< Mwanzo 33 >

1 Yakobo akainua macho yake na, tazama, Esau alikuwa anakuja, na alikuwa na watu mia nne pamoja naye. Yakobo akawagawanya watoto kati ya Lea, Raheli, na wale wajakazi wawili.
And Jacob lifts up his eyes, and looks, and behold, Esau is coming, and with him four hundred men; and he divides the children to Leah, and to Rachel, and to the two maidservants;
2 Kisha akawaweka wajakazi na wanao mbele, wakifuatiwa na Lea na watoto wake, Raheli na Yusufu wakafuata mwisho wa wote.
and he sets the maidservants and their children first, and Leah and her children behind, and Rachel and Joseph last.
3 Yeye mwenyewe akatangulia mbele yao. Akasujudu mara saba kuelekea ardhi, hata alipomkaribia ndugu yake.
And he himself passed over before them, and bows himself to the earth seven times, until his drawing near to his brother,
4 Esau akakimbia kumlaki, akamkumbatia, akakumbatia shingo yake na kumbusu. Kisha wakalia.
and Esau runs to meet him, and embraces him, and falls on his neck, and kisses him, and they weep;
5 Esau alipoinua macho, aliona wanawake na watoto. Akauliza, “Hawa watu pamoja nawe ni kinanani?” Yakobo akasema, Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako kwa neema.”
and he lifts up his eyes, and sees the women and the children, and says, “What [are] these to you?” And he says, “The children with whom God has favored your servant.”
6 Kisha wajakazi wakakaribia pamoja na watoto wao, nao wakasujudia.
And the maidservants draw near, they and their children, and bow themselves;
7 Akafuata Lea pia na watoto wake wakaja na kusujudia. Mwisho Yusufu na Raheli wakaja na kusujudia.
and Leah also draws near, and her children, and they bow themselves; and afterward Joseph has drawn near with Rachel, and they bow themselves.
8 Esau akasema, Unamaanisha nini kwa makundi haya yote niliyokutana nayo?” Yakobo akasema, “Kutafuta kibali mbele za bwana wangu.
And he says, “What to you [is] all this camp which I have met?” And he says, “To find grace in the eyes of my lord.”
9 Esau akasema, “Ninayo ya kutosha, ndugu yangu. Tunza uliyonayo kwa ajili yako mwenyewe.”
And Esau says, “I have abundance, my brother, that which you have, let it be for yourself.”
10 Yakobo akasema, “Hapana, tafadhari, ikiwa nimeona kibali mbele zako, basi upokee zawadi yangu kutoka mkononi mwangu, na ni kama kuona uso wa Mungu, na umenipokea.
And Jacob says, “No, please, now if I have found grace in your eyes, then you have received my present from my hand, because that I have seen your face, as the seeing of the face of God, and you are pleased with me;
11 Tafadhari pokea zawadi yangu uliyoletewa, kwa sababu Mungu amenitendea kwa neema, na kwa sababu ninavyo vya kutosha.” Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali.
please receive my blessing which is brought to you, because God has favored me, and because I have all [things]”; and he presses on him, and he receives [it],
12 Kisha Esau akasema, “Haya na tuondoke. Nitakutangulia.”
and says, “Let us journey and go on, and I go on before you.”
13 Yakobo akamwambia, “Bwana wangu anajua kwamba watoto ni wadogo, na kwamba kondoo na ng'ombe wananyonyesha ndama wao. Ikiwa watapelekwa kwa haraka hata siku moja, wanyama wote watakufa.
And he says to him, “My lord knows that the children [are] tender, and the suckling flock and the herd [are] with me; when they have beaten them one day, then all the flock has died.
14 Tafadhari bwana wangu na amtangulie mtumishi wake. Nitasafiri polopole, kwa kadili ya mifugo iliyo mbele yangu, na kadili ya watoto, hata nitakapofika kwa bwana wangu huko Seiri.”
Please let my lord pass over before his servant, and I lead on gently, according to the foot of the work which [is] before me, and to the foot of the children, until I come to my lord, to Seir.”
15 Esau akasema, haya nikuachie baadhi ya watu wangu waliopamoja nami.” Yakobo akasema, “Kwa nini kufanya hivyo? Bwana wangu amekuwa mkalimu kwangu kiasi cha kutosha.”
And Esau says, “Please let me place with you some of the people who [are] with me”; and he said, “Why [is] this? I find grace in the eyes of my lord.”
16 Hivyo Esau akaanza kurudi Seiri.
And Esau turns back on that day on his way to Seir;
17 Yakobo akasafiri kuelekea Sukothi, akajijengea nyumba, na akafanya mazizi kwa ajili ya mifugo wake. Hivyo jina la eneo linaitwa Sukothi.
and Jacob has journeyed to Succoth, and builds a house for himself, and has made shelters for his livestock, therefore he has called the name of the place Succoth.
18 Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu, akafika salama katika mji wa Shekemu, uliyo katika nchi ya Kanaani. Akapiga kambi karibu na mji.
And Jacob comes safe [to the] city of Shechem, which [is] in the land of Canaan, in his coming from Padan-Aram, and encamps before the city,
19 Kisha akanunu sehemu ya ardhi alipokuwa ameweka hema yake kutoka kwa wana wa Hamori, baba wa Shekemu, kwa vipande mia vya fedha.
and he buys the portion of the field where he has stretched out his tent, from the hand of the sons of Hamor, father of Shechem, for one hundred kesitah;
20 Akajenga madhabahu pale na kuiita El Elohe Israeli.
and he sets up there an altar, and proclaims at it God—the God of Israel.

< Mwanzo 33 >