< Mwanzo 32 >

1 Yakobo pia akaendelea na safari yake, na malaika wa Mungu wakakutana naye.
And Jacob has gone on his way, and messengers of God come on him;
2 Yakobo alipowaona, akasema, “Hii ni kambi ya Mungu,” hivyo akapaita mahali pale Mahanaimu.
and Jacob says, when he has seen them, “This [is] the camp of God”; and he calls the name of that place “Two Camps.”
3 Yakobo akatuma wajumbe mbele yake waende kwa Esau ndugu yake katika nchi ya Seiri, katika eneo la Edomu.
And Jacob sends messengers before him to his brother Esau, toward the land of Seir, the field of Edom,
4 Aliwaagiza, kusema, “Hivi ndivyo mtakavyosema kwa bwana wangu Esau: Hivi ndivyo mtumishi wako Yakobo asemavyo: 'Nimekuwa nikikaa na Labani, naye amekawilisha kurudi kwangu hata sasa.
and commands them, saying, “Thus you say to my lord, to Esau, Thus said your servant Jacob: I have sojourned with Laban, and I linger until now;
5 Nina ng'ombe, punda, na kondoo, wajori na wajakazi. Nimetuma ujumbe huu kwa bwana wangu, ili kwamba nipate kibali mbele zako.”
and I have ox, and donkey, flock, and manservant, and maidservant, and I send to declare to my lord, to find grace in his eyes.”
6 Wajumbe wakarudi kwa Yakobo na kusema, “Tulikwenda kwa Esau ndugu yako. Anakuja kukulaki, na watu mia nne pamoja naye.”
And the messengers return to Jacob, saying, “We came to your brother, to Esau, and he is also coming to meet you, and four hundred men with him”;
7 Ndipo Yakobo alipoogopa sana na kutaabika. Hivyo akagawanya watu aliokuwa nao katika kambi mbili, na kondoo pia, mbuzi na ngamia.
and Jacob fears exceedingly, and is distressed, and he divides the people who [are] with him, and the flock, and the herd, and the camels, into two camps,
8 Akasema, “Ikiwa Esau ataishambulia kambi moja, ndipo kambi nyingine itakaposalimika.”
and says, “If Esau comes to one camp, and has struck it—then the camp which is left has been for an escape.”
9 Yakobo akasema, “Mungu wa baba yangu Ibrahimu, na Mungu wa baba yangu Isaka, Yahwe, uliyeniambia, 'Rudi katika nchi yako na kwa jamaa yako, nami nitakustawisha,'
And Jacob says, “God of my father Abraham and God of my father Isaac, YHWH who says to me, Return to your land and to your family, and I do good with you:
10 Mimi sistahili matendo yako yote ya agano la uaminifu na ustahilifu wote uliomfanyia mtumishi wako. Kwa maana nilikuwa na fimbo tu nilipovuka mto huu wa Yordani, na sasa nimekuwa matuo mawili.
I have been unworthy of all the kind acts and of all the truth which You have done with your servant—for with my staff I passed over this Jordan, and now I have become two camps.
11 Tafadhari niokoe kutoka katika mikono ya ndugu yangu, mikono ya Esau, kwa maana namwogopa, kwamba atakuja na kunishambulia mimi na wamama na watoto.
Please deliver me from the hand of my brother, from the hand of Esau: for I am fearing him, lest he come and has struck me—mother beside sons;
12 Lakini ulisema, 'hakika nitakufanya ufanikiwe. Nitaufanya uzao wako kuwa kama mchanga wa bahari, ambao hauwezi kuhesabika kwa hesabu yake.”
and You have said, I certainly do good with you, and have set your seed as the sand of the sea, which is not numbered because of the multitude.”
13 Yakobo akakaa pale usiku huo. Akachukua baadhi ya alivyokuwa navyo kama zawadi kwa Esau, ndugu yake:
And he lodges there during that night, and takes from that which is coming into his hand, a present for his brother Esau:
14 mbuzi majike mia mbili na mabeberu ishirini, kondoo majike mia mbili na madume ya kondoo ishirini,
female goats two hundred, and male goats twenty, ewes two hundred, and rams twenty,
15 ngamia wakamwao thelathini na wana wao, ng'ombe madume arobaini na madume kumi ya ng'ombe, punda wa kike ishirini na madume yake ishirini.
suckling camels and their young ones thirty, cows forty, and bullocks ten, female donkeys twenty, and foals ten;
16 Akawaweka katika mikono ya watumishi wake, kila kundi peke yake. Akawambia watumishi, “Tangulieni mbele yangu na mwache nafasi kati ya makundi ya wanyama.”
and he gives into the hand of his servants every drove by itself, and says to his servants, “Pass over before me, and a space you put between drove and drove.”
17 Akamwagiza mtumishi wa kwanza, akisema, “Ndugu yangu Esau atakapokutana nawe na kukuuliza, akasema, 'Ninyi ni wa nani? Mnakwenda wapi? Na wanyama hawa mbele yenu ni wa nani?
And he commands the first, saying, “When my brother Esau meets you, and has asked you, saying, Whose [are] you? And to where do you go? And whose [are] these before you?
18 Ndipo umwambie, 'Ni wa mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi wanaopelekwa kwa bwana wangu Esau. Na tazama, yeye pia anakuja nyuma yetu.”
Then you have said, Your servant Jacob’s: it [is] a present sent to my lord, to Esau; and behold, he also [is] behind us.”
19 Yakobo akatoa maelekezo kwa kundi la pili pia, la tatu, na watu wote walioyafuata makundi ya wanyama. Akasema, mseme vilevile kwa Esau mtakapokutana naye.
And he commands also the second, also the third, also all who are going after the droves, saying, “According to this manner do you speak to Esau in your finding him,
20 Mnapaswa pia kusema, 'mtumwa wako Yakobo pia anakuja nyuma yetu.” Kwani alifikiri, “nitamtuliza Esau kwa zawadi nilizozituma mbele yangu. Kisha baadaye, nitakapomwona, bila shaka atanipokea.”
and you have also said, Behold, your servant Jacob [is] behind us”; for he said, “I pacify his face with the present which is going before me, and afterward I see his face; it may be he lifts up my face”;
21 Hivyo zawadi zikatangulia mbele yake. Yeye mwenyewe akakaa kambini usiku huo
and the present passes over before his face, and he has lodged during that night in the camp.
22 Yakobo akaamka wakati wa usiku, na akawachukua wakeze, wajakazi wake na wanaye kumi na wawili. Akawawavusha kijito cha Yaboki.
And he rises in that night, and takes his two wives, and his two maidservants, and his eleven children, and passes over the passage of Jabbok;
23 Kwa njia hii akawapeleka kupitia chemichemi pamoja na mali yake yote.
and he takes them, and causes them to pass over the brook, and he causes that which he has to pass over.
24 Yakobo akaachwa peke yake, na mtu akashindana naya mpaka alfajiri.
And Jacob is left alone, and One wrestles with him until the ascending of the dawn;
25 Mtu yule alipoona kwamba hawezi kumshinda, akalipiga paja lake. Paja la Yakobo likatenguka alipokuwa akishindana naye.
and He sees that He is not able for him, and He comes against the hollow of his thigh, and the hollow of Jacob’s thigh is disjointed in his wrestling with Him;
26 Yule mtu akasema, “Niache niende, kwani kunakucha.” Yakobo akasema, sitakuacha uende mpaka uwe umenibariki.”
and He says, “Send Me away, for the dawn has ascended”: and he says, “I do not send You away, except You have blessed me.”
27 Yule mtu akamwuliza, “Jina lako ni nani?” Yakobo akasema, “Yakobo.” Yule mtu akasema,
And He says to him, “What [is] your name?” And he says, “Jacob.”
28 “Jina lako halitakuwa Yakobo tena, ila Israeli. Kwa kuwa umeshindana na Mungu na wanadamu na umeshinda.”
And He says, “Your name is no longer called Jacob, but Israel; for you have reigned with God and with men, and prevail.”
29 Yakobo akamwambia, “Tafadhari niambie jina lako.” Akasema, “Kwa nini kuniuliza jina langu?” Kisha akambariki pale.
And Jacob asks and says, “Please declare Your Name”; and He says, “Why [is] this, you ask for My Name?” And He blesses him there.
30 Yakobo akapaita mahali pale Penieli kwani alisema, “Nimemwona Mungu uso kwa uso, na maisha yangu yamesalimika.”
And Jacob calls the name of the place Peniel: “For I have seen God face to face, and my life is delivered”;
31 Jua likatoka wakati Yakobo anaipita Penieli. Alikuwa akichechemea kwa sababu ya paja lake.
and the sun rises on him when he has passed over Penuel, and he is halting on his thigh;
32 Ndiyo maana wana wa Israeli hawali kano ya paja iliyopo katika nyonga ya paja, kwa sababu yule mtu aliziumiza hizo kano alipotegua paja la Yakobo.
therefore the sons of Israel do not eat the sinew which shrank, which [is] on the hollow of the thigh, to this day, because He came against the hollow of Jacob’s thigh, against the sinew which shrank.

< Mwanzo 32 >