< Yohana 1 >
1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
Au commencement était le Verbe, et le Verbe était en Dieu, et le Verbe était Dieu.
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
C’est lui qui au commencement était en Dieu.
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
Toutes choses ont été faites par lui; et sans lui rien n’a été fait de ce qui a été fait.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
En lui était la vie, et la vie était la lumière des hommes;
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
Et la lumière luit dans les ténèbres, et les ténèbres ne l’ont pas comprise.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
Il y eut un homme envoyé de Dieu dont le nom était Jean.
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
Celui-ci vint comme témoin pour rendre témoignage à la lumière, afin que tous crussent par lui;
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
Il n’était pas la lumière, mais il devait rendre témoignage à la lumière.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
Celui-là était la vraie lumière, qui illumine tout homme venant en ce monde.
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
Il était dans le monde, et le monde a été fait par lui, et le monde ne l’a pas connu.
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
Il est venu chez lui, et les siens ne l’ont pas reçu.
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
Mais à tous ceux qui l’ont reçu, il a donné le pouvoir d’être faits enfants de Dieu; à ceux qui croient en son nom;
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
Qui ne sont point nés du sang, ni de la volonté de la chair, ni de la volonté de l’homme, mais de Dieu.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
Et le Verbe a été fait chair, et il a habité parmi nous et nous avons vu sa gloire comme la gloire qu’un fils unique reçoit de son père, plein de grâce et de vérité.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
Jean rend témoignage de lui, et il crie, disant: Voici celui-ci dont j’ai dit: Celui qui doit venir après moi a été fait avant moi, parce qu’il était avant moi.
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
Et nous avons tous reçu de sa plénitude, et grâce pour grâce;
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
Car la loi a été donnée par Moïse, la grâce et la vérité sont venues par Jésus-Christ.
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
Personne n’a jamais vu Dieu: le Fils unique qui est dans le sein du Père est celui qui l’a fait connaître.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
Or voici le témoignage de Jean, lorsque les Juifs lui envoyèrent de Jérusalem des prêtres et des lévites pour lui demander: Qui es-tu?
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
Car il confessa, et il ne le nia point; il confessa: Ce n’est pas moi qui suis le Christ.
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
Et ils lui demandèrent: Quoi donc? Es-tu Elie? Et il dit: Non. Es-tu le prophète? Et il répondit: Non.
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
Ils lui dirent donc: Qui es-tu, afin que nous donnions une réponse à ceux qui nous ont envoyés? Que dis-tu de toi-même?
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
Je suis, répondit-il, la voix de celui qui crie dans le désert: Redressez la voie du Seigneur, comme l’a dit le prophète Isaïe.
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
Or ceux qui avaient été envoyés étaient du nombre des pharisiens.
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
Ils l’interrogèrent encore et lui dirent: Pourquoi donc baptises-tu, si tu n’es ni le Christ, ni Élie, ni le prophète?
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
Jean leur répondit, disant: Moi je baptise dans l’eau, mais il y a au milieu de vous quelqu’un que vous ne connaissez point.
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
C’est lui qui doit venir après moi, qui a été fait avant moi; je ne suis même pas digne de délier la courroie de sa chaussure.
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
Ceci se passa en Béthanie, au-delà du Jourdain où Jean baptisait.
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
Le jour suivant Jean vit Jésus venant à lui, et il dit: Voici l’agneau de Dieu, voici celui qui ôte le péché du monde.
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
C’est celui de qui j’ai dit: Après moi vient un homme qui a été fait avant moi, parce qu’il était avant moi;
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
Et moi je ne le connaissais pas; mais c’est pour qu’il fût manifesté en Israël, que je suis venu baptisant dans l’eau.
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
Jean rendit encore témoignage, disant: J’ai vu l’Esprit descendant sur lui en forme de colombe, et il s’est reposé sur lui.
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
Et moi je ne le connaissais pas; mais celui qui m’a envoyé baptiser dans l’eau m’a dit: Celui sur qui tu verras l’Esprit descendre et se reposer, c’est celui-là qui baptisera dans l’Esprit-Saint.
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
Et je l’ai vu, et j’ai rendu témoignage que c’est lui qui est le Fils de Dieu.
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
Le jour suivant, Jean se trouvait de nouveau avec deux de ses disciples.
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
Et regardant Jésus qui se promenait, il dit: Voilà l’agneau de Dieu.
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
Les deux disciples l’entendirent parler ainsi, et ils suivirent Jésus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
Or Jésus s’étant retourné et les voyant qui le suivaient, leur dit: Que cherchez-vous? Ils lui répondirent; Rabbi (ce qui veut dire, par interprétation, Maître), où demeurez-vous?
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
Il leur dit: Venez et voyez. Ils vinrent, et virent où il demeurait, et ils restèrent avec lui ce jour-là: or, il était environ la dixième heure,
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
Or André, frère de Simon-Pierre, était un des deux qui avaient entendu de Jean ce témoignage, et qui avaient suivi Jésus.
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
Or il rencontra d’abord son frère Simon, et lui dit: Nous avons trouvé le Messie (ce qu’on interprète par le Christ).
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
Et il l’amena à Jésus. Et Jésus l’ayant regardé, dit: Tu es Simon, fils de Jona; tu seras appelé Céphas, ce qu’on interprète par Pierre.
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
Le lendemain, Jésus voulut aller en Galilée; il trouva Philippe et lui dit: Suis-moi.
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
Or Philippe était de Bethsaïde, de la même ville qu’André et Pierre.
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Philippe trouva Nathanaël, et lui dit: Nous avons trouvé celui de qui Moïse a écrit dans la loi et ensuite les prophètes, Jésus, fils de Joseph de Nazareth.
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
Et Nathanaël lui demanda: Peut-il venir de Nazareth quelque chose de bon? Philippe lui répondit: Viens et vois.
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
Jésus vit venir à lui Nathanaël, et il dit de lui: Voici vraiment un Israélite en qui il n’y a point d’artifice.
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
Nathanaël lui demanda: D’où me connaissez-vous? Jésus répondit et lui dit: Avant que Philippe t’appelât, lorsque tu étais sous le figuier, je t’ai vu.
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
Nathanaël lui répondit et dit: Rabbi, vous êtes le Fils de Dieu, vous êtes le roi d’Israël.
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
Jésus répliqua et lui dit: Parce que je t’ai dit: Je t’ai vu sous le figuier, tu crois; tu verras de plus grandes choses.
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Et il ajouta: En vérité, en vérité, je vous le dis, vous verrez le ciel ouvert et les anges de Dieu montant et descendant sur le Fils de l’homme.