< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
This is the booke of the generations of Adam. In the day that God created Adam, in the likenes of God made he him,
2 Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
Male and female created he them, and blessed them, and called their name Adam in the day that they were created.
3 Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
Nowe Adam liued an hundred and thirtie yeeres, and begate a childe in his owne likenes after his image, and called his name Sheth.
4 Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
And the dayes of Adam, after he had begotten Sheth, were eight hundreth yeeres, and he begate sonnes and daughters.
5 Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
So all the dayes that Adam liued, were nine hundreth and thirtie yeeres: and he died.
6 Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
And Sheth liued an hundreth and fiue yeeres, and begate Enosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
And Sheth liued, after he begate Enosh, eight hundreth and seuen yeeres, and begate sonnes and daughters.
8 Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
So all the dayes of Sheth were nine hundreth and twelue yeeres: and he died.
9 Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Also Enosh liued ninetie yeeres, and begate Kenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
And Enosh liued, after he begate Kenan, eight hundreth and fifteene yeeres, and begate sonnes and daughters.
11 Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
So all the dayes of Enosh were nine hundreth and fiue yeeres: and he died
12 Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Likewise Kenan liued seuentie yeeres, and begate Mahalaleel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
And Kenan liued, after he begate Mahalaleel, eight hundreth and fourtie yeeres, and begate sonnes and daughters.
14 Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
So all the dayes of Kenan were nine hundreth and tenne yeeres: and he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
Mahalaleel also liued sixtie and fiue yeres, and begate Iered.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
Also Mahalaleel liued, after he begate Iered, eight hundreth and thirtie yeeres, and begate sonnes and daughters.
17 Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
So all the dayes of Mahalaleel were eight hundreth ninetie and fiue yeeres: and he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
And Iered liued an hundreth sixtie and two yeeres, and begate Henoch.
19 Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
Then Iered liued, after he begate Henoch, eight hundreth yeeres, and begate sonnes and daughters.
20 Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
So all the dayes of Iered were nine hundreth sixtie and two yeeres: and he died.
21 Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
Also Henoch liued sixtie and fiue yeeres, and begate Methushelah.
22 Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
And Henoch walked with God, after he begate Methushelah, three hundreth yeeres, and begate sonnes and daughters.
23 Henoko aliishi miaka 365.
So all the dayes of Henoch were three hundreth sixtie and fiue yeeres.
24 Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
And Henoch walked with God, and he was no more seene: for God tooke him away.
25 Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
Methushelah also liued an hundreth eightie and seuen yeeres, and begate Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
And Methushelah liued, after he begate Lamech, seuen hundreth eightie and two yeeres, and begate sonnes and daughters.
27 Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
So al the dayes of Methushelah were nine hundreth sixtie and nine yeeres: and he died.
28 Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Then Lamech liued an hundreth eightie and two yeeres, and begate a sonne,
29 Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
And called his name Noah, saying, This same shall comfort vs concerning our worke and sorowe of our hands, as touching the earth, which the Lord hath cursed.
30 Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
And Lamech liued, after he begate Noah, fiue hundreth ninetie and fiue yeeres, and begate sonnes and daughters.
31 Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
So all the dayes of Lamech were seuen hundreth seuentie and seuen yeeres: and he died.
32 Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
And Noah was fiue hundreth yeere olde. And Noah begate Shem, Ham and Iapheth.

< Mwanzo 5 >