< Ezekieli 2 >

1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
And he said to me O son of humankind stand on feet your so I may speak you.
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
And it came in me a spirit just when he spoke to me and it made stand up me on feet my and I heard [one who] spoke to me.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
And he said to me O son of humankind [am] sending I you to [the] people of Israel to nations rebellious which they have rebelled against me they and ancestors their they have transgressed against me until [the] substance of the day this.
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And the children [are] stern of face and hard of heart I [am] sending you to them and you will say to them thus he says [the] Lord Yahweh.
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
And they whether they will listen and or they will refrain for [are] a house of rebellion they and they will know that a prophet he has been in midst of them.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
And you O son of humankind may not you be afraid from them and from words their may not you be afraid for nettles and thorns with you and to scorpions you [are] dwelling from words their may not you be afraid and from faces their may not you be dismayed for [are] a house of rebellion they.
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
And you will speak words my to them whether they will listen and or they will refrain for [are] rebellious they.
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
And you O son of humankind hear [that] which I [am] speaking to you may not you be rebellious like [the] house of rebellion open mouth your and eat [that] which I [am] giving to you.
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
And I saw and there! a hand [was] stretched out to me and there! [was] in it a scroll of a document.
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
And he spread out it before me and it [was] written face and back and [was] written to it lamentations and moaning and wailing.

< Ezekieli 2 >