< Luka 4 >

1 Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
And Jesus, full of the Holy Ghost, returned from the Jordan and was led by the Spirit into the wilderness, tempted by the devil forty days.
2 kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
And He ate nothing during those days; and they having been completed, He afterward hungered.
3 Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
And the devil said to Him, If thou art the Son of God, speak to this stone, in order that it may become bread.
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
And Jesus responded to him, saying; It has been written, That man shall not live upon bread alone, but upon every word of God.
5 Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
And the devil leading Him up, he showed Him all the kingdoms of the world in a moment of time.
6 Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
And the devil said to Him, I will give all the authority and glories of these to thee: because it has been given unto me: and I give it to whom I may wish;
7 Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
then if thou mayest worship before me all shall belong to thee.
8 Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
And Jesus responding said to him; It has been written, Thou shalt worship the Lord thy God and Him only shalt thou serve.
9 Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
And he led Him into Jerusalem, and placed Him on a pinnacle of the temple, and said to Him, If thou art the Son of God cast thyself down from thence;
10 Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
for it has been written, That He will give His angels charge concerning thee, in order to guard thee,
11 na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
and they will bear thee upon their hands, lest at any time thou mayest dash thy foot against a stone.
12 Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
And Jesus responding said to him; That it has been said, Thou shalt not tempt the Lord thy God.
13 Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
And the devil having perfected every temptation, departed from Him for a season.
14 Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
And Jesus returned in the power of the spirit into Galilee. And the fame concerning Him went throughout the whole country.
15 Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
And He was teaching in their synagogues, being glorified by all.
16 Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
And He came into Nazareth, where He was brought up: and according to the custom to Him, He came into the synagogue on the Sabbath-day, and stood up to read.
17 Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
And the Book of Isaiah the prophet was given to Him; and having opened the book, He found the place where it was written,
18 “Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
The Spirit of the Lord is upon me, because He anointed me to preach the gospel to the poor: hath sent me to heal the brokenhearted, to proclaim deliverance to the captives, and sight to the blind, and to set at liberty them that are bruised,
19 kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
to proclaim the acceptable year of the Lord.
20 Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
And having closed the book, and giving it back to the officer, He sat down: and the eyes of all in the synagogue were fastened on Him.
21 Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
And He began to say to them; This day has this Scripture been fulfilled in your ears.
22 Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
And they all continued to witness to Him, and wonder at the words of grace proceeding out from His mouth: and say, Is not this the son of Joseph?
23 Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
And He said to them, You truly speak to me this parable, Physician, heal thyself: so many things as we heard having been done in Capernaum, do also here in thy own country.
24 Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
And He said, Truly I say unto you, that no prophet is acceptable in his own country.
25 Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
And in truth I say unto you, There were many widows in Israel in the days of Elijah. When the heaven was shut up three years and six months, how the famine was great over all the land;
26 Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
and Elijah was sent to none of them, except to a widow woman in Sarepta of Sidon.
27 Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
And there were many lepers in Israel in the time of the prophet Elisha; and none of them were cleansed except Naaman the Syrian.
28 Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
And all in the synagogue, hearing these things, were filled with wrath.
29 Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
And rising up, they cast Him out of the city, and were leading Him to the brink of the mountain on which their city was built, to hurl Him down;
30 Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
and He having passed through the midst of them went away.
31 Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
And He came down into Capernaum, a city of Galilee, And He was teaching them on the Sabbath.
32 Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
And they were astonished at His teaching; because His word was with authority.
33 Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
And in the synagogue there was a man having a spirit of an unclean demon, and he cried with a great voice,
34 “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
saying, Let me alone; what is there to us and to thee, O Jesus the Nazarene? Hast thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
35 Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
Jesus rebuked him, saying, Be silent and come out from him; and the demon having thrown him down in the midst came out from him, not having injured him.
36 Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
And fear came upon them all, and they were talking together to one another, saying, What word is this? because with authority and power He commands the unclean spirits, and they come out.
37 Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
And the report concerning Him was going out into every place in the surrounding country,
38 Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
Having arisen up from the synagogue, He came into the house of Simon. And the mother-in-law of Simon was afflicted with a great fever; and they asked Him concerning her.
39 Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
And He, standing over her, rebuked the fever; and dismissed it; and immediately, having stood up, she continued to minister unto them.
40 Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
And the sun having gone down, all so many as had people afflicted with various diseases continued to lead them to Him; and He having put His hands on each one of them, healed them.
41 Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
And the demons continued to go out from many, crying, and saying, Thou art the Christ, the Son of God. And rebuking them, He did not suffer them to speak, because they knew that He was the Christ.
42 Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
And it being day, having come out, He departed into a desert place: and the multitudes continued to seek Him; and they came unto Him, and they constrained Him not to depart from them.
43 Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
And He said to them, That, it behooveth me to preach the gospel of the kingdom of God to many other cities: because unto this I have been sent.
44 Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.
And He was preaching in the synagogues of Galilee.

< Luka 4 >