< Luka 24 >

1 Mapema sana siku ya kwanza ya juma, walikuja kaburini, wakileta manukato ambayo walikuwa wameyaandaa.
Mais le premier jour de la semaine, elles vinrent de grand matin au sépulcre, apportant les parfums qu’elles avaient préparés;
2 Wakakuta jiwe limevingirishwa mbali na kaburi.
Et elles trouvèrent la pierre ôtée du sépulcre.
3 Wakaingia ndani, lakini hawakuukuta mwili wa Bwana Yesu.
Et étant entrées, elles ne trouvèrent point le corps du Seigneur Jésus.
4 Ilitokea kwamba, wakati wamechanganyikiwa kuhusu hili, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi ya kung'aa.
Or il arriva, pendant qu’en leur âme elles en étaient consternées, que près d’elles parurent deux hommes avec des robes resplendissantes.
5 Wanawake wakiwa wamejaa hofu na wakiinamisha nyuso zao chini, wakawaambia wanawake, “Kwanini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?
Et comme elles étaient effrayées et baissaient le visage vers la terre, ils leur dirent: Pourquoi cherchez-vous parmi les morts celui qui est vivant?
6 Hayupo hapa, ila amefufuka! Kumbukeni alivyosema nanyi alipokuwa angali Galilaya,
Il n’est pas ici, mais il est ressuscité; rappelez-vous comment il vous a parlé quand il était encore en Galilée,
7 akisema kwamba Mwana wa Adamu lazima atolewe kwenye mikono ya watu wenye dhambi na asulubishwe, na siku ya tatu, afufuke tena.”
Disant: Il faut que le Fils de l’homme soit livré entre les mains des hommes pécheurs, qu’il soit crucifié, et que le troisième jour il ressuscite.
8 Wale wanawake wakakumbuka maneno yake,
Et elles se ressouvinrent de ses paroles.
9 na wakarudi kutoka kaburini na wakawaambia mambo haya yote wale kumi na moja na wengine wote.
Et revenues du sépulcre, elles annoncèrent toutes ces choses aux onze et à tous les autres.
10 Basi Maria Magdalena, Joana, Maria mama wa Yakobo, na wanawake wengine pamoja nao wakatoa taarifa hizi kwa mitume.
Or c’étaient Marie-Madeleine, Jeanne, Marie, mère de Jacques, et les autres qui étaient avec elles, qui rapportaient ces choses aux apôtres.
11 Lakini ujumbe huu ukaonekana kama mzaha tu kwa mitume, na hawakuwaamini wale wanawake.
Et ce récit leur parut comme du délire, et ils ne les crurent pas.
12 Hata hivyo Petro aliamka, na akakimbia kuelekea kaburini, na akichungulia na kuangalia ndani, aliona sanda peke yake. Petro kisha akaondoka akaenda nyumbani kwake, akistaajabu nini ambacho kimetokea.
Cependant Pierre, se levant, courut au sépulcre; et s’étant penché, il ne vit que les linges posés à terre, et il s’en alla, admirant en lui-même ce qui était arrivé.
13 Na tazama, wawili miongoni mwao walikuwa wakienda siku hiyo hiyo katika kijiji kimoja kiitwacho Emmau, ambacho kilikuwa maili sitini kutoka Yerusalemu.
Or voici que deux d’entre eux allaient ce même jour à un village nommé Emmaüs, qui était à la distance de soixante stades de Jérusalem.
14 Wakajadiliana wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotokea.
Et ils s’entretenaient de tout ce qui s’était passé.
15 Ikatokea kwamba, wakati walipokuwa wakijadiliana na kuulizana maswali, Yesu akasogea karibu akaambatana nao.
Et il arriva, que pendant qu’ils discouraient et conféraient ensemble, Jésus lui-même s’étant approché, marchait avec eux.
16 Lakini macho yao yalizuiliwa katika kumtambua yeye.
Mais leurs yeux étaient retenus de peur qu’ils ne le reconnussent.
17 Yesu akawaambia, “Nini ambacho ninyi wawili mnakiongelea wakati mnatembea?” Wakasimama pale wakionekana na huzuni.
Et il leur dit: Quels sont ces discours que vous tenez ainsi en marchant, et pourquoi êtes-vous tristes?
18 Mmoja wao, jina lake Cleopa, akamjibu, “Je wewe ni mtu pekee hapa Yerusalemu ambaye hajui mambo yaliyotokea huko siku hizi?”
Et l’un d’eux, nommé Cléophas, répondant, lui dit: Es-tu seul si étranger dans Jérusalem, que tu ne saches point ce qui s’y est passé ces jours-ci?
19 Yesu akawaambia, “Mambo gani?” Wakamjibu, “Mambo kuhusu Yesu Mnazareti, ambaye alikuwa nabii, muweza katika matendo na maneno mbele za Mungu na watu wote.
Quoi? leur dit-il. Et ils répondirent: Touchant Jésus de Nazareth, qui fut un prophète puissant en œuvres et en paroles devant Dieu et devant tout le peuple:
20 Na kwa jinsi ambayo wakuu wa makuhani na viongozi wetu walivyomtoa kuhukumiwa kifo na kumsulubisha.
Et comment les princes des prêtres et nos chefs l’ont livré pour être condamné à mort et l’ont crucifié:
21 Lakini tulitumaini kwamba yeye ndiye atakaye waweka huru Israeli. Ndiyo, mbali na haya yote, sasa ni siku ya tatu tangu mambo haya yatokee.
Pour nous, nous espérions que c’était lui qui devait racheter Israël: et cependant, après tout cela, voici déjà le troisième jour que ces choses sont arrivées.
22 Lakini pia, baadhi ya wanawake kutoka katika kundi letu walitushangaza, baada ya kuwapo kaburini asubuhi na mapema.
À la vérité, quelques femmes qui sont des nôtres nous ont effrayés; car étant allées avant le jour au sépulcre,
23 Walipoukosa mwili wake, wakaja, wakisema kwamba waliona pia maono ya malaika waliosema kwamba yu hai.
Et n’ayant point trouvé son corps, elles sont venues disant qu’elles ont vu des anges même qui disent qu’il est vivant.
24 Baadhi ya wanaume ambao walikuwa pamoja nasi walienda kaburini, na kukuta ni kama vile wanawake walivyosema. Lakini hawakumuona yeye.”
Quelques-uns des nôtres sont allés aussi au sépulcre, et ont trouvé toutes choses comme les femmes l’ont dit; mais lui, ils ne l’ont pas trouvé.
25 Yesu akawaambia, “Ninyi watu wajinga na wenye mioyo mizito ya kuamini yote ambayo manabii wamesema!
Alors il leur dit: Ô insensés et lents de cœur à croire tout ce qu’ont dit les prophètes!
26 Je haikuwa lazima Yesu kuteseka kwa mambo haya, na kuingia katika utukufu wake?”
Ne fallait-il pas que le Christ souffrît ces choses, et entrât ainsi dans sa gloire?
27 Kisha kuanzia kutoka kwa Musa na manabii wote, Yesu akawatafsiria mambo yanayomuhusu yeye katika maandiko yote.
Et commençant par Moïse, et par tous les prophètes, il leur interprétait dans toutes les Ecritures ce qui le concernait.
28 Walipokaribia kile kijiji, huko walikokuwa wakienda, Yesu akafanya kana kwamba anaendelea mbele.
Cependant ils approchèrent du village où ils allaient; et Jésus feignit d’aller plus loin.
29 Lakini walimlazimisha, wakisema, “Kaa pamoja nasi, maana inaelekea jioni na siku ni kama imeisha.” Hivyo Yesu akaingia kwenda kukaa nao.
Mais ils le pressèrent, disant: Demeure avec nous, car il se fait tard, et déjà le jour est sur son déclin. Et il entra avec eux.
30 Ilitokea kwamba, wakati amekaa nao kula, alichukua mkate, akaubariki, na kuuvunja, akawapa.
Or il arriva, pendant qu’il était à table avec eux, qu’il prit le pain, le bénit, le rompit, et il le leur présentait.
31 Kisha macho yao yakafunguliwa, wakamjua, na akatoweka ghafla mbele ya macho yao.
Alors leurs yeux s’ouvrirent, et ils le reconnurent: et il disparut de devant leurs yeux.
32 Wakasemezana wao kwa wao, “Hivi mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, wakati alipoongea nasi njiani, wakati alipotufungulia maandiko?”
Et ils se dirent l’un à l’autre: Notre cœur n’était-il pas tout brûlant au dedans de nous, lorsqu’il nous parlait dans le chemin, et nous ouvrait le sens des Ecritures?
33 Wakanyanyuka saa hiyo hiyo, na kurudi Yerusalemu. Wakawakuta wale kumi na mmoja wamekusanyika pamoja, na wale waliokuwa pamoja nao,
Puis se levant à l’heure même, ils retournèrent à Jérusalem, et ils trouvèrent les onze assemblés, et ceux qui étaient avec eux,
34 wakisema, “Bwana amefufuka kwelikweli, na amemtokea Simoni.”
Et disant: Le Seigneur est vraiment ressuscité, et il est apparu à Simon.
35 Hivyo wakawaambia mambo yaliyotokea njiani, na namna Yesu alivyodhihirishwa kwao katika kuumega mkate.
Et eux, à leur tour, racontèrent ce qui leur était arrivé en chemin, et comment ils l’avaient reconnu à la fraction du pain.
36 Wakati wakiongea mambo hayo, Yesu mwenyewe alisimama katikati yao, na akawaambia, “Amani iwe kwenu.”
Or, pendant qu’ils s’entretenaient ainsi, Jésus parut au milieu d’eux, et leur dit: Paix à vous! c’est moi: ne craignez point.
37 Lakini waliogopa na kujawa na hofu, na wakafikiri kwamba waliona roho.
Mais eux, troublés et épouvantés, croyaient voir un esprit.
38 Yesu akawaambia, Kwanini mnafadhaika? Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?
Et il leur dit: Pourquoi êtes-vous troublés, et pourquoi ces pensées s’élèvent-elles dans vos cœurs?
39 Angalieni mikono yangu na miguu yangu, kwamba ni mimi mwenyewe. Niguseni na muone. Kwa maana roho haina nyama na mifupa, kama mnionavyo mimi kuwa navyo.”
Voyez mes mains et mes pieds; c’est bien moi: touchez et voyez: un esprit n’a ni chair ni os, comme vous voyez que j’ai.
40 Alipokwisha kusema hivi, akawaonyesha mikono yake na miguu yake.
Et lorsqu’il eut dit cela, il leur montra ses mains et ses pieds.
41 Walipokuwa bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini, na kustaajabu, Yesu akawaambia, “Je mna kitu chochote cha kula?”
Mais eux ne croyant point encore, et étant transportés d’admiration et de joie, il dit: Avez-vous ici quelque chose à manger?
42 Wakampa kipande cha samaki aliyechomwa.
Et ils lui présentèrent un morceau de poisson rôti et un rayon de miel.
43 Yesu akakichukua, na kukila mbele yao.
Or, lorsqu’il eut mangé devant eux, prenant les restes, il les leur donna.
44 Akawaambia, “Nilipokuwa nanyi, niliwaambia kwamba yote yalioandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na Zaburi lazima yatimilike.”
Puis il leur dit: Voilà ce que je vous ai dit, lorsque j’étais encore avec vous: qu’il fallait que fût accompli tout ce qui est écrit de moi dans la loi de Moïse, dans les prophètes et dans les psaumes.
45 Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.
Alors il leur ouvrit l’esprit, pour qu’ils comprissent les Ecritures;
46 Akawaambia, “Kwamba imeandikwa, Kristo lazima ateseke, na kufufuka tena kutoka katika wafu siku ya tatu.
Et il leur dit: Il est ainsi écrit, et c’est ainsi qu’il fallait que le Christ souffrît, et qu’il ressuscitât d’entre les morts le troisième jour;
47 Na toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe kwa jina lake kwa mataifa yote, kuanzia kutokea Yerusalemu.
Et qu’on prêchât en son nom la pénitence et la rémission des péchés à toutes les nations, en commençant par Jérusalem.
48 Ninyi ni mashahidi wa mambo haya.
Pour vous, vous êtes témoins de ces choses.
49 Angalia, nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu. Lakini subirini hapa jijini, mpaka mtakapovishwa nguvu kutoka juu.
Et moi, je vais vous envoyer le don promis de mon Père. Vous, demeurez dans la ville, jusqu’à ce que vous soyez revêtus de la force d’en haut.
50 Kisha Yesu akawaongoza nje mpaka walipokaribia Bethania. Akainua mikono yake juu, na akawabariki.
Puis il les mena du côté de Béthanie; et les mains levées, il les bénit.
51 Ikatokea kwamba, wakati alipokuwa akiwabariki, aliwaacha na akabebwa juu kuelekea mbinguni.
Et il arriva que, pendant qu’il les bénissait, il s’éloigna d’eux, et s’éleva au ciel.
52 Basi wakamwabudu, na kurudi Yerusalemu na furaha kuu.
Et eux, l’ayant adoré, revinrent à Jérusalem avec une grande joie.
53 Waliendelea kuwepo hekaluni, wakimbariki Mungu.
Et ils étaient toujours dans le temple, louant et bénissant Dieu. Amen.

< Luka 24 >