< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
«آیا لویاتان را با قلاب توانی کشید؟ یازبانش را با ریسمان توانی فشرد؟۱
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
آیادر بینی او مهار توانی کشید؟ یا چانه‌اش را باقلاب توانی سفت؟۲
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
آیا او نزد تو تضرع زیادخواهد نمود؟ یا سخنان ملایم به تو خواهدگفت؟۳
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
آیا با تو عهد خواهد بست یا او را برای بندگی دایمی خواهی گرفت؟۴
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
آیا با او مثل گنجشک بازی توانی کرد؟ یا او را برای کنیزان خود توانی بست؟۵
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
آیا جماعت (صیادان ) از اوداد و ستد خواهند کرد؟ یا او را در میان تاجران تقسیم خواهند نمود؟۶
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
آیا پوست او را با نیزه هامملو توانی کرد؟ یا سرش را با خطافهای ماهی گیران؟۷
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
اگر دست خود را بر او بگذاری جنگ را به یاد خواهی داشت و دیگر نخواهی کرد.۸
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
اینک امید به او باطل است. آیا از رویتش نیز آدمی به روی درافکنده نمی شود؟۹
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
کسی اینقدر متهور نیست که او را برانگیزاند. پس کیست که در حضور من بایستد؟۱۰
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
کیست که سبقت جسته، چیزی به من داده، تابه او رد نمایم؟ هرچه زیر آسمان است از آن من می‌باشد.۱۱
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
«درباره اعضایش خاموش نخواهم شد و ازجبروت و جمال ترکیب او خبر خواهم داد.۱۲
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
کیست که روی لباس او را باز تواند نمود؟ وکیست که در میان دو صف دندانش داخل شود؟۱۳
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
کیست که درهای چهره‌اش را بگشاید؟ دایره دندانهایش هولناک است.۱۴
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
سپرهای زورآورش فخر او می‌باشد، با مهر محکم وصل شده است.۱۵
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
با یکدیگر چنان چسبیده‌اند که باد از میان آنهانمی گذرد.۱۶
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
با همدیگر چنان وصل شده‌اند و باهم ملتصقند که جدا نمی شوند.۱۷
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
از عطسه های او نور ساطع می‌گردد و چشمان او مثل پلکهای فجر است.۱۸
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
از دهانش مشعلها بیرون می‌آید وشعله های آتش برمی جهد.۱۹
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
از بینی های او دودبرمی آید مثل دیگ جوشنده و پاتیل.۲۰
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
از نفس او اخگرها افروخته می‌شود و از دهانش شعله بیرون می‌آید.۲۱
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
بر گردنش قوت نشیمن دارد، وهیبت پیش رویش رقص می‌نماید.۲۲
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
طبقات گوشت او بهم چسبیده است، و بر وی مستحکم است که متحرک نمی شود.۲۳
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
دلش مثل سنگ مستحکم است، و مانند سنگ زیرین آسیا محکم می‌باشد.۲۴
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
چون او برمی خیزد نیرومندان هراسان می‌شوند، و از خوف بی‌خود می‌گردند.۲۵
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
اگر شمشیر به او انداخته شود اثر نمی کند، و نه نیزه و نه مزراق و نه تیر.۲۶
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
آهن را مثل کاه می‌شمارد و برنج را مانند چوب پوسیده.۲۷
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
تیرهای کمان او را فرار نمی دهد و سنگهای فلاخن نزد او به کاه مبدل می‌شود.۲۸
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
عمود مثل کاه شمرده می‌شود و بر حرکت مزراق می‌خندد.۲۹
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
در زیرش پاره های سفال تیز است و گردون پرمیخ را بر گل پهن می‌کند.۳۰
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
لجه را مثل دیگ می‌جوشاند و دریا را مانند پاتیلچه عطاران می‌گرداند.۳۱
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
راه را در عقب خویش تابان می‌سازد به نوعی که لجه را سفیدمو گمان می‌برند.۳۲
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
بر روی خاک نظیر او نیست، که بدون خوف آفریده شده باشد.۳۳
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
بر هرچیز بلند نظر می‌افکندو بر جمیع حیوانات سرکش پادشاه است.»۳۴

< Ayubu 41 >