< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
پس بلدد شوحی در جواب گفت:۱
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
«تا به کی این چیزها را خواهی گفت و سخنان دهانت باد شدید خواهد بود؟۲
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
آیا خداوندداوری را منحرف سازد؟ یا قادر مطلق انصاف رامنحرف نماید؟۳
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
چون فرزندان تو به او گناه ورزیدند، ایشان را به‌دست عصیان ایشان تسلیم نمود.۴
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
اگر تو به جد و جهد خدا را طلب می‌کردی و نزد قادر مطلق تضرع می‌نمودی،۵
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
اگر پاک و راست می‌بودی، البته برای تو بیدارمی شد، و مسکن عدالت تو را برخوردارمی ساخت.۶
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
و اگر‌چه ابتدایت صغیر می‌بود، عاقبت تو بسیار رفیع می‌گردید.۷
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
زیرا که ازقرنهای پیشین سوال کن، و به آنچه پدران ایشان تفحص کردند توجه نما،۸
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
چونکه ما دیروزی هستیم و هیچ نمی دانیم، و روزهای ما سایه‌ای برروی زمین است.۹
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
آیا ایشان تو را تعلیم ندهند وبا تو سخن نرانند؟ و از دل خود کلمات بیرون نیارند؟۱۰
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
آیا نی، بی‌خلاب می‌روید، یا قصب، بی‌آب نمو می‌کند؟۱۱
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
هنگامی که هنوز سبزاست و بریده نشده، پیش از هر گیاه خشک می‌شود.۱۲
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
همچنین است راه جمیع فراموش کنندگان خدا. و امید ریاکار ضایع می شود،۱۳
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
که امید او منقطع می‌شود، واعتمادش خانه عنکبوت است.۱۴
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
بر خانه خودتکیه می‌کند و نمی ایستد، به آن متمسک می‌شودو لیکن قایم نمی ماند.۱۵
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
پیش روی آفتاب، تر وتازه می‌شود و شاخه هایش در باغش پهن می‌گردد.۱۶
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
ریشه هایش بر توده های سنگ درهم بافته می‌شود، و بر سنگلاخ نگاه می‌کند.۱۷
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
اگر ازجای خود کنده شود، او را انکار کرده، می‌گوید: تو را نمی بینم.۱۸
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
اینک خوشی طریقش همین است و دیگران از خاک خواهند رویید.۱۹
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
هماناخدا مرد کامل را حقیر نمی شمارد، و شریر رادستگیری نمی نماید،۲۰
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
تا دهان تو را از خنده پرکند، و لبهایت را از آواز شادمانی.۲۱
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
خصمان توبه خجالت ملبس خواهند شد، و خیمه شریران نابود خواهد گردید.»۲۲

< Ayubu 8 >