijichoshe mwenyewe kwa sababu mimi sistahili wewe kuingia kwenye dari yangu.
And Jesus went along with them. And already He being not far from the house, the centurion sent friends to Him, saying to Him, Lord, be not troubled: for I am not worthy that you may come in under my roof:
7 Kwa sababu hii sikufikiria hata mimi mwenyewe kuwa ninafaa kuja kwako, lakini sema neno tu na mtumishi wangu atapona.
Therefore I did not count myself worthy to come to thee; but speak the word, and my servant shall be healed.
8 Kwani mimi pia ni mtu niliyewekwa kwenye mamlaka na nina askari chini yangu. Husema kwa huyu “Nenda” na huenda, na kwa mwingine, “Njoo” naye huja, na kwa mtumishi wangu 'Fanya hiki', na yeye hufanya”.
For I am also a man placed under authority, having soldiers under me: and I say to this one, Go, and he goeth; and to another, Come, and he cometh; and to my servant, Do this, and he doeth it.
9 Yesu aliposikia haya alishangaa, na kuwageukia makutano waliokuwa wanamfuata na kusema.”Nawaambia, hata katika Israeli, sijawahi kuona mtu mwenye imani kuu kama huyu.
And Jesus, having heard these words, was astonished at him, and turning to the multitude following said, I say unto you, I did not find so great faith in Israel.
10 Kisha wale waliokuwa wametumwa walirudi nyumbani na kumkuta mtumishi akiwa mzima.
And those having been sent, returning to the house, found the servant well.
11 fulani baada ya haya, ilitokea kuwa Yesu alikuwa anasafiri kwenda mji ulioitwa Naini. wanafunzi wake wakaenda pamoja naye wakiambana na umati wa watu.
And it came to pass consecutively, He departed into a city called Nain; and His many disciples and a great multitude went along with Him.
12 Alipofika karibu na Lango la jiji tazama, mtu aliyekufa alikuwa amebebwa, na ni mtoto wa pekee kwa mama yake. aliyekuwa mjane, na umati wa wawakilishi kutoka kwenye jiji walikuwa pamoja naye.
And when He drew nigh unto the gate of the city, behold, a dead man, an only born son to his mother, and she a widow, was indeed being carried out: and a great multitude of the city was along with her.
13 Alipomwona, Bwana akamsogelea kwa huruma kubwa sana juu yake na akamwambia, “Usilie”.
And the Lord seeing her, was moved with compassion towards her, and said to her, Weep not.
14 Kisha akasogea mbele akaligusa jeneza ambalo walibebea mwili, na wale waliobeba wakasimama akasema “Kijana nasema amka”
And having come forward He touched the bier: and the pall-bearers stood still: and He said, Young man, I say unto thee, Arise.
15 Mfu akainuka na kukaa chini na akaanza kuongea. Kisha Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
And the dead man sat up, and began to talk, and Ile gave him to his mother.
16 Kisha hofu ikawajaa wote. wakaendelea kumtukuza Mungu wakisema “Nabii mkuu ameinuliwa miongoni mwetu” na “Mungu amewaangalia watu wake”
And fear seized them all: and they continued to glorify God, saying that, A great prophet has arisen among us: and, God has looked upon His people.
17 Hizi habari njema za Yesu zilienea Yudea yote na kwa mikoa yote ya jirani.
And that word about Him went out in all Judea, and all the country round about.
18 Wanafunzi wa Yohana walimwamwambia mambo haya yote.
And His disciples proclaimed to John concerning all these things.
19 Ndipo Yohana akawaita wawili wa wanafunzi wake na kuwatuma kwa Bwana kusema “Wewe ndiye yule ajaye, au kuna mtu mwingine tumtazamie?
And John calling certain two of his disciples sent them to the Lord, saying, Art thou the one coming, or must we expect another?
20 Walipofika karibu na Yesu hawa wakasema, “Yohana mbatizaji ametutuma kwako kusema, 'Wewe ni yule ajaye au kuna mtu mwingine tumtazamie?”
And the men having come to Him, said; John the Baptist sent us to thee, saving; Art thou the one coming, or must we expect another?
21 kwa wakati huo aliowaponya watu wengi kutoka katika magonjwa na mateso, kutoka kwa roho wachafu, na kwa watu wenye upofu aliwapa kuona.
And at that hour He healed many of their diseases and ailments and evil spirits; and He conferred on many blind people the power to see.
22 Yesu akajibu na kusema kwao. “Baada ya kuwa mmekwenda mlikotoka mtamjulisha Yohana mlichokiona na kukisikia. Wenye upofu wanapokea kuona na viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na kuwa hai tena, masikini wanaambiwa habari njema.
And Jesus responding said to them, Having gone, proclaim to John those things which you saw and heard; that the blind are seeing, the lame are walking about, the lepers are being cleansed, the deaf are hearing, the dead are being raised up, the poor are having the gospel preached unto them;
23 Na mtu ambaye hataacha kuniamini mimi kwa sababu ya matendo yangu amebarikiwa”.
and happy is he whosoever may not be offended in me.
24 Baada ya wale waliotumwa na Yohana kurudi walikotoka, Yesu akaanza kusema kwa makutano juu ya Yohana, “Mlikwenda nje kuona nini, mwanzi ukiwa unatikiswa na upepo?
And the messengers of John having gone away, He began to speak to the multitudes concerning John, What went ye out into the wilderness to see? a reed shaken by the wind?
25 lakini mlikwenda nje kuona nini, mtu aliyevaa vizuri? tazama watu wale wanaovaa mavazi ya kifalme na kuishi maisha ya starehe wako kwenye nafasi za wafalme.
But what went you out into the wilderness to see? a man clothed in soft raiment? Behold those who are in gaudy apparel and luxury, are in royal palaces.
26 lakini mnakwenda nje kuona nini, Nabii? Ndiyo, ninasema kwenu na zaidi sana kuliko nabii.
But what went you out to see? a prophet? Yea, and I say unto you even more than a prophet.
27 Huyu ndiye aliyeandikiwa, “Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya macho yenu, atakeyeandaa njia kwa ajili yangu,
This is he concerning whom it has been written, Behold, I send my messenger before thy face, who will prepare thy way before thee.
28 Nasema kwenu, kati ya wale waliozaliwa na mwanamke, hakuna mkuu kama Yohana, lakini mtu asiye muhimu sana atakayeishi na Mungu mahali alipo yeye, atakuwa mkuu kuliko Yohana.”
I say unto you, among those having been born of women no prophet is greater than John the Baptist; nevertheless the least in the kingdom of God is greater than he.
29 Na watu wote waliposikia haya pamoja na watoza ushuru, walitangaza kuwa Mungu ni mwenye Haki. Walikuwepo kati yao wale waliobatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
And all the people hearing and the publicans justified God, being baptized with the baptism of John.
30 Lakini mafarisayo na wataalamu wa sheria za kiyahudi, ambao hawakubatizwa na yeye walikataa hekima za Mungu kwa ajili yao wenyewe.
But the Pharisees and theologians rejected the counsel of God, against themselves, not having been baptized by him.
31 Tena naweza kuwalinganisha na nini watu wa kizazi hiki? Wakoje hasai?
Then to whom shall I liken the men of this generation, and to whom are they like?
32 Wanafanana na watoto wanaocheza kwenye eneo la soko, wanaokaa na kuitana mmoja baada wa mwingine wakisema, 'Tumepuliza filimbi kwa ajili yenu, na hamkucheza. tumeomboleza na hamkulia.'
They are like unto little children sitting in the market-place, and calling to one another, and saying, We piped unto you, and you did not dance; we mourned unto you, and you did not weep.
33 Yohana mbatizaji alikuja hakula mkate wala hakunywa divai, na mkasema “Ana pepo.
For John the Baptist has come neither eating bread nor drinking wine; and you say, He has a demon.
34 Mwana wa Mtu amekuja amekula na kunywa na mkasema, “Angali ni mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!
The Son of man has come eating and drinking, and you say, Behold, a gluttonous wine-drinking man, a friend of publicans and sinners.
35 Lakini hekima imetambulika kuwa ina haki kwa watoto wake wote.”
Truly wisdom is justified by her children.
36 Mmoja wa mafarisayo alimwomba Yesu aende kula pamoja naye. Baada ya Yesu kuingia kwenye nyumba ya farisayo, aliegemea kwenye meza ili ale.
And a certain one of the Pharisees, asked Him, that He would eat with him, and having come into the house of the Pharisee, He sat down to the table.
37 Tazama kulikuwa na mwanamke mmoja katika jiji hilo aliyekuwa na dhambi. Akagundua kuwa alikuwa amekaa kwa Farisayo, akaleta chupa ya manukato.
Behold, a woman who was a sinner, in the city, also having learned that He is dining in the house of the Pharisee, breaking an alabaster box of myrrh,
38 Alisimama nyuma yake karibu na miguu yake huku akilia. Tena alianza kulowanisha miguu yake kwa machozi, na kuifuta kwa nywele za kichwa chake, akiibusu miguu yake na kuipaka manukato.
and standing behind by His feet, weeping, began to moisten His feel with tears, and she wiped them with the hairs of her head, and she continued to copiously kiss His feet, and to anoint them with the myrrh.
39 Na yule farisayo aliyekuwa amemwalika Yesu alipoona hivyo, akawaza mwenyewe akisema, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua huyu ni nani na ni aina gani ya mwanamke anayemgusa, ya kuwa ni mwenye dhambi.
And the Pharisee, having invited Him, seeing, spoke within himself, saying, If He were a prophet, He would know who and what kind the woman is, who touches Him, because she is a sinner.
40 Yesu akajibu na kumwambia, “Simoni nina kitu cha kukuambia. “Akasema” “Kiseme tu mwalimu!”
And Jesus responding said to him, Simon, I have something to say to thee. And he says, Speak, Teacher.
41 Yesu akasema “Kulikuwa na wadaiwa wawili kwa mkopeshaji mmoja. Mmoja alikuwa anadaiwa dinari mia tano na wa pili alidaiwa dinari hamsini.
There were two debtors to a certain creditor: the one owed him five hundred denaria, and the other fifty.
42 Na walipokuwa hawana pesa ya kumlipa aliwasamehe wote. Sasa ni nani atampenda zaidi?
And they not being able to pay, he forgave them both. Then which one of them will love him the more?
43 Simoni akamjibu na kusema, “Nadhani aliyesamehewa zaidi.”Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
Simon responding said, I perceive, that he, to whom he forgave the more. And He said to him, You answered correctly.
44 Yesu akamgeukia mwanamke na kusema kwa Simoni, “Unamwona huyu mwanamke. Nimeingia kwenye Nyumba yako. Hukunipa maji kwa ajili ya miguu yangu, lakini huyu, kwa machozi yake, alilowanisha miguu yangu na kuifuta kwa nywele zake.
And turning to the woman He said to Simon, Do you see this woman? I came into thy house, thou gavest me no water for my feet: but she washed my feet with tears, and wiped them with her hairs.
45 Hukunibusu, lakini yeye, tangu alipoingia humu hakuacha kunibusu miguu yangu.
Thou gavest me no kiss: she, from the time I came in, did not cease copiously kissing my feet.
46 Hukuipaka miguu yangu kwa mafuta, lakini ameipaka miguu yangu kwa manukato.
Thou didst not anoint my head with oil: but she anointed my feet with myrrh.
47 Kwa jambo hili, nakwambia kwamba alikuwa na dhambi nyingi na amesamehewa zaidi, na pia alipenda zaidi. Lakini aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo tu.”
Therefore I say unto thee, her sins, which are many, are forgiven; for she loved much: but he to whom little is forgiven, loveth little.
48 Baadaye akamwambia mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa”
And He said to her; Thy sins are forgiven.
49 Wale waliokaa mezani pamoja naye wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani mpaka anasamehe dhambi?”
And those sitting along with Him began to say among themselves, Who is this who even forgives sins?
50 Na Yesu akamwambia mwanamke, “Imani yako imekuokoa. Enenda kwa amani”
And He said to the woman, Thy faith hath saved them; go in peace.