< Ayubu 39 >

1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
“Have you known the time of The bearing of the wild goats of the rock? Do you mark the bringing forth of does?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
Do you number the months they fulfill? And have you known the time of their bringing forth?
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
They bow down, They bring forth their young ones safely, They cast forth their pangs.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Their young ones are safe, They grow up in the field, they have gone out, And have not returned to them.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
Who has sent forth the wild donkey free? Indeed, who opened the bands of the wild donkey?
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
Whose house I have made the wilderness, And his dwellings the barren land,
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
He laughs at the multitude of a city, He does not hear the cries of an exactor.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
The range of mountains [is] his pasture, And he seeks after every green thing.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
Is a wild ox willing to serve you? Does he lodge by your crib?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
Do you bind a wild ox in a furrow [with] his thick band? Does he harrow valleys after you?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
Do you trust in him because his power [is] great? And do you leave your labor to him?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
Do you trust in him That he brings back your seed, And gathers [it to] your threshing-floor?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
[The] wing of the crying ostriches exults, but as a pinion and feather of a stork?
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
For she leaves her eggs on the earth, And she warms them on the dust,
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
And she forgets that a foot may press it, And a beast of the field treads it down.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
It has hardened her young ones without her, Her labor [is] in vain, without fear.
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
For God has caused her to forget wisdom, And He has not given a portion To her in understanding;
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
At the time she lifts herself up on high, She laughs at the horse and his rider.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
Do you give might to the horse? Do you clothe his neck [with] a mane?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
Do you cause him to rush as a locust? The splendor of his snorting [is] terrible.
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
They dig in a valley, and he rejoices in power, He goes forth to meet the armor.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
He laughs at fear, and is not frightened, And he does not turn back from the face of the sword.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
Quiver rattles against him, The flame of a spear, and a javelin.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
He swallows the ground with trembling and rage, And does not remain steadfast Because of the sound of a horn.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
Among the horns he says, Aha, And from afar he smells battle, Roaring of princes and shouting.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
By your understanding does a hawk fly? Does he spread his wings to the south?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
At your command does an eagle go up high? Or lift up his nest?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
He inhabits a rock, Indeed, he lodges on the tooth of a rock, and fortress.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
From there he has sought food, His eyes look attentively to a far-off place,
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
And his brood sucks up blood, And where the pierced [are]—there [is] he!”

< Ayubu 39 >