< Ayubu 10 >
1 Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
Dodijao je duši mojoj život moj; pustiæu od sebe tužnjavu svoju, govoriæu u jadu duše svoje.
2 Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
Reæi æu Bogu: nemoj me osuditi; kaži mi zašto se preš sa mnom.
3 ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
Je li ti milo da èiniš silu, da odbacuješ djelo ruku svojih i savjet bezbožnièki obasjavaš?
4 Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
Jesu li u tebe oèi tjelesne? vidiš li kao što vidi èovjek?
5 Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
Jesu li dani tvoji kao dani èovjeèji, i godine tvoje kao vijek ljudski,
6 hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
Te istražuješ moje bezakonje i za grijeh moj razbiraš?
7 ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
Ti znaš da nijesam kriv, i nema nikoga ko bi izbavio iz tvoje ruke.
8 Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
Tvoje su me ruke stvorile i naèinile, i ti me otsvuda potireš.
9 Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
Opomeni se da si me kao od kala naèinio, i opet æeš me u prah obratiti.
10 Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
Nijesi li me kao mlijeko slio i kao sir usirio me?
11 Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
Navukao si na me kožu i meso, i kostima i žilama spleo si me.
12 Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
Životom i milošæu darivao si me; i staranje tvoje èuvalo je duh moj.
13 Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
I sakrio si to u srcu svojem; ali znam da je u tebe.
14 kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
Ako sam zgriješio, opazio si me, i nijesi me oprostio bezakonja mojega.
15 Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
Ako sam skrivio, teško meni! ako li sam prav, ne mogu podignuti glave, pun sramote i videæi muku svoju.
16 Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
I ako se podigne, goniš me kao lav, i opet èiniš èudesa na meni.
17 Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
Ponavljaš svjedoèanstva svoja protiv mene, i umnožavaš gnjev svoj na me; vojske jedna za drugom izlaze na me.
18 Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
Zašto si me izvadio iz utrobe? o da umrijeh! da me ni oko ne vidje!
19 Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
Bio bih kao da nigda nijesam bio; iz utrobe u grob bio bih odnesen.
20 Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
Nije li malo dana mojih? prestani dakle i okani me se da se malo oporavim,
21 kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
Prije nego otidem odakle se neæu vratiti, u zemlju tamnu i u sjen smrtni,
22 ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”
U zemlju tamnu kao mrak i u sjen smrtni, gdje nema promjene i gdje je vidjelo kao tama.