< Kutoka 38 >

1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
[Several men helped] Bezalel to make the altar for burning sacrifices. They made it from acacia wood. It was square, (7-1/2 feet/2.2 meters) on each side, and it was (4-1/2 feet/1.3 meters) high.
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
They made [a projection that looked like] a horn on each of the top corners. The projections were carved from the same block of wood that the altar [was made of]. They covered the whole altar with bronze.
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
They made the pans in which to put the greasy ashes [from the animal sacrifices]. They also made the shovels for cleaning out the ashes. They made the basins and forks for turning the meat as it cooked, and buckets for carrying hot coals/ashes. All of those things were made from bronze.
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
They also made a bronze grating to hold the wood and burning coals. They put the grating under the rim that went around the altar. [They] made it so that it was [inside the altar], halfway down.
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
They made bronze rings in which to put the poles [for carrying the altar], and fastened one of them to each of the corners of the altar.
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
They made the poles from acacia wood and covered them with bronze.
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
They put the poles through the rings on each side of the altar. The poles were for carrying the altar.
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
The altar was [hollow] like an empty box. It was made from boards [of acacia wood]. They made/cast the washbasin and its base from bronze. The bronze was from the mirrors that belonged to the women who worked at the entrance of the Sacred Tent.
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
[Around the Sacred Tent] Bezalel and his helpers made a courtyard. To form the courtyard, they made curtains of fine white linen. On the south side, the curtain was (150 feet/46 meters) long.
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
[To hang the curtain], they made 20 bronze posts and 20 bronze bases, [one for under each post]. [To fasten the curtains to] the posts, they made silver hooks, and [they made metal] rods [covered with] silver.
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
They made the same kind of curtains, posts, bases, and hooks for the north side of the courtyard.
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
On the west side [of the courtyard], they made a curtain (75 feet/23 meters) long. They also made ten posts on which to hang the curtains, and ten bases, with silver hooks and [metal] rods [covered with] silver.
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
On the east side, [where the entrance is], the courtyard was (75 feet/23 meters) wide.
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
On each side of the entrance, they made a curtain (22-1/2 feet/6.6 meters) wide. On each side they [were hung from] three posts, and one base was under each post.
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
All the curtains around the courtyard were made from fine white linen.
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
All the posts around the courtyard were made of bronze, but the tops were covered with silver. The posts were connected with [metal] rods [covered with] silver. The clasps/fasteners and hooks were made of silver.
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
For the entrance of the courtyard, they made a curtain from fine white linen, and a skilled weaver embroidered it with blue, purple, and red yarn/thread. The curtain was (30 feet/9 meters) long and (7-1/2 feet/2.3 meters) high, just like the other curtains around the courtyard.
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
All the curtains were made of fine white linen. They were supported by four posts, and [under each post] was a base made of bronze. All the posts around the courtyard were connected with [metal] rods [covered with] silver. The clasps/fasteners were made of silver, and the tops of the posts were covered with silver.
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
All the tent pegs to support the Sacred Tent and the curtains around the courtyard were made of bronze.
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
Here is a list of the amounts of metal used to make the Sacred Tent. Moses/I told [some men from] the tribe of Levi to [count all the materials used and] write down the amounts. Ithamar, the son of Aaron the priest, supervised those men.
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
Bezalel the son of Uri and grandson of Hur made all the things that Yahweh commanded Moses/me to be made.
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
Bezalel’s helper was Oholiab, the son of Ahisamach, of the tribe of Dan. Oholiab was a skilled engraver who made artistic things. He made fine white linen, and he embroidered designs using blue, purple, and red yarn/thread. He also made other cloth.
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
All the gold that was used to make the Sacred Tent weighed (2,195 pounds/1,000 kg.). They used the official standard when they weighed the gold.
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
All the silver that the people contributed when the leaders (took the census/counted the men) weighed (7,500 pounds/3,400 kg.). They also used the official standard when they weighed the silver.
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
All the men who were at least 20 years old were counted, and they each paid the required amount. That was a total of 603,550 men.
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
They used (75 pounds/34 kg.) of silver for making/casting each of the 100 bases to [put under the posts to support] the curtains of the Sacred Tent.
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
Bezalel [and his helpers] used the (50 pounds/30 kg.) of silver that was not used for the bases to make the rods and the hooks for the posts, and to cover the tops of the posts.
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
The bronze that the people contributed weighed (5,310 pounds/2,425 kg.).
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
With the bronze, Bezalel and his helpers made the bases for under the posts at the entrance of the Sacred Tent. They also made the altar for burning sacrifices, the grating for it and the tools used with it,
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
the bases for the posts [that supported the curtains] that surrounded the courtyard and the bases for the entrance to the courtyard, and the pegs for the Sacred Tent and for [the curtains around] the courtyard.

< Kutoka 38 >