< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
アダムの系図は次のとおりである。神が人を創造された時、神をかたどって造り、
2 Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
彼らを男と女とに創造された。彼らが創造された時、神は彼らを祝福して、その名をアダムと名づけられた。
3 Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
アダムは百三十歳になって、自分にかたどり、自分のかたちのような男の子を生み、その名をセツと名づけた。
4 Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
アダムがセツを生んで後、生きた年は八百年であって、ほかに男子と女子を生んだ。
5 Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
アダムの生きた年は合わせて九百三十歳であった。そして彼は死んだ。
6 Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
セツは百五歳になって、エノスを生んだ。
7 Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
セツはエノスを生んだ後、八百七年生きて、男子と女子を生んだ。
8 Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
セツの年は合わせて九百十二歳であった。そして彼は死んだ。
9 Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
エノスは九十歳になって、カイナンを生んだ。
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
エノスはカイナンを生んだ後、八百十五年生きて、男子と女子を生んだ。
11 Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
エノスの年は合わせて九百五歳であった。そして彼は死んだ。
12 Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
カイナンは七十歳になって、マハラレルを生んだ。
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
カイナンはマハラレルを生んだ後、八百四十年生きて、男子と女子を生んだ。
14 Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
カイナンの年は合わせて九百十歳であった。そして彼は死んだ。
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
マハラレルは六十五歳になって、ヤレドを生んだ。
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
マハラレルはヤレドを生んだ後、八百三十年生きて、男子と女子を生んだ。
17 Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
マハラレルの年は合わせて八百九十五歳であった。そして彼は死んだ。
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
ヤレドは百六十二歳になって、エノクを生んだ。
19 Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
ヤレドはエノクを生んだ後、八百年生きて、男子と女子を生んだ。
20 Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
ヤレドの年は合わせて九百六十二歳であった。そして彼は死んだ。
21 Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
エノクは六十五歳になって、メトセラを生んだ。
22 Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
エノクはメトセラを生んだ後、三百年、神とともに歩み、男子と女子を生んだ。
23 Henoko aliishi miaka 365.
エノクの年は合わせて三百六十五歳であった。
24 Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
エノクは神とともに歩み、神が彼を取られたので、いなくなった。
25 Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
メトセラは百八十七歳になって、レメクを生んだ。
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
メトセラはレメクを生んだ後、七百八十二年生きて、男子と女子を生んだ。
27 Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
メトセラの年は合わせて九百六十九歳であった。そして彼は死んだ。
28 Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
レメクは百八十二歳になって、男の子を生み、
29 Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
「この子こそ、主が地をのろわれたため、骨折り働くわれわれを慰めるもの」と言って、その名をノアと名づけた。
30 Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
レメクはノアを生んだ後、五百九十五年生きて、男子と女子を生んだ。
31 Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
レメクの年は合わせて七百七十七歳であった。そして彼は死んだ。
32 Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
ノアは五百歳になって、セム、ハム、ヤペテを生んだ。

< Mwanzo 5 >