< Kutoka 38 >

1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
И сделал жертвенник всесожжения из дерева ситтим длиною в пять локтей и шириною в пять локтей, четырехугольный, вышиною в три локтя;
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
и сделал роги на четырех углах его, так что из него выходили роги, и обложил его медью.
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
И сделал все принадлежности жертвенника: горшки, лопатки, чаши, вилки и угольницы; все принадлежности его сделал из меди.
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
И сделал для жертвенника решетку, род сетки, из меди, по окраине его внизу до половины его;
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
и сделал четыре кольца на четырех углах медной решетки для вкладывания шестов.
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
И сделал шесты из дерева ситтим, и обложил их медью,
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
и вложил шесты в кольца на боках жертвенника, чтобы носить его посредством их; пустой внутри из досок сделал его.
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
И сделал умывальник из меди и подножие его из меди с изящными изображениями, украшающими вход скинии собрания.
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
И сделал двор: с полуденной стороны, к югу, завесы из крученого виссона, длиною во сто локтей;
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
столбов для них двадцать и подножий к ним двадцать медных; крючки у столбов и связи их из серебра.
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
И по северной стороне - завесы во сто локтей; столбов для них двадцать и подножий к ним двадцать медных; крючки у столбов и связи их из серебра.
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
И с западной стороны - завесы в пятьдесят локтей, столбов для них десять и подножий к ним десять; крючки у столбов и связи их из серебра.
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
И с передней стороны к востоку - завесы в пятьдесят локтей.
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
Для одной стороны ворот двора - завесы в пятнадцать локтей, столбов для них три и подножий к ним три;
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
и для другой стороны по обеим сторонам ворот двора - завесы в пятнадцать локтей, столбов для них три и подножий к ним три.
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
Все завесы во все стороны двора из крученого виссона,
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
а подножия у столбов из меди, крючки у столбов и связи их из серебра; верхи же у них обложены серебром, и все столбы двора соединены связями серебряными.
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
Завеса же для ворот двора узорчатой работы из голубой, пурпуровой и червленой шерсти и из крученого виссона, длиною в двадцать локтей, вышиною в пять локтей, по всему протяжению, подобно завесам двора;
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
и столбов для нее четыре, и подножий к ним четыре медных; крючки у них серебряные, а верхи их обложены серебром, и связи их серебряные.
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
Все колья вокруг скинии и двора медные.
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
Вот исчисление того, что употреблено для скинии откровения, сделанное по повелению Моисея, посредством левитов под надзором Ифамара, сына Ааронова, священника.
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
Делал же все, что повелел Господь Моисею, Веселеил, сын Урии, сына Ора, из колена Иудина,
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
и с ним Аголиав, сын Ахисамахов, из колена Данова, резчик и искусный ткач и вышиватель по голубой, пурпуровой, червленой и виссонной ткани.
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Всего золота, употребленного в дело на все принадлежности святилища, золота, принесенного в дар, было двадцать девять талантов и семьсот тридцать сиклей, сиклей священных;
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
серебра же от исчисленных лиц общества сто талантов и тысяча семьсот семьдесят пять сиклей, сиклей священных;
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
с шестисот трех тысяч пятисот пятидесяти человек, с каждого поступившего в исчисление, от двадцати лет и выше, по полсиклю с человека, считая на сикль священный.
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
Сто талантов серебра употреблено на вылитие подножий святилища и подножий у завесы; сто подножий из ста талантов, по таланту на подножие;
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
а из тысячи семисот семидесяти пяти сиклей сделал он крючки у столбов и покрыл верхи их и сделал связи для них.
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
Меди же, принесенной в дар, было семьдесят талантов и две тысячи четыреста сиклей;
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
из нее сделал он подножия для столбов у входа в скинию свидетельства, и жертвенник медный, и решетку медную для него, и все сосуды жертвенника,
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
и подножия для столбов всего двора, и подножия для столбов ворот двора, и все колья скинии и все колья вокруг двора.

< Kutoka 38 >