< Mambo ya Walawi 22 >

1 Yahweh akazungumza na Musa, kusema,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
2 “Ongea na Aroni na wanawe, waambie wajiepushe na vitu vitakatifu vya watu wa Israeli wanavyovitenga kwangu. Wasilinajisi jina langu. Mimi ndimi Yahweh.
« Parle à Aaron et à ses fils, afin qu’ils s’abstiennent des choses saintes que me consacrent les enfants d’Israël, et qu’ils ne profanent pas mon saint nom. Je suis Yahweh.
3 Waambie, 'Ikiwa mmoja wa wazao wenu katika vizazi vyenu vyote anakaribia vitu vitakatiifu vile ambavyo watu wa Israeli wamevitenga kwa Yahweh, wakati akiwa najisi, sharti mtu huyo akatiliwe mbali atoke mbele zangu. Mimi ndimi Yahweh.
Dis-leur: Tout homme de votre race qui, dans toutes vos générations, ayant sur lui quelque impureté, s’approchera des choses saintes que les enfants d’Israël consacrent à Yahweh, sera retranché de devant moi. Je suis Yahweh.
4 Hatakuwapo yeyote wa uzao wa Aroni aliye na ungonjwa wa ngozi wa kuambukiza, au maambukizi yatirirkayo kutoka mwilini mwake, atakayekula sehemu yoyote ya dhabihu inatolewayo kwa Yahweh mpaka atakapotakasika. Yeyote agusaye kitu chochote kilichonajisi kwa njia ya kugusa maiti, au kwa kumgusa mtu yeyote aliyetokwa na shahawa,
Tout homme de la race d’Aaron qui aura la lèpre ou une gonorrhée, ne mangera pas des choses saintes, jusqu’à ce qu’il soit pur. Il en sera de même de celui qui aura touché une personne souillée par le contact d’un cadavre, de celui qui aura eu un épanchement séminal,
5 au yeyote agusaye mnyama atakayemtia unajisi, au mtu yeyote atakayemfanya najisi, kwa hiyo unajisi wowote unaweza kuwa—
de celui qui aura touché soit un animal rampant qui l’ait rendu impur, soit un homme impur qui lui ait communiqué sa souillure quelle qu’elle soit.
6 kuhani yeyote agusaye kitu chochote kisichosafi atakuwa najisi hata jioni. Hatakula chochote cha vitu vitakatifu, isipokuwa ameuosha mwili wake katika maji.
Celui qui touchera ces choses sera impur jusqu’au soir et il ne mangera pas des choses saintes; mais il baignera son corps dans l’eau
7 Jua linapotua, ndipo atakuwa safi. Baada ya machweo anaweza kula kutoka katika vitu vitakatifu, kwasababu hivyo ni vyakuala vyake.
et, après le coucher du soleil, il sera pur; il pourra manger alors des choses saintes, car c’est sa nourriture.
8 Asile mzoga wowote uliookotwa au mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori, ambaye kwake atajitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh.
Il ne mangera pas d’une bête morte ou déchirée, de manière à être souillé par elle; je suis Yahweh.
9 Ni lazima makuhani wafuate maagizo yangu, ama sivyo watakuwa na hatia ya dhambi na wangeweza kufa kwa kunitia unajisi. Mimi ndimi Yahweh ninayewafanya wao watakatifu.
Ils observeront mes commandements, de peur qu’ils ne se chargent d’un péché à ce sujet, et qu’ils ne meurent pour avoir profané les choses saintes. Je suis Yahweh, qui les sanctifie.
10 Hakuna mtu kutoka nje ya familia ya kuahani, wakiwemo wageni wa kuhani au watumwa wake wa kuajiliwa, atakayeweza kula kitu chochote kilicho kitakatifu.
Aucun étranger ne mangera des choses saintes; celui qui demeure chez un prêtre et le mercenaire ne mangeront point des choses saintes.
11 Lakini kama huyo kuhani amenunua mtumwa kwa fedha yake mwenyewe, mtumwa huyo anaweza kula kutoka katika vitu vilivyotengwa kwa Yahweh. Na watu wa familia ya kuhani na watumwa waliozaliwa nyumbani mwake, pia wanaweza kula pamoja naye kutoka katika vitu hivyo.
Mais un esclave acquis par le prêtre à prix d’argent pourra en manger; il en est de même de celui qui est né dans sa maison: ils mangeront de sa nourriture.
12 Ikiwa binti wa kuhani ameolewa na mtu asiye kuhani, hataweza kula chochote cha mchango wa matoleo matakatifu.
La fille d’un prêtre, mariée à un étranger, ne mangera pas de ce qui a été prélevé sur les choses saintes.
13 Lakini ikiwa huyo binti wa kuhani ni mjane au ametalikiwa, na ikiwa hana mtoto, na anarudi kuishi knyumbani kwa baba yake kama alivyokuwa wakati wa ujana wake, anaweza kula kutoka katika chakula cha baba yake. Lakini hakuna yeyote asiye wa familia ya kikuhani anatakayeruhusiwa kula kutoka katika chakula cha kuhani.
Mais si la fille d’un prêtre, devenue veuve ou répudiée, sans avoir d’enfants, retourne dans la maison de son père, comme elle y était dans sa jeunesse, elle pourra manger de la nourriture de son père; mais aucun étranger n’en mangera.
14 Kama mtu anakula chakula kitakatifu bila ya kukijua, naye atamlipa kuahani kwa ajili ya hicho; itampasa kuongeza moja ya tano juu yake na kukirejesha kwa kuhani.
Si un homme mange par erreur d’une chose sainte, il restituera au prêtre la valeur de la chose sainte, en y ajoutant un cinquième.
15 Haiwapasi watu wa Israeli kutoheshimu vitu vitakatifu ambavyo vimeinuliwa juu na kuletwa kwa Yahweh,
Les prêtres ne profaneront point les choses saintes des enfants d’Israël, ce qu’ils ont prélevé pour Yahweh,
16 kisha wakajisababishia wenyewe kuchukua dhambi amabyo ingewafanya kuwa na hatia ya kula chakula kitakatifu, kwa kuwa mimi ndimi Yahweh awafanyaye wao watakatifu.”
et ne leur feront pas porter le poids de la faute qu’ils commettraient en mangeant leurs choses saintes; car je suis Yahweh, qui les sanctifie. »
17 Yahweh akazungumza na Musa, akasema,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
18 “Sema na Aroni na wanawe, na kwa watu wa Israeli wote. Waambie, Mwisraeli yeyote, au Mgeni anayeishi katika Israeli, waletapo dhabihu—iwe ni kutimiza kiapo, au iwe ni sadaka ya hiari, au wanaleta kwa Yahweh sadaka ya kuteketezwa kwa moto,
« Parle à Aaron et à ses fils, ainsi qu’à tous les enfants d’Israël; et dis-leur: Qui que ce soit de la maison d’Israël ou des étrangers en Israël qui présente son offrande, soit pour l’accomplissement d’un vœu, soit comme don volontaire, s’il l’offre à Yahweh en holocauste,
19 ikiwa wanataka ikubalike, ni lazima watowe mnyama dume asiye na dosari, kutoka kwenye kundi la ng'ombe, kondoo au mbuzi
pour que vous soyez agréés, que la victime soit un mâle sans défaut, d’entre les bœufs, les brebis ou les chèvres.
20 Lakini hamtatoa chochote kilicho na dosari. Sitakipokea kwa niaba yenu.
Vous n’en offrirez aucune qui ait un défaut, car elle ne serait pas agréée.
21 Yeyote atoae dhabihu ya sadaka ya ushirika kutoka katika kundi la ng'ombe au la kondoo kwa Yahweh ili kutimiza kiapo, au kama sadaka ya hiari, ili ikubalike, ni lazima isiwe na kilema. Ni lazima pasiweko na kasoro katika mnyama.
Quand un homme offre à Yahweh du gros ou du menu bétail en sacrifice pacifique, soit pour s’acquitter d’un vœu, soit comme offrande volontaire, la victime, pour être agréée, devra être parfaite; il n’y aura en elle aucun défaut.
22 Msitoe kabisa wanyama waliovipofu, waliojeruhiwa, wala walio na kilema, wenye upele, vidonda vitokavyo usaha, wala wenye vigaga. Msiwatoe hawa kuwa dhabihu ya kuteketezwa kwa moto iliyotolewa kwa Yahweh juu ya madhabahu.
Un animal aveugle, estropié ou mutilé, ayant un ulcère, la gale ou une dartre, vous ne l’offrirez pas à Yahweh; vous n’en ferez point sur l’autel un sacrifice par le feu à Yahweh.
23 Unaweza kumleta makisai au mwana-kondoo mlemavu au aliyedumaa kuwa sadaka ya hiari, lakini sadaka kama hiyo kwa ajili kutimiza kiapo, haitapokelewa.
Tu pourras immoler comme offrande volontaire un bœuf ou une brebis ayant un membre trop long ou trop court; mais, pour l’accomplissement d’un vœu, cette victime ne serait pas agréée.
24 Usitoe kwa Yahweh mnyama yeyote aliyetiwa jeraha, kupondwa, au kukatwa korodani zake.
Vous n’offrirez point à Yahweh un animal qui ait les testicules froissés, écrasés, arrachés ou coupés; vous ne ferez pas cela dans votre pays.
25 Usifanye haya katika nchi yako. Usilete mkate wa Mungu wako kutoka mkononi mwa mgeni. Hao wanyama wenye vilema na dosari ndani yao, hawatapokelewa kabisa kwa ajili yako.
Même de la main d’un étranger, vous n’accepterez aucune de ces victimes pour l’offrir comme aliment de votre Dieu; car elles sont corrompues, il y a en elles un défaut: elles ne seraient pas agréées pour vous. »
26 Yahweh akamwambia Musa na akasema,
Yahweh dit à Moïse:
27 “Wakati ndama, mwana—kondo au mwana—mbuzi azaliwapo, sharti abaki na mama yake kwa muda wa siku saba. Ndipo kuanzia siku ya nane na kuendelea, anaweza kupokelewa kuwa dhabihu iliyofanywa kwa moto kwa Yahweh.
« Un bœuf, un agneau ou une chèvre, quand il naîtra, restera sept jours sous sa mère; à partir du huitième jour et les jours suivants, il sera agréé pour être offert en sacrifice fait par le feu à Yahweh.
28 Usimchinje ng'ombe jike pamoja na ndama wake au mbuzi jike pamoja na kitoto chake kwa siku moja.
Bœuf ou agneau, vous n’immolerez pas l’animal et son petit le même jour.
29 Utoapo sadaka ya shukrani kwa Yahweh utaitoa kwa njia iliyokubalika.
Quand vous offrirez à Yahweh un sacrifice d’actions de grâces, vous l’offrirez de manière qu’il soit agréé;
30 Ni lazima iliwe siku iyo hiyo inayotolewa. Hutakiwi kubakiza chochote hata asubuhi. Mimi ndimi Yahweh.
pour cela, la victime sera mangée le même jour; vous n’en laisserez rien jusqu’au matin. Je suis Yahweh.
31 Kwa hiyo imewapasa kuzishika amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Yahweh.
Vous observerez mes commandements et les mettrez en pratique: je suis Yahweh.
32 Msiliabishe jina langu takatifu. Ni lazima nitambuliwe kuwa ni mtakatifu na watu wa Israeli. Mimi ndimi Yahweh niwafanyaye ninyi watakatifu,
Vous ne profanerez pas mon saint nom, et je serai sanctifié au milieu des enfants d’Israël. Je suis Yahweh, qui vous sanctifie,
33 ambaye amewaleta kutoka katika nchi ya Misri ili niwe Mungu wenu: Mimi ndimi Yahweh.”
celui qui vous a fait sortir du pays d’Égypte, pour être votre Dieu. Je suis Yahweh. »

< Mambo ya Walawi 22 >