< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
“And yet, please, O Job, Hear my speech and give ear [to] all my words.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Now behold, I have opened my mouth, My tongue has spoken in the palate.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Of the uprightness of my heart [are] my sayings, And my lips have clearly spoken knowledge.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
The Spirit of God has made me, And the breath of the Mighty quickens me.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
If you are able—answer me, Set in array before me—station yourself.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Behold, I [am], according to your word, for God, I have also been formed from the clay.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Behold, my terror does not frighten you, And my burden on you is not heavy.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
Surely you have spoken in my ears, And the sounds of words I hear:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
I [am] pure, without transgression, I [am] innocent, and I have no iniquity.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Behold, He develops hindrances against me, He reckons me for an enemy to Him,
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
He puts my feet in the stocks, He watches all my paths.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Behold, you have not been righteous [in] this, I answer you, that God is greater than man.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Why have you striven against Him, When [for] all His matters He does not answer?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
For once God speaks, and twice (he does not behold it),
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
In a dream—a vision of night, In the falling of deep sleep on men, In slumberings on a bed.
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Then He uncovers the ear of men, And seals for their instruction,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
To turn aside man [from] doing, And He conceals pride from man.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
He keeps back his soul from corruption, And his life from passing away by a dart.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
And he has been reproved With pain on his bed, And the strife of his bones [is] enduring.
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
And his life has nauseated bread, And his soul desirable food.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
His flesh is consumed from being seen, And his bones are high, they were not seen!
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
And his soul draws near to the pit, And his life to those causing death.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
If there is a messenger by him, An interpreter—one of a thousand, To declare for man his uprightness,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
Then He favors him and says, Ransom him from going down to the pit, I have found an atonement.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Fresher [is] his flesh than a child’s, He returns to the days of his youth.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
He makes supplication to God, And He accepts him. And he sees His face with shouting, And He returns to man His righteousness.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
[Then] he looks on men and says, I sinned, and I have perverted uprightness, And it has not been profitable to me.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
He has ransomed my soul From going over into the pit, And my life looks on the light.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
Behold, God works all these, Twice, [even] three times with man,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
To bring back his soul from the pit, To be enlightened with the light of the living.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Attend, O Job, listen to me, Keep silent, and I speak.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
If there are words—answer me, Speak, for I have a desire to justify you.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
If there are not—listen to me, Keep silent, and I teach you wisdom.”

< Ayubu 33 >