< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Alors Baldad de Suhé prit la parole et dit:
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
Jusques à quand tiendras-tu ces discours, et tes paroles seront-elles comme un souffle de tempête?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Est-ce que Dieu fait fléchir le droit, ou bien le Tout-Puissant renverse-t-il la justice?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
Si tes fils ont péché contre lui, il les a livrés aux mains de leur iniquité.
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Pour toi, si tu as recours à Dieu, si tu implores le Tout-Puissant,
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
si tu es droit et pur, alors il veillera sur toi, il rendra le bonheur à la demeure de ta justice;
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
ton premier état semblera peu de chose, tant le second sera florissant.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
Interroge les générations passées, sois attentif à l'expérience des pères: —
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
car nous sommes d'hier, et nous ne savons rien, nos jours sur la terre passent comme l'ombre; —
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
ne vont-ils pas t'enseigner, te parler, et de leur cœur tirer des sentences:
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
« Le papyrus croît-il en dehors des marais? Le jonc s'élève-t-il sans eau?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
Encore tendre, sans qu'on le coupe, il sèche avant toute herbe.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Telles sont les voies de tous ceux qui oublient Dieu; l'espérance de l'impie périra.
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
Sa confiance sera brisée; son assurance ressemble à la toile de l'araignée.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
Il s'appuie sur sa maison, et elle ne tient pas; il s'y attache, et elle ne reste pas debout.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
Il est plein de vigueur, au soleil, ses rameaux s'étendent sur son jardin,
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
ses racines s'entrelacent parmi les pierres, il plonge jusqu'aux profondeurs du roc.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
Si Dieu l'arrache de sa place, sa place le renie: Je ne t'ai jamais vu.
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
C'est là que sa joie se termine, et du même sol d'autres s'élèveront après lui. »
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Non, Dieu ne rejette pas l'innocent, il ne prend pas la main des malfaiteurs.
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Il remplira ta bouche d'éclats de rire, et mettra sur tes lèvres des chants d'allégresse.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
Tes ennemis seront couverts de honte, et la tente des méchants disparaîtra.

< Ayubu 8 >