< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
et respondens Iob ait
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
vere scio quod ita sit et quod non iustificetur homo conpositus Deo
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
si voluerit contendere cum eo non poterit ei respondere unum pro mille
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
sapiens corde est et fortis robore quis restitit ei et pacem habuit
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
qui transtulit montes et nescierunt hii quos subvertit in furore suo
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
qui commovet terram de loco suo et columnae eius concutiuntur
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
qui praecipit soli et non oritur et stellas claudit quasi sub signaculo
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
qui extendit caelos solus et graditur super fluctus maris
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
qui facit Arcturum et Oriona et Hyadas et interiora austri
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
qui facit magna et inconprehensibilia et mirabilia quorum non est numerus
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
si venerit ad me non videbo si abierit non intellegam eum
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
si repente interroget quis respondebit ei vel quis dicere potest cur facis
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Deus cuius resistere irae nemo potest et sub quo curvantur qui portant orbem
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
quantus ergo sum ego qui respondeam ei et loquar verbis meis cum eo
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
qui etiam si habuero quippiam iustum non respondebo sed meum iudicem deprecabor
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
et cum invocantem exaudierit me non credo quod audierit vocem meam
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
in turbine enim conteret me et multiplicabit vulnera mea etiam sine causa
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
non concedit requiescere spiritum meum et implet me amaritudinibus
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
si fortitudo quaeritur robustissimus est si aequitas iudicii nemo pro me audet testimonium dicere
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
si iustificare me voluero os meum condemnabit me si innocentem ostendere pravum me conprobabit
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
etiam si simplex fuero hoc ipsum ignorabit anima mea et taedebit me vitae meae
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
unum est quod locutus sum et innocentem et impium ipse consumit
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
si flagellat occidat semel et non de poenis innocentum rideat
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
terra data est in manu impii vultum iudicum eius operit quod si non ille est quis ergo est
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
dies mei velociores fuerunt cursore fugerunt et non viderunt bonum
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
pertransierunt quasi naves poma portantes sicut aquila volans ad escam
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
cum dixero nequaquam ita loquar commuto faciem meam et dolore torqueor
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
verebar omnia opera mea sciens quod non parceres delinquenti
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
si autem et sic impius sum quare frustra laboravi
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
si lotus fuero quasi aquis nivis et fulserint velut mundissimae manus meae
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
tamen sordibus intingues me et abominabuntur me vestimenta mea
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
neque enim viro qui similis mei est respondebo nec qui mecum in iudicio ex aequo possit audiri
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
non est qui utrumque valeat arguere et ponere manum suam in ambobus
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
auferat a me virgam suam et pavor eius non me terreat
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
loquar et non timebo eum neque enim possum metuens respondere

< Ayubu 9 >