< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Alors Job prit la parole et dit:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Je sais bien qu'il en est ainsi: comment l'homme serait-il juste vis-à-vis de Dieu?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
S'il voulait contester avec lui, sur mille choses il ne pourrait répondre à une seule.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Dieu est sage en son cœur, et puissant en force: qui lui a résisté, et est demeuré en paix?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Il transporte les montagnes, sans qu'elles le sachent, il les renverse dans sa colère;
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
il secoue la terre sur sa base, et ses colonnes sont ébranlées.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Il commande au soleil, et le soleil ne se lève pas; il met un sceau sur les étoiles.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
Seul, il étend les cieux, il marche sur les hauteurs de la mer.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Il a créé la Grande Ourse, Orion, les Pléiades, et les régions du ciel austral.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Il fait des merveilles qu'on ne peut sonder, des prodiges qu'on ne saurait compter.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Voici qu'il passe près de moi, et je ne le vois pas; il s'éloigne, sans que je l'aperçoive.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
S'il ravit une proie, qui s'y opposera, qui lui dira: « Que fais-tu? »
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Dieu! Rien ne fléchit sa colère; devant lui s'inclinent les légions d'orgueil.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Et moi je songerais à lui répondre, à choisir mes paroles pour discuter avec lui!
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Aurais-je pour moi la justice, je ne répondrais pas; j'implorerais la clémence de mon juge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Même s'il se rendait à mon appel, je ne croirais pas qu'il eût écouté ma voix:
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
lui qui me brise comme dans un tourbillon, et multiplie mes blessures sans motif;
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
qui ne me laisse point respirer, et me rassasie d'amertume.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
S'agit-il de force, voici qu'il est fort, s'agit-il de droit, il dit: « Qui m'assigne? »
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Serais-je irréprochable, ma bouche même me condamnerait; serais-je innocent, elle me déclarerait pervers.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Innocent! Je le suis; je ne tiens pas à l'existence, et la vie m'est à charge.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
Il m'importe après tout; c'est pourquoi j'ai dit: « Il fait périr également le juste et l'impie. »
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
Si du moins le fléau tuait d'un seul coup! Hélas! il se rit des épreuves de l'innocent!
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
La terre est livrée aux mains du méchant, Dieu voile la face de ses juges: si ce n'est pas lui, qui est-ce donc?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
Mes jours sont plus rapides qu'un courrier, ils fuient sans avoir vu le bonheur;
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
ils passent comme la barque de jonc, comme l'aigle qui fond sur sa proie.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Si je dis: « Je veux oublier ma plainte, quitter mon air triste, prendre un air joyeux, »
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
je tremble pour toutes mes douleurs, je sais que tu ne me tiendras pas pour innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Je serai jugé coupable: pourquoi prendre une peine inutile?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Quand je me laverais dans la neige, quand je purifierais mes mains avec le bor,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
tu me plongerais dans la fange, et mes vêtements m'auraient en horreur.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Dieu n'est pas un homme comme moi, pour que je lui réponde, pour que nous comparaissions ensemble en justice.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Il n'y a pas entre nous d'arbitre qui pose sa main sur nous deux.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Qu'il retire sa verge de dessus moi, que ses terreurs cessent de m'épouvanter:
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
alors je parlerai sans le craindre; autrement, je ne suis point à moi-même.

< Ayubu 9 >