< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
Here is a list of the descendants of Adam. When God created humans, he caused them to be like him in many ways.
2 Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
He created one man and one woman. He blessed them, and on the day that he created them, he called them ‘human beings’.
3 Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
When Adam was 130 years old, he became the father of a son who [grew up to] be just like him. That was the son he named Seth.
4 Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
After Seth was born, Adam lived 800 more years, and during those years he became the father of other sons and daughters.
5 Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
Adam lived 930 years altogether, and then he died.
6 Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
When Seth was 105 years old, he became the father of Enosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
After Enosh was born, Seth lived 807 more years, and became the father of other sons and daughters.
8 Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
Seth lived 912 years altogether, and then he died.
9 Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
When Enosh was 90 years old, he became the father of Kenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
After Kenan was born, Enosh lived 815 more years and became the father of other sons and daughters.
11 Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
Enosh lived 905 years altogether, and then he died.
12 Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
When Kenan was 70 years old, he became the father of Mahalalel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
After Mahalalel was born, Kenan lived 840 more years and became the father of other sons and daughters.
14 Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
Kenan lived 910 years altogether, and then he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
When Mahalalel was 65 years old, he became the father of Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
After Jared was born, Mahalalel lived 830 more years and became the father of other sons and daughters.
17 Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
Mahalalel lived 895 years altogether, and then he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
When Jared was 162 years old, he became the father of Enoch.
19 Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
Jared lived 800 years after Enoch was born, and he became the father of other sons and daughters.
20 Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
Jared lived 962 years altogether, and then he died.
21 Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
When Enoch was 65 years old, he became the father of Methuselah.
22 Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
Enoch lived in close fellowship with God for 300 years after Methuselah was born, and he became the father of other sons and daughters.
23 Henoko aliishi miaka 365.
Enoch lived 365 years altogether in close fellowship with God.
24 Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
Then one day he disappeared, because God took him away [to be with him in heaven].
25 Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
When Methuselah was 187 years old, he became the father of Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
Methuselah lived 782 years after Lamech was born, and became the father of other sons and daughters.
27 Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
Methuselah lived 969 years altogether, and then he died.
28 Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
When Lamech was 182 years old, he became the father of a son,
29 Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
whom he named Noah, [which sounds like the Hebrew word that means ‘relief’], because he said, “He will bring us relief from all the hard work we have been doing to produce food from the ground that Yahweh cursed.”
30 Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
Lamech lived 595 years after Noah was born and became the father of other sons and daughters.
31 Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
Lamech lived 777 years altogether, and then he died.
32 Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
When Noah was 500 years old, he became the father of a son whom he named Shem. Later he became the father of another son whom he named Ham, and later he became the father of another son whom he named Japheth.

< Mwanzo 5 >