< Ayubu 21 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Job contestó:
2 “Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
“Por favor, escuchen atentamente lo que digo; eso sería un consuelo que podrían darme.
3 Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
Tengan paciencia conmigo; déjenme hablar. Después de que haya habladao, pueden seguir burlándose de mí.
4 Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
¿Me estoy quejando de la gente? Por supuesto que no. ¿Por qué no debería estar impaciente?
5 Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
Mírenme. ¿No están horrorizados? Tápense la boca con la mano en señal de asombro.
6 Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
Cada vez que pienso en lo que me ha pasado me horrorizo y tiemblo de miedo.
7 Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
“¿Por qué siguen viviendo los malvados, que envejecen y son cada vez más poderosos?
8 Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
Sus hijos están con ellos; ven crecer a sus nietos.
9 Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
Viven en sus casas con seguridad; no tienen miedo. Dios no usa su vara para golpearlos.
10 Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
Sus toros siempre crían con éxito; sus vacas paren terneros y no abortan.
11 Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
Sacan a jugar a sus pequeños como si fueran corderos; sus niños bailan alrededor.
12 Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
Cantan acompañados de la pandereta y la lira; celebran con la música de la flauta.
13 Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
Viven felices y bajan al sepulcro en paz. (Sheol h7585)
14 Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
Sin embargo, le dicen a Dios: ‘¡Vete lejos! No queremos saber nada de ti.
15 Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
¿Quién se cree el Todopoderoso para que le sirvamos como esclavos? ¿Qué beneficio hay para nosotros si le oramos?’
16 Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
Esa gente cree que hace su propia fortuna, pero yo no acepto su forma de pensar.
17 Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
“Cuántas veces se apaga la lámpara de los malvados? ¿Cuántas veces les sobreviene el desastre? ¿Cuántas veces castiga Dios a los impíos en su cólera?
18 Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
¿Son arrastrados como paja en el viento? ¿Viene un tornado y se los lleva?
19 Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
Algunos dicen: ‘Dios guarda el castigo de la gente para sus hijos’. Pero yo digo: ‘Dios debería castigar a esas personas para que aprendan de ello’.
20 Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
Que ellos mismos vean su destrucción y beban profundamente de la ira de Dios.
21 Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
Porque no les importará lo que les ocurra a sus familias una vez que hayan muerto.
22 Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
“¿Puede alguien enseñarle a Dios algo que no sepa ya, puesto que él es quien juzga incluso a los seres celestiales?
23 Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
Una persona muere con buena salud, totalmente cómoda y segura.
24 Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
Su cuerpo está gordo por haber comido bien; sus huesos aún son fuertes.
25 Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
Otro muere después de una vida miserable sin haber experimentado la felicidad.
26 Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
Sin embargo, ambos son enterrados en el mismo polvo; son tratados de igual manera en la muerte, comidos por los gusanos.
27 Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
“Sé lo que piensan y sus planes para hacerme mal.
28 Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
Pueden preguntarme: ‘¿Dónde está la casa del gran hombre? ¿Dónde está el lugar donde viven los malvados?’
29 Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
¿No le han preguntado a los viajeros? ¿No le prestan atención a lo que dicen?
30 kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
La gente malvada se salva en tiempos de desastre; es rescatada del día del juicio.
31 Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
¿Quién cuestiona sus acciones? ¿Quién les paga por lo que han hecho?
32 Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
Cuando finalmente mueren y son llevados al cementerio, su tumba está custodiada. La tierra de la tumba los cubre suavemente.
33 Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
Todo el mundo asiste a sus funerales; una enorme procesión de gente viene a presentar sus últimos respetos.
34 Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”
¿Por qué tratan de consolarme con tonterías? Sus respuestas no son más que una sarta de mentiras!”

< Ayubu 21 >