< Mwanzo 5 >
1 Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
This is the book of the lineage of Adam. In the day that God created man, he made him to the likeness of God.
2 Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
He created them, male and female; and he blessed them. And he called their name Adam, in the day when they were created.
3 Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
Then Adam lived for one hundred and thirty years. And then he conceived a son in his own image and likeness, and he called his name Seth.
4 Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
And after he conceived Seth, the days of Adam that passed were eight hundred years. And he conceived sons and daughters.
5 Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
And all the time that passed while Adam lived was nine hundred and thirty years, and then he died.
6 Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Seth likewise lived for one hundred and five years, and then he conceived Enos.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
And after he conceived Enos, Seth lived for eight hundred and seven years, and he conceived sons and daughters.
8 Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
And all the days of Seth that passed were nine hundred and twelve years, and then he died.
9 Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
In truth, Enos lived ninety years, and then he conceived Cainan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
After his birth, he lived eight hundred and fifteen years, and he conceived sons and daughters.
11 Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
And all the days of Enos that passed were nine hundred and five years, and then he died.
12 Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Likewise, Cainan lived seventy years, and then he conceived Mahalalel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
And after he conceived Mahalalel, Cainan lived for eight hundred and forty years, and he conceived sons and daughters.
14 Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
And all the days of Cainan that passed were nine hundred and ten years, and then he died.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
And Mahalalel lived sixty-five years, and then he conceived Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
And after he conceived Jared, Mahalalel lived for eight hundred and thirty years, and he conceived sons and daughters.
17 Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
And all the days of Mahalalel that passed were eight hundred and ninety-five years, and then he died.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
And Jared lived for one hundred and sixty-two years, and then he conceived Enoch.
19 Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
And after he conceived Enoch, Jared lived for eight hundred years, and he conceived sons and daughters.
20 Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
And all the days of Jared that passed were nine hundred and sixty-two years, and then he died.
21 Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
Now Enoch lived for sixty-five years, and then he conceived Methuselah.
22 Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
And Enoch walked with God. And after he conceived Methuselah, he lived for three hundred years, and he conceived sons and daughters.
23 Henoko aliishi miaka 365.
And all the days of Enoch that passed were three hundred and sixty-five years.
24 Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
And he walked with God, and then he was seen no more, because God took him.
25 Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
Likewise, Methuselah lived for one hundred and eighty-seven years, and then he conceived Lamech.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
And after he conceived Lamech, Methuselah lived for seven hundred and eighty-two years, and he conceived sons and daughters.
27 Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
And all the days of Methuselah that passed were nine hundred and sixty-nine years, and then he died.
28 Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Then Lamech lived for one hundred and eighty-two years, and he conceived a son.
29 Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
And he called his name Noah, saying, “This one will console us from the works and hardships of our hands, in the land that the Lord has cursed.”
30 Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
And after he conceived Noah, Lamech lived for five hundred and ninety-five years, and he conceived sons and daughters.
31 Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
And all the days of Lamech that passed were seven hundred and seventy-seven years, and then he died.
32 Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
In truth, when Noah was five hundred years old, he conceived Shem, Ham, and Japheth.