< Kutoka 39 >
1 Na kutokana na ule uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili wakafanya mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Basi wakafanya yale mavazi matakatifu yaliyokuwa kwa ajili ya Aruni, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
Avec la pourpre violette, la pourpre écarlate et le cramoisi, on fit les vêtements de cérémonie peur le service dans le sanctuaire, et on fit les vêtements sacrés pour Aaron, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
2 Basi akaifanya ile naivera ya dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
On fit l’éphod d’or, de pourpre violette, de pourpre écarlate, de cramoisi et de lin retors.
3 Kisha wakafua mabamba ya dhahabu yawe mabamba membamba, naye akakata nyuzi za kufuma pamoja na ule uzi wa bluu na ile sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kile kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kile kitani bora, kama kazi ya mjenzi.
On étendit l’or en lames et on les coupa en fils, que l’on entrelaça dans la pourpre violette, la pourpre écarlate, le cramoisi et le fin lin; ouvrage de dessin varié.
4 Wakaifanyia vipande vya begani vilivyounganishwa. Iliunganishwa kwenye miisho yake miwili.
On fit des épaulettes pour le joindre, et ainsi il était joint à ses deux extrémités.
5 Nao mshipi, uliokuwa juu yake ili kuifunga, ulikuwa wa kitambaa kilekile kulingana na ufundi wake, wa dhahabu, uzi wa bluu, na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
La ceinture pour attacher l’éphod en passant dessus faisait corps avec lui et était du même travail; elle était d’or, de pourpre violette, de pourpre écarlate, de cramoisi et de lin retors, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
6 Kisha wakafanya mawe ya shohamu yaliyopangwa kwenye mapambo ya dhahabu, yaliyochongwa kwa michoro ya muhuri kulingana na majina ya wana wa Israeli.
On fit les pierres d’onyx enchâssées dans des chatons d’or, sur lesquelles on grava les noms des fils d’Israël, comme on grave les cachets.
7 Bezaleli akayaweka kwenye vile vipande vya begani vya naivera yawe mawe ya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli, kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa.
On les plaça sur les épaulettes de l’éphod comme pierres de souvenir pour les enfants d’Israël, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
8 Kisha akafanya kile kifuko cha kifuani kwa ufundi wa mjenzi, kama ule ufundi wa naivera, kutokana na dhahabu, uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa.
On fit le pectoral, artistement travaillé, du même travail que l’éphod, d’or, de pourpre violette, de pourpre écarlate, de cramoisi et de lin retors.
9 Kilikuwa mraba kilipokunjwa. Walikifanya kile kifuko cha kifuani, kinapokunjwa, shubiri moja urefu wake na shubiri moja upana wake.
Il était carré; on fit le pectoral double; sa longueur était d’un empan et sa largeur d’un empan; il était double.
10 Kisha wakakijaza kwa mistari minne ya mawe. Mstari wa zabarijadi, topazi na zumaridi ulikuwa mstari wa kwanza.
On le garnit de quatre rangées de pierres: une rangée de sardoine, de topaze, d’émeraude: première rangée;
11 Nao mstari wa pili ulikuwa feruzi, yakuti na yaspi.
deuxième rangée: une escarboucle, un saphir, un diamant;
12 Nao mstari wa tatu ulikuwa jiwe la leshemi, akiki na amethisti.
troisième rangée: une opale, une agate, une améthyste;
13 Nao mstari wa nne ulikuwa krisolito na shohamu na yashefi. Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu katika mahali pake.
quatrième rangée: une chrysolithe, un onyx, un jaspe. Ces pierres étaient entourées de rosettes d’or dans leurs garnitures.
14 Na mawe hayo yalikuwa kulingana na majina ya wana wa Israeli. Yalikuwa kumi na mawili kulingana na majina yao, kwa michongo ya muhuri, kila moja kulingana na jina lake kwa ajili ya yale makabila kumi na mawili.
Les pierres étaient selon les noms des fils d’Israël, douze selon leurs noms; elles étaient gravées comme des cachets, chacune avec son nom, pour les douze tribus. —
15 Nao wakafanya juu ya kile kifuko cha kifuani minyororo yenye mashada, msokoto wa kamba, wa dhahabu safi.
On fit pour le pectoral des chaînettes d’or pur, tressées en forme de cordons.
16 Kisha wakafanya mapambo mawili ya dhahabu na pete mbili za dhahabu na kuziweka hizo pete mbili kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani.
On fit deux chatons d’or et deux anneaux d’or, et on mit les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
17 Baada ya hilo wakapitisha zile kamba mbili za dhahabu kwenye zile pete mbili zilizo kwenye miisho ya kile kifuko cha kifuani.
On passa les deux cordons d’or dans les deux anneaux, aux extrémités du pectoral,
18 Nao wakapitisha ile miisho miwili ya zile kamba mbili kwenye yale mapambo mawili. Halafu wakaiweka juu ya vile vipande vya begani vya naivera, mbele yake.
et l’on attacha les deux bouts des deux cordons aux deux chatons, et on les plaça sur les épaulettes de l’éphod, par devant.
19 Kisha wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka kwenye ile miisho miwili ya kile kifuko cha kifuani kwenye upindo wake ulio upande unaoelekea ile efodi upande wa ndani.
On fit encore deux anneaux d’or, que l’on mit aux deux extrémités inférieures du pectoral, sur le bord intérieur appliqué contre l’éphod.
20 Halafu wakafanya pete mbili za dhahabu na kuziweka juu ya vile vipande viwili vya begani vya efodi upande wake wa chini, sehemu yake ya mbele, karibu na mahali pake pa kuungania, juu ya ule mshipi wa naivera.
On fit deux autres anneaux d’or, que l’un mit au bas des deux épaulettes de l’éphod sur le devant, près de l’attache, au-dessus de la ceinture de l’éphod.
21 Mwishowe wakakifunga kile kifuko cha kifuani kwa pete zake kwenye zile pete za efodi kwa uzi wa bluu, ili kipate kuwa juu ya mshipi wa efodi na kile kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
On attacha le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l’éphod avec un ruban de pourpre violette, afin que le pectoral fût au-dessus de la ceinture de l’éphod; et le pectoral ne pouvait se séparer de l’éphod, comme Yahweh l’a ordonné à Moïse.
22 Bezaleli akafanya lile koti la naivera, lote la uzi wa zambarau, kazi ya mshonaji.
On fit la robe de l’éphod, œuvre du tisseur, tout entière en pourpre violette.
23 Na sehemu wazi ya hilo koti ilikuwa katikati yake, kama sehemu wazi ya vazi la chuma. Sehemu hiyo iliyo wazi ilikuwa na ukingo kuizunguka pande zote ili isiraruke.
Il y avait, au milieu de la robe de l’éphod, une ouverture semblable à celle d’une cotte d’arme, et cette ouverture avait un rebord tissé tout autour, afin que la robe ne se déchirât pas.
24 Halafu wakafanya kwenye upindo wa hilo koti makomamanga ya uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, vilivyosokotwa pamoja.
On mit au bord inférieur de la robe des grenades de pourpre violette, de pourpre écarlate, de cramoisi, de lin retors;
25 Wakafanya kengele za dhahabu safi na kuziweka kengele hizo katikati ya makomamanga kwenye upindo wa lile koti kuzunguka pande zote, katikati ya makomamanga;
on fit des clochettes d’or pur, et l’on mit ces clochettes au milieu des grenades, sur le bord inférieur de la robe tout autour, au milieu des grenades:
26 kengele na komamanga, kengele na komamanga kwenye upindo wa hilo koti kuzunguka pande zote, kwa ajili ya kuhudumu, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
une clochette et une grenade, une clochette et une grenade, sur le bord de la robe tout autour, pour le service, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
27 Kisha wakafanya zile kamba za kitani bora, kwa ajili ya Haruni na wanawe.
On fit les tuniques de lin, œuvre du tisseur, pour Aaron et pour ses fils;
28 Na kile kilemba cha kitani bora na yale mavalio ya kichwani ya mapambo ya kitani bora na zile suruali za kitani bora kilichosokotwa,
la tiare de lin, et les mitres de lin servant de parure; les caleçons blancs de lin retors;
29 na ule ukumbuu wa kitani bora kilichosokotwa na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili, kazi ya mfumaji, kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
la ceinture de lin retors, en pourpre violette, en pourpre écarlate et en cramoisi, damassée, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
30 Mwishowe wakafanya lile bamba linalong’aa, ishara takatifu ya wakfu, kutokana na dhahabu safi na kuandika juu yake maandishi kwa mchongo wa muhuri: “Utakatifu kwa Yahweh.”
On fit d’or pur la lame, diadème sacré, et l’on y grava, comme on grave sur un cachet: Sainteté à Yahweh.
31 Kisha wakalitia uzi wa bluu ili waliweke juu ya kile kilemba upande wa juu. Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa.
On l’attacha avec un ruban de pourpre violette pour la placer sur la tiare, en haut, comme Yahweh l’avait ordonné à Moïse.
32 Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake. Kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
Ainsi fut achevé tout l’ouvrage de la Demeure, de la tente de réunion; et les enfants d’Israël exécutèrent tout selon ce que Yahweh avait ordonné à Moïse; ils firent ainsi.
33 Nao wakaileta maskani kwa Musa, lile hema pamoja na vyombo vyake vyote, kulabu zake, viunzi vyake vya mbao, miti yake na nguzo zake na vikalio vyake,
On présenta la Demeure à Moïse, la tente et tous ses ustensiles, ses agrafes, ses planches, ses traverses, ses colonnes et ses socles;
34 na kifuniko chake cha ngozi za kondoo-dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko chake cha ngozi za sili na pazia la kisitiri,
la couverture de peaux de béliers teintes en rouge, la couverture de peaux de veaux marins et le voile de séparation;
35 na sanduku la ushuhuda na miti yake na kifuniko.
l’arche du témoignage avec ses barres et le propitiatoire;
36 Wakaleta meza, vyombo vyake vyote, na ule mkate wa wonyesho,
la table avec tous ses ustensiles et les pains de proposition;
37 kile kinara cha taa cha dhahabu safi, taa zake, ule mstari wa taa, na vyombo vyake vyote na yale mafuta ya kuangazia taa,
le chandelier d’or pur, ses lampes, les lampes à y ranger, tous ses ustensiles et l’huile pour le luminaire;
38 na madhabahu ya dhahabu na yale mafuta yanayotumiwa kutia mafuta na ule uvumba uliotiwa manukato na kile kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema,
l’autel d’or, l’huile d’onction et le parfum pour l’encens, ainsi que le rideau pour l’entrée de la tente;
39 ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, miti yake na vyombo vyake vyote, ile beseni na kinara chake,
l’autel d’airain, sa grille d’airain, ses barres et tous ses ustensiles; la cuve avec sa base; les rideaux du parvis, ses colonnes, ses socles,
40 Wakaleta mapazia ya ua, nguzo zake na vikalio vyake na kile kisitiri kwa ajili ya lango la ua, kamba zake za hema na misumari yake ya hema na vyombo vyote kwa ajili ya utumishi wa maskani, kwa ajili ya hema ya kukutania.
la tenture de la porte du parvis, ses cordages et ses pieux, et tous les ustensiles pour le service de la Demeure, pour la tente de réunion;
41 Wakaleta yale mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika patakatifu, yale mavazi matakatifu kwa ajili ya Aruni kuhani na mavazi ya wanawe ya kutumikia wakiwa makuhani.
les vêtements de cérémonie pour le service du sanctuaire, les vêtements sacrés pour le grand prêtre Aaron, et les vêtements de ses fils pour les fonctions du sacerdoce.
42 Kulingana na yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa, hivyo ndivyo wana wa Israeli walivyoufanya utumishi wote.
Les enfants d’Israël avaient fait tout cet ouvrage conformément à tout ce que Yahweh avait ordonné à Moïse.
43 Naye Musa akaiona ile kazi yote, na, tazama, walikuwa wameifanya kama vile Yahweh alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya. Basi Musa akawabariki.
Moïse examina tout l’ouvrage, et voici, ils l’avaient exécuté; ils l’avaient fait comme Yahweh l’avait ordonné. Et Moïse les bénit.