< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
Og Herren svara Job og sagde:
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
«Vil klandraren med Allvald trætta? Lat han som lastar Gud då svara!»
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
Då svara Job Herren og sagde:
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
«For ring eg er; kva skal eg svara? Eg handi legg på munnen min.
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
Ein gong eg tala, no eg tegjer, tvo gong’ - eg gjer det ikkje meir.»
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
Og Herren svara Job or stormen og sagde:
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
«Spenn som mann ditt beltet på, gjev meg på mine spursmål svar:
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
Vil du forspille meg min rett, fordøma meg, so du fær rett?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Hev du vel slik ein arm som Gud? Kann du som han med røysti dundra?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
Pryd deg med høgd og herredom, klæd deg i glans og herlegdom,
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
Lat so din vreide strøyma fram, sjå kvar ein stolt og audmyk han!
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Så kvar ein stolt og bøyg han ned, og slå til jord dei gudlause!
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
Og gøym deim alle under jordi, bitt deira andlit fast i løynd!
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
So skal eg og lovprisa deg, som siger med di høgre vann.
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
Sjå elvhesten! Eg hev skapt han liksom deg; som ein ukse et han gras.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
Sjå då krafti i hans lender, i bukmusklarne hans styrke!
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
Halen gjer han stiv som ceder, fast bogsenarne er tvinna.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
Knokarne er koparrøyrer, beini som jarnstenger er.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
Av Guds verk er han det fyrste, av sin skapar fekk han sverd.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
Bergi ber åt honom for, alle villdyr leikar der.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
Under lotusbusk han kviler, løyner seg i røyr og sev.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
Lotusbusk gjev honom skugge, piletre umkransar honom.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
Strid gjeng elvi, ei han ottast; trygg er han um so sjølve Jordan fossar imot hans gap.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
Kann ein tak han so han ser det, draga snara gjenom snuten?

< Ayubu 40 >