< Mwanzo 11 >

1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
ויהי כל הארץ שפה אחת ודברים אחדים
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
ויהי בנסעם מקדם וימצאו בקעה בארץ שנער וישבו שם
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
ויאמרו איש אל רעהו הבה נלבנה לבנים ונשרפה לשרפה ותהי להם הלבנה לאבן והחמר היה להם לחמר
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
ויאמרו הבה נבנה לנו עיר ומגדל וראשו בשמים ונעשה לנו שם פן נפוץ על פני כל הארץ
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
וירד יהוה לראת את העיר ואת המגדל אשר בנו בני האדם
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
ויאמר יהוה הן עם אחד ושפה אחת לכלם וזה החלם לעשות ועתה לא יבצר מהם כל אשר יזמו לעשות
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
הבה נרדה ונבלה שם שפתם--אשר לא ישמעו איש שפת רעהו
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
ויפץ יהוה אתם משם על פני כל הארץ ויחדלו לבנת העיר
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
על כן קרא שמה בבל כי שם בלל יהוה שפת כל הארץ ומשם הפיצם יהוה על פני כל הארץ
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
אלה תולדת שם--שם בן מאת שנה ויולד את ארפכשד שנתים אחר המבול
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי שם אחרי הולידו את ארפכשד חמש מאות שנה ויולד בנים ובנות
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
וארפכשד חי חמש ושלשים שנה ויולד את שלח
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי ארפכשד אחרי הולידו את שלח שלש שנים וארבע מאות שנה ויולד בנים ובנות
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
ושלח חי שלשים שנה ויולד את עבר
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי שלח אחרי הולידו את עבר שלש שנים וארבע מאות שנה ויולד בנים ובנות
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
ויחי עבר ארבע ושלשים שנה ויולד את פלג
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי עבר אחרי הולידו את פלג שלשים שנה וארבע מאות שנה ויולד בנים ובנות
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
ויחי פלג שלשים שנה ויולד את רעו
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי פלג אחרי הולידו את רעו תשע שנים ומאתים שנה ויולד בנים ובנות
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
ויחי רעו שתים ושלשים שנה ויולד את שרוג
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי רעו אחרי הולידו את שרוג שבע שנים ומאתים שנה ויולד בנים ובנות
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
ויחי שרוג שלשים שנה ויולד את נחור
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי שרוג אחרי הולידו את נחור--מאתים שנה ויולד בנים ובנות
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
ויחי נחור תשע ועשרים שנה ויולד את תרח
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
ויחי נחור אחרי הולידו את תרח תשע עשרה שנה ומאת שנה ויולד בנים ובנות
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
ויחי תרח שבעים שנה ויולד את אברם את נחור ואת הרן
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
ואלה תולדת תרח--תרח הוליד את אברם את נחור ואת הרן והרן הוליד את לוט
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
וימת הרן על פני תרח אביו בארץ מולדתו באור כשדים
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
ויקח אברם ונחור להם נשים שם אשת אברם שרי ושם אשת נחור מלכה בת הרן אבי מלכה ואבי יסכה
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
ותהי שרי עקרה אין לה ולד
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
ויקח תרח את אברם בנו ואת לוט בן הרן בן בנו ואת שרי כלתו אשת אברם בנו ויצאו אתם מאור כשדים ללכת ארצה כנען ויבאו עד חרן וישבו שם
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
ויהיו ימי תרח חמש שנים ומאתים שנה וימת תרח בחרן

< Mwanzo 11 >