< Kutoka 38 >

1 Naye akafanya madhabahu ya toleo la kuteketezwa kwa mbao za mshita. Mikono mitano urefu wake, na mikono mitano upana wake, ilikuwa mraba, na mikono mitatu kimo chake.
Derpaa lavede han Brændofferalteret af Akacietræ, fem Alen langt og fem Alen bredt, firkantet, og tre Alen højt.
2 Halafu akafanya pembe zake kwenye zile ncha zake nne. Pembe zake zilitoka kwake. Kisha akaifunika kwa shaba.
Han lavede Horn til dets fire Hjørner, saaledes at de var i eet dermed, overtrak det med Kobber
3 Baada ya hilo akavifanya vyombo vyote vya madhabahu, yale makopo na zile sepetu na yale mabakuli, zile nyuma na vile vyetezo. Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba.
og lavede alt Alterets Tilbehør, Karrene, Skovlene, Skaalene, Gaflerne og Panderne; alt dets Tilbehør lavede han af Kobber.
4 Tena akaifanyia madhabahu kiunzi cha fito, mtandao wa shaba, chini ya ukingo wake, chini kuelekea katikati yake.
Derpaa omgav han Alteret med et flettet Kobbergitter neden under dets Liste, saaledes at det naaede op til Alterets halve Højde.
5 Halafu akatengeneza pete nne kwenye ile miisho minne karibu na kile kiunzi cha shaba, ili kuitegemeza ile miti.
Derefter støbte han fire Ringe til Kobbergitterets fire Hjørner til at stikke Bærestængerne i.
6 Bezaleli akafanya miti ya mshita na kuifunika kwa shaba.
Bærestængerne lavede han at Akacietræ og overtrak dem med Kobber.
7 Kisha akaitia ile miti kwenye zile pete zilizo pande za madhabahu ili kuibeba. Akaifanya kuwa sanduku la mbao lenye uwazi.
Og Stængerne stak han gennem Ringene paa Alterets Sider, for at det kunde bæres med dem. Han lavede det hult af Brædder.
8 Kisha akafanya beseni ya shaba na kinara chake cha shaba. Kwa kutumia vioo vya watumishi wanawake ambao walifanya utumishi uliopangwa kwenye mwingilio wa hema la mkutano.
Derpaa lavede han Vandkummen med Fodstykke af Kobber og brugte dertil Spejle, som tilhørte Kvinderne, der gjorde Tjeneste ved Indgangen til Aabenbaringsteltet.
9 Naye akafanya ule ua. Upande unaokabili Negebu, kuelekea kusini, mapazia ya ua yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa, kwa mikono mia moja.
Derpaa indrettede han Forgaarden: Til Sydsiden det hundrede Alen lange Forgaardsomhæng af tvundet Byssus
10 Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha
med tyve Piller og tyve Fodstykker af Kobber og med Knager og Baand af Sølv til Pillerne.
11 Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini kulikuwa na mikono mia. Nguzo zake ishirini na vikalio vyake ishirini vilikuwa vya shaba. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
Til Nordsiden hundrede Alen med tyve Piller og tyve Fodstykker af Kobber og med Knager og Baand af Sølv til Pillerne.
12 Lakini kwa ajili ya upande wa magharibi mapazia yalikuwa mikono hamsini. Nguzo zake zilikuwa kumi na vikalio vyake kumi. Misumari ya nguzo na viungo vyake vilikuwa vya fedha.
Til Vestsiden det halvtredsindstyve Alen lange Omhæng med ti Piller og ti Fodstykker og med Knager og Baand af Sølv til Pillerne.
13 Na kwa ajili ya upande wa mashariki kulikuwa na mikono hamsini.
Og til Forsiden mod Øst, der var halvtredsindstyve Alen bred,
14 Mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano kwa upande mmoja. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
det femten Alen lange Omhæng med fire Piller og tre Fodstykker til den ene Side af Indgangen,
15 Na kwa ajili ya upande ule mwingine, huu na ule, wa lango la ua, mapazia yalikuwa mikono kumi na mitano. Nguzo zake zilikuwa tatu na vikalio vyake vitatu.
og det femten Alen lange Omhæng med tre Piller og tre Fodstykker til den anden Side af Indgangen.
16 Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani bora kilichosokotwa.
Alle Omhæng rundt om Forgaarden var af tvundet Byssus,
17 Navyo vikalio vya nguzo vilikuwa vya shaba. Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha navyo vilifunikwa kwa shaba sehemu ya juu, na kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua.
Fodstykkerne til Pillerne af Kobber, men deres Knager og Baand af Sølv; alle Pillernes Hoveder var overtrukket med Sølv; og de havde Baand af Sølv.
18 Nacho kisitiri cha lango la ua kilikuwa na mikono ishirini urefu. Cha uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, na urefu wake ulikuwa mikono ishirini, nacho kimo kotekote kilikuwa mikono mitano sawasawa na mapazia ya ua.
Forhænget til Forgaardens Indgang var af violet og rødt Purpurgarn i broget Vævning, karmoisinrødt Garn og tvundet Byssus, tyve Alen langt og fem Alen højt, svarende til Bredden paa Forgaardens Omhæng.
19 Na nguzo zake nne na vikalio vyake vinne vilikuwa vya shaba. Misumari yake ilikuwa ya fedha na utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha.
Dertil hørte fire Piller med fire Fodstykker af Kobber; Knagerne var af Sølv og Overtrækket paa Hovederne og Baandene ligeledes af Sølv.
20 Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba
Alle Pælene til Boligen og Forgaarden rundt om var af Kobber.
21 Hivi ndivyo vitu vilivyohesabiwa vya maskani, maskani ya Ushuhuda, vilivyohesabiwa kwa amri ya Musa, kuwa utumishi wa Walawi chini ya uongozi wa Ithamari mwana wa Aruni kuhani.
Her følger Regnskabet over Boligen, Vidnesbyrdets Bolig, som paa Moses's Bud blev opgjort af Leviterne under Ledelse af Itamar, en Søn af Præsten Aron;
22 Naye Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda alifanya yote ambayo Yahweh alikuwa amemwamuru Musa.
Bezal'el, en Søn af Hurs Søn Uri, af Judas Stamme havde udført alt, hvad HERREN havde paalagt Moses,
23 Na pamoja naye alikuwa Oholiabu mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani, fundi na mtarizi na mfumaji wa uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora.
sammen med Oholiab, Ahisamaks Søn, af Dans Stamme, som udførte Udskæringsarbejdet, Kunstvævningen og den brogede Vævning af violet og rødt Purpur, Karmoisin og Byssus.
24 Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi katika kazi yote ya mahali patakatifu ikawa jumla ya dhahabu ya toleo la kutikisa, talanta ishirini na tisa na shekeli 730 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
Hvad angaar Guldet, der anvendtes til Arbejdet, under hele Arbejdet paa Helligdommen, saa løb det som Gave viede Guld op til 29 Talenter og 730 Sekel efter hellig Vægt.
25 Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko ilikuwa talanta mia moja na shekeli 1, 775 kulingana na shekeli ya mahali patakatifu,
Det ved Menighedens Mønstring indkomne Sølv løb op til 100 Talenter og 1775 Sekel efter hellig Vægt:
26 ile nusu shekeli kwa ajili ya mtu mmoja ilikuwa nusu shekeli kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, Kwa kila mtu aliyekuwa akipita kuingia upande wa wale waliokuwa wameandikishwa kuanzia miaka ishirini na zaidi, jumla ya watu 603, 550.
en, Beka, det halve af en Sekel efter hellig Vægt, af enhver, der maatte lade sig mønstre, altsaa fra Tyveaarsalderen og opefter, i alt 603 550 Mand:
27 Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza vikalio vya mahali patakatifu na vikalio vya lile pazia. Vikalio mia moja vilitoshana na talanta mia moja, talanta moja kwa kikalio kimoja.
De 100 Talenter Sølv medgik til Støbningen af Helligdommens og Forhængets Fodstykker, 100 Talenter til 100 Fodstykker, en Talent til hvert Fodstykke.
28 Na kutokana na zile shekeli 1, 775 alifanyiza vibanio vya nguzo na kuvifunika sehemu yake ya juu na kuviunganisha pamoja.
Men de 1775 Sekel anvendte han til Knager til Pillerne, til at overtrække deres Hoveder med og til Baand paa dem.
29 Nayo shaba ya toleo la kutikisa ilikuwa talanta sabini na shekeli 2, 400.
Det som Gave viede Kobber udgjorde 70 Talenter og 2400 Sekel.
30 Naye akaitumia kufanya vile vikalio vya mwingilio wa hema la mkutano na ile madhabahu ya shaba na kile kiunzi chake cha shaba, na vyombo vyote vya madhabahu,
Deraf lavede han Fodstykkerne til Aabenbaringsteltets Indgang, Kobberalteret med dets Kobbergitter og alt Alterets Tilbehør,
31 na vile vikalio vya ua kuzunguka pande zote, na vile vikalio vya lango la ua, na misumari yote ya maskani na misumari yote ya ua kuzunguka pande zote.
Fodstykkerne til Forgaarden rundt om og til Forgaardens Indgang og alle Teltpælene til Boligen og alle Teltpælene til Forgaarden hele Vejen rundt.

< Kutoka 38 >