< Ayubu 13 >

1 Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
“Behold, my eye has seen all, My ear has heard, and it attends to it.
2 Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
According to your knowledge I have known—also I. I am not more fallen than you.
3 Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
Yet I speak for the Mighty One, And I delight to argue for God.
4 Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
And yet, you [are] forgers of falsehood, Physicians of nothing—all of you,
5 Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
O that you would keep perfectly silent, And it would be to you for wisdom.
6 Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
Please hear my argument, And attend to the pleadings of my lips,
7 Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
Do you speak perverseness for God? And do you speak deceit for Him?
8 Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
Do you accept His face, if you strive for God?
9 Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
Is [it] good that He searches you, If, as one mocks at a man, you mock at Him?
10 Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
He surely reproves you, if you accept faces in secret.
11 Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
Does His excellence not terrify you? And His dread fall on you?
12 Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
Your remembrances [are] allegories of ashes, For high places of clay [are] your heights.
13 Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
Keep silent from me, and I speak, And pass over me what will.
14 Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
Why do I take my flesh in my teeth? And my soul put in my hand?
15 Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
Behold, He slays me—I do not wait! Only, I argue my ways to His face.
16 Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
Also—He [is] to me for salvation, For the profane do not come before Him.
17 Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
Hear my word diligently, And my declaration with your ears.
18 Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
Now behold, I have set the cause in order, I have known that I am righteous.
19 Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
Who [is] he that strives with me? For now I keep silent and gasp.
20 Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
Only two things, O God, do with me, Then I am not hidden from Your face:
21 Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
Put Your hand far off from me, And do not let Your terror terrify me.
22 Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
And You call, and I answer, Or—I speak, and You answer me.
23 Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
How many iniquities and sins do I have? Let me know my transgression and my sin.
24 Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
Why do You hide Your face? And reckon me for an enemy to You?
25 Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
Do You terrify a leaf driven away? And do You pursue the dry stubble?
26 Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
For You write bitter things against me, And cause me to possess iniquities of my youth,
27 Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
And you put my feet in the stocks, And observe all my paths—You set a print on the roots of my feet,
28 japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.
And he, as a rotten thing, wears away, A moth has consumed him as a garment.”

< Ayubu 13 >