< Luka 7 >

1 Baada ya Yesu kumaliza kila kitu alichokuwa anasema kwa watu waliomsikiliza, akaingia Kapernaumu.
When he'd finished speaking to the people, Jesus left for Capernaum.
2 Mtumwa fulani wa akida, aliyekuwa wa thamani sana kwake, alikuwa mgonjwa sana na alikuwa karibu ya kufa.
A centurion lived there who had a servant he greatly valued who was sick and was about to die.
3 Lakini akiwa amesikia kuhusu Yesu, yule Akida alimtuma kiongozi wa kiyahudi, kumwomba aje kumwokoa mtumwa wake ili asife.
When he heard about Jesus, the centurion sent some Jewish elders to him, asking him to come and heal his servant.
4 Walipofika karibu na Yesu, walimsihi kwa bidii na kusema, “anastahili kwamba unapaswa kufanya hivi kwa ajili yake,
When the elders came to Jesus, they pleaded with him strongly, saying, “Please come and do what he asks. He deserves your help,
5 kwa sababu analipenda taifa letu, na ndiye aliyejenga sinagogi kwa ajili yetu”.
because he loves our people and he built a synagogue for us.”
6 Yesu akaendelea na safari yake pamoja nao. lakini kabla hajaenda mbali na nyumba, afisa mmoja aliwatuma marafiki zake kuzungumza naye. “Bwana, usijichoshe mwenyewe kwa sababu mimi sistahili wewe kuingia kwenye dari yangu.
Jesus went with them and as they approached the house, the centurion sent some friends to Jesus to tell him, “Lord, please don't trouble yourself by coming into my house, because I'm not worthy of that.
7 Kwa sababu hii sikufikiria hata mimi mwenyewe kuwa ninafaa kuja kwako, lakini sema neno tu na mtumishi wangu atapona.
I didn't even think that I was worthy to come and see you. Just give the command, and my servant will be healed.
8 Kwani mimi pia ni mtu niliyewekwa kwenye mamlaka na nina askari chini yangu. Husema kwa huyu “Nenda” na huenda, na kwa mwingine, “Njoo” naye huja, na kwa mtumishi wangu 'Fanya hiki', na yeye hufanya”.
For I'm under the authority of my superior officers, and I have soldiers under my authority too. I command one to go and he goes, another to come and he comes. I command my servant to do something and he does it.”
9 Yesu aliposikia haya alishangaa, na kuwageukia makutano waliokuwa wanamfuata na kusema.”Nawaambia, hata katika Israeli, sijawahi kuona mtu mwenye imani kuu kama huyu.
When Jesus heard this he was astounded. He turned to the crowd that was following him, and said, “I tell you, I haven't found trust like this even in Israel.”
10 Kisha wale waliokuwa wametumwa walirudi nyumbani na kumkuta mtumishi akiwa mzima.
Then the centurion's friends returned to the house and found the servant in good health.
11 fulani baada ya haya, ilitokea kuwa Yesu alikuwa anasafiri kwenda mji ulioitwa Naini. wanafunzi wake wakaenda pamoja naye wakiambana na umati wa watu.
Soon after Jesus went to a town called Nain, accompanied by his disciples and a large crowd.
12 Alipofika karibu na Lango la jiji tazama, mtu aliyekufa alikuwa amebebwa, na ni mtoto wa pekee kwa mama yake. aliyekuwa mjane, na umati wa wawakilishi kutoka kwenye jiji walikuwa pamoja naye.
As he approached the town gate a funeral procession was coming the other way. The man who had died was the only son of a widow, and a sizeable crowd from the town was with her.
13 Alipomwona, Bwana akamsogelea kwa huruma kubwa sana juu yake na akamwambia, “Usilie”.
When the Lord saw her he was filled with compassion for her. “Don't cry,” he told her.
14 Kisha akasogea mbele akaligusa jeneza ambalo walibebea mwili, na wale waliobeba wakasimama akasema “Kijana nasema amka”
Jesus went over to the coffin and touched it, and the pall-bearers stopped. Jesus said, “Young man, I tell you, get up.”
15 Mfu akainuka na kukaa chini na akaanza kuongea. Kisha Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
The dead man sat up and began to talk, and Jesus gave him back to his mother.
16 Kisha hofu ikawajaa wote. wakaendelea kumtukuza Mungu wakisema “Nabii mkuu ameinuliwa miongoni mwetu” na “Mungu amewaangalia watu wake”
A sense of awe filled everyone there and they praised God, saying, “A great prophet has arisen among us,” and “God has visited his people.”
17 Hizi habari njema za Yesu zilienea Yudea yote na kwa mikoa yote ya jirani.
News about Jesus spread throughout Judea, and all around.
18 Wanafunzi wa Yohana walimwamwambia mambo haya yote.
The disciples of John told John about all this.
19 Ndipo Yohana akawaita wawili wa wanafunzi wake na kuwatuma kwa Bwana kusema “Wewe ndiye yule ajaye, au kuna mtu mwingine tumtazamie?
John called two of his disciples and told them to go and see Jesus, and ask, “Are you the one we've been expecting, or should we wait for someone else?”
20 Walipofika karibu na Yesu hawa wakasema, “Yohana mbatizaji ametutuma kwako kusema, 'Wewe ni yule ajaye au kuna mtu mwingine tumtazamie?”
When they came to Jesus, they said, “John the Baptist sent us to you, to ask you, ‘Are you the one we've been expecting or should we wait for someone else?’”
21 kwa wakati huo aliowaponya watu wengi kutoka katika magonjwa na mateso, kutoka kwa roho wachafu, na kwa watu wenye upofu aliwapa kuona.
At that very moment Jesus was healing many people of their diseases, illnesses, evil spirits, and making the blind to see.
22 Yesu akajibu na kusema kwao. “Baada ya kuwa mmekwenda mlikotoka mtamjulisha Yohana mlichokiona na kukisikia. Wenye upofu wanapokea kuona na viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na kuwa hai tena, masikini wanaambiwa habari njema.
Jesus answered John's disciples, “Go and tell John what you've seen and heard. The blind see, the lame walk, the lepers cured, the deaf hear, the dead raised back to life, the poor are told the good news.
23 Na mtu ambaye hataacha kuniamini mimi kwa sababu ya matendo yangu amebarikiwa”.
How good it is for those who are not offended because of me!”
24 Baada ya wale waliotumwa na Yohana kurudi walikotoka, Yesu akaanza kusema kwa makutano juu ya Yohana, “Mlikwenda nje kuona nini, mwanzi ukiwa unatikiswa na upepo?
After the messengers from John had left, Jesus began telling the crowd, “About John: what did you expect to see when you went out to meet him in the desert? Some reed blown about by the wind?
25 lakini mlikwenda nje kuona nini, mtu aliyevaa vizuri? tazama watu wale wanaovaa mavazi ya kifalme na kuishi maisha ya starehe wako kwenye nafasi za wafalme.
Did you come looking for a man dressed in fine clothes? No, those who have stylish clothes and live in luxury are found in palaces.
26 lakini mnakwenda nje kuona nini, Nabii? Ndiyo, ninasema kwenu na zaidi sana kuliko nabii.
Were you looking for a prophet? Yes he is, and I'm telling you, he's much more than a prophet.
27 Huyu ndiye aliyeandikiwa, “Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya macho yenu, atakeyeandaa njia kwa ajili yangu,
It was written about him in Scripture: ‘Look, I'm sending my messenger to go before you to prepare your way.’
28 Nasema kwenu, kati ya wale waliozaliwa na mwanamke, hakuna mkuu kama Yohana, lakini mtu asiye muhimu sana atakayeishi na Mungu mahali alipo yeye, atakuwa mkuu kuliko Yohana.”
I tell you, no one born of women is greater than John, but even the most unimportant person in God's kingdom is greater than he is!”
29 Na watu wote waliposikia haya pamoja na watoza ushuru, walitangaza kuwa Mungu ni mwenye Haki. Walikuwepo kati yao wale waliobatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
When they heard this, all of them—even the tax collectors—followed what God said was good and right, for they had been baptized by John.
30 Lakini mafarisayo na wataalamu wa sheria za kiyahudi, ambao hawakubatizwa na yeye walikataa hekima za Mungu kwa ajili yao wenyewe.
But the Pharisees and the religious teachers rejected what God wanted them to do, for they had refused to be baptized by John.
31 Tena naweza kuwalinganisha na nini watu wa kizazi hiki? Wakoje hasai?
“What shall I compare these people to?” asked Jesus. “What are they like?
32 Wanafanana na watoto wanaocheza kwenye eneo la soko, wanaokaa na kuitana mmoja baada wa mwingine wakisema, 'Tumepuliza filimbi kwa ajili yenu, na hamkucheza. tumeomboleza na hamkulia.'
They're like children sitting in the market who tell one other, ‘We played the flute for you but you didn't dance; we sang sad songs but you didn't cry.’
33 Yohana mbatizaji alikuja hakula mkate wala hakunywa divai, na mkasema “Ana pepo.
When John the Baptist came he didn't eat bread or drink wine, but you say he's demon-possessed.
34 Mwana wa Mtu amekuja amekula na kunywa na mkasema, “Angali ni mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!
Now the Son of man is here, and eats and drinks with people, but you say, ‘Look, he spends his time eating too much food and drinking too much wine. Plus he's a friend of tax collectors and sinners.’
35 Lakini hekima imetambulika kuwa ina haki kwa watoto wake wote.”
However, God's wise ways are proved right by all who follow him!”
36 Mmoja wa mafarisayo alimwomba Yesu aende kula pamoja naye. Baada ya Yesu kuingia kwenye nyumba ya farisayo, aliegemea kwenye meza ili ale.
One of the Pharisees invited Jesus to come and eat with him. Jesus went to the Pharisee's house and sat down to the meal.
37 Tazama kulikuwa na mwanamke mmoja katika jiji hilo aliyekuwa na dhambi. Akagundua kuwa alikuwa amekaa kwa Farisayo, akaleta chupa ya manukato.
A woman who was a sinner in that town found out that Jesus was eating in the Pharisee's house. She went there, carrying an alabaster jar of perfume.
38 Alisimama nyuma yake karibu na miguu yake huku akilia. Tena alianza kulowanisha miguu yake kwa machozi, na kuifuta kwa nywele za kichwa chake, akiibusu miguu yake na kuipaka manukato.
She kneeled beside Jesus and with her tears wet his feet, and dried them with her hair. She kissed his feet, and then she poured the perfume over them.
39 Na yule farisayo aliyekuwa amemwalika Yesu alipoona hivyo, akawaza mwenyewe akisema, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua huyu ni nani na ni aina gani ya mwanamke anayemgusa, ya kuwa ni mwenye dhambi.
When the Pharisee who had invited Jesus saw this he said to himself, “If this man was really a prophet he would know who this woman was who's touching him, and what kind of person she was—that she's a sinner!”
40 Yesu akajibu na kumwambia, “Simoni nina kitu cha kukuambia. “Akasema” “Kiseme tu mwalimu!”
Jesus spoke up and said, “Simon, I have something to tell you.” “Tell me, Teacher,” he responded.
41 Yesu akasema “Kulikuwa na wadaiwa wawili kwa mkopeshaji mmoja. Mmoja alikuwa anadaiwa dinari mia tano na wa pili alidaiwa dinari hamsini.
“Once two people were in debt to a money-lender. One owed five hundred denarii, the other only fifty.
42 Na walipokuwa hawana pesa ya kumlipa aliwasamehe wote. Sasa ni nani atampenda zaidi?
Neither of them could repay him, so he forgave the debts. Which one will love him the most?”
43 Simoni akamjibu na kusema, “Nadhani aliyesamehewa zaidi.”Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
“The one he forgave the most, I would think,” Simon answered. “You're absolutely right,” said Jesus.
44 Yesu akamgeukia mwanamke na kusema kwa Simoni, “Unamwona huyu mwanamke. Nimeingia kwenye Nyumba yako. Hukunipa maji kwa ajili ya miguu yangu, lakini huyu, kwa machozi yake, alilowanisha miguu yangu na kuifuta kwa nywele zake.
Turning to the woman, he said to Simon, “You see this woman? When I came into your house, you didn't give me water to wash my feet. But she has washed my feet with her tears, and wiped them with her hair.
45 Hukunibusu, lakini yeye, tangu alipoingia humu hakuacha kunibusu miguu yangu.
You didn't give me a kiss, but since I came in she hasn't stopped kissing my feet.
46 Hukuipaka miguu yangu kwa mafuta, lakini ameipaka miguu yangu kwa manukato.
You didn't anoint my head with oil, but she poured perfume over my feet.
47 Kwa jambo hili, nakwambia kwamba alikuwa na dhambi nyingi na amesamehewa zaidi, na pia alipenda zaidi. Lakini aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo tu.”
So I tell you, her many sins have been forgiven—that's why she loves so much. But whoever is forgiven little, only loves a little.”
48 Baadaye akamwambia mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa”
Then Jesus said to the woman, “Your sins have been forgiven.”
49 Wale waliokaa mezani pamoja naye wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani mpaka anasamehe dhambi?”
Those who were sitting eating with him began talking among themselves, saying, “Who is this who even forgives sins?”
50 Na Yesu akamwambia mwanamke, “Imani yako imekuokoa. Enenda kwa amani”
But Jesus told the woman, “Your trust has saved you, go in peace.”

< Luka 7 >