< Kutoka 38 >
1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
And he made [the] altar of the burnt offering wood of acacia [was] five cubits length its and [was] five cubits breadth its square and [was] three cubits height its.
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
And he made horns its on [the] four corners its from it they were horns its and he overlaid it bronze.
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
And he made all [the] articles of the altar the pots and the shovels and the bowls the forks and the fire-pans all articles its he made bronze.
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
And he made for the altar a grating a work of a net of bronze under ledge its from to downwards to middle its.
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
And he cast four rings on [the] four the ends for [the] grating of bronze holders for the poles.
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
And he made the poles wood of acacia and he overlaid them bronze.
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
And he put the poles in the rings on [the] sides of the altar to carry it by them hollow of boards he made it.
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
And he made the laver bronze and base its bronze with [the] mirrors of the serving [women] who they served [the] entrance of [the] tent of meeting.
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
And he made the courtyard for [the] side of - [the] south south-ward [the] curtains of the courtyard [were] fine linen twisted one hundred by the cubit.
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
Pillars their twenty and bases their twenty [were] bronze [the] hooks of the pillars and bands their [were] silver.
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
And for [the] side of [the] north one hundred by the cubit pillars their twenty and bases their twenty [were] bronze [the] hooks of the pillars and bands their [were] silver.
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
And for [the] side of [the] west curtains fifty by the cubit pillars their ten and bases their ten [the] hooks of the pillars and bands their [were] silver.
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
And for [the] side of east-ward east-ward fifty cubit[s].
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
Curtains fif-teen cubit[s] to the side pillars their three and bases their three.
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
And for the side second from this and from this to [the] gate of the courtyard curtains [were] fif-teen cubit[s] pillars their three and bases their three.
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
All [the] curtains of the courtyard all around [were] fine linen twisted.
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
And the bases for the pillars [were] bronze [the] hooks of the pillars and bands their [were] silver and [the] overlay of tops their [was] silver and they [were] furnished with bands silver all [the] pillars of the courtyard.
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
And [the] screen of [the] gate of the courtyard [was] [the] work of a worker in colors violet stuff and purple and scarlet stuff of scarlet and fine linen twisted and [was] twenty cubit[s] [the] length and [the] height in breadth [was] five cubits corresponding to [the] curtains of the courtyard.
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
And pillars their four and bases their four [were] bronze hooks their [were] silver and [the] overlay of tops their and bands their [were] silver.
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
And all the tent pegs for the tabernacle and for the courtyard all around [were] bronze.
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
These [were] [the] expenses of the tabernacle [the] tabernacle of the testimony which it was recorded on [the] mouth of Moses [the] service of the Levites by [the] hand of Ithamar [the] son of Aaron the priest.
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
And Bezalel [the] son of Uri [the] son of Hur of [the] tribe of Judah he made all that he had commanded Yahweh Moses.
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
And [was] with him Oholiab [the] son of Ahisamach of [the] tribe of Dan an engraver and a skillful worker and a worker in colors in the violet stuff and in the purple and in [the] scarlet stuff of the scarlet and in the fine linen.
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
All the gold that was used for the work in all [the] work of the holy place and it was - [the] gold of the wave-offering nine and twenty talent[s] and seven hundred and thirty shekel[s] by [the] shekel of the holy place.
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
And [the] silver of [those who] were enrolled of the congregation [was] one hundred talent[s] and one thousand and seven hundred and five and seventy shekel[s] by [the] shekel of the holy place.
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
A beka for the head [the] half of the shekel by [the] shekel of the holy place for every [one who] passed over to those [who] were enrolled from a son of twenty year[s] and up-wards to six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
And it was [the] one hundred [the] talent[s] of silver to cast [the] bases of the holy place and [the] bases of the curtain a hundred bases for [the] one hundred the talent[s] a talent for base.
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
And the one thousand and [the] seven the hundred and five and seventy he made hooks for the pillars and he overlaid tops their and he furnished with bands them.
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
And [the] bronze of the wave-offering [was] seventy talent[s] and two thousand and four hundred shekel[s].
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
And he made with it [the] bases of [the] entrance of [the] tent of meeting and [the] altar of bronze and [the] grating of bronze which [belonged] to it and all [the] articles of the altar.
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
And [the] bases of the courtyard all around and [the] bases of [the] gate of the courtyard and all [the] tent pegs of the tabernacle and all [the] tent pegs of the courtyard all around.