< Kutoka 38 >

1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
and to make [obj] altar [the] burnt offering tree: wood acacia five cubit length his and five cubit width his to square and three cubit height his
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
and to make horn his upon four corner his from him to be horn his and to overlay [obj] him bronze
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
and to make [obj] all article/utensil [the] altar [obj] [the] pot and [obj] [the] shovel and [obj] [the] bowl [obj] [the] fork and [obj] [the] censer all article/utensil his to make bronze
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
and to make to/for altar grate deed: work net bronze underneath: under ledge his from to/for beneath till half his
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
and to pour: cast metal four ring in/on/with four [the] end to/for grate [the] bronze house: container to/for alone: pole
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
and to make [obj] [the] alone: pole tree: wood acacia and to overlay [obj] them bronze
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
and to come (in): bring [obj] [the] alone: pole in/on/with ring upon side [the] altar to/for to lift: bear [obj] him in/on/with them be hollow tablet to make [obj] him
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
and to make [obj] [the] basin bronze and [obj] stand his bronze in/on/with mirror [the] to serve which to serve entrance tent meeting
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
and to make [obj] [the] court to/for side south south [to] curtain [the] court linen to twist hundred in/on/with cubit
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
pillar their twenty and socket their twenty bronze hook [the] pillar and ring their silver: money
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
and to/for side north hundred in/on/with cubit pillar their twenty and socket their twenty bronze hook [the] pillar and ring their silver: money
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
and to/for side sea: west curtain fifty in/on/with cubit pillar their ten and socket their ten hook [the] pillar and ring their silver: money
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
and to/for side east [to] east [to] fifty cubit
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
curtain five ten cubit to(wards) [the] shoulder pillar their three and socket their three
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
and to/for shoulder [the] second from this and from this to/for gate [the] court curtain five ten cubit pillar their three and socket their three
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
all curtain [the] court around linen to twist
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
and [the] socket to/for pillar bronze hook [the] pillar and ring their silver: money and plating head: top their silver: money and they(masc.) to connect silver: money all pillar [the] court
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
and covering gate [the] court deed: work to weave blue and purple and worm scarlet and linen to twist and twenty cubit length and height in/on/with width five cubit to/for close curtain [the] court
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
and pillar their four and socket their four bronze hook their silver: money and plating head: top their and ring their silver: money
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
and all [the] peg to/for tabernacle and to/for court around bronze
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
these reckoning [the] tabernacle tabernacle [the] testimony which to reckon: list upon lip: word Moses service: work [the] Levi in/on/with hand: power Ithamar son: child Aaron [the] priest
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
and Bezalel son: child Uri son: child Hur to/for tribe Judah to make [obj] all which to command LORD [obj] Moses
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
and with him Oholiab son: child Ahisamach to/for tribe Dan artificer and to devise: design and to weave in/on/with blue and in/on/with purple and in/on/with worm [the] scarlet and in/on/with linen
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
all [the] gold [the] to make: do to/for work in/on/with all work [the] holiness and to be gold [the] wave offering nine and twenty talent and seven hundred and thirty shekel in/on/with shekel [the] holiness
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
and silver: money to reckon: list [the] congregation hundred talent and thousand and seven hundred and five and seventy shekel in/on/with shekel [the] holiness
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
bekah to/for head half [the] shekel in/on/with shekel [the] holiness to/for all [the] to pass upon [the] to reckon: list from son: aged twenty year and above [to] to/for six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
and to be hundred talent [the] silver: money to/for to pour: cast metal [obj] socket [the] holiness and [obj] socket [the] curtain hundred socket to/for hundred [the] talent talent to/for socket
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
and [obj] [the] thousand and seven [the] hundred and five and seventy to make hook to/for pillar and to overlay head: top their and to connect [obj] them
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
and bronze [the] wave offering seventy talent and thousand and four hundred shekel
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
and to make in/on/with her [obj] socket entrance tent meeting and [obj] altar [the] bronze and [obj] grate [the] bronze which to/for him and [obj] all article/utensil [the] altar
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
and [obj] socket [the] court around and [obj] socket gate [the] court and [obj] all peg [the] tabernacle and [obj] all peg [the] court around

< Kutoka 38 >