< Waefeso 3 >
1 Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
For this reason I, Paul, the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles—
2 Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
surely you have heard of the dispensation of the grace of God that was given to me for you,
3 Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
how that by revelation He made known to me the ‘secret’ (as I have written briefly already,
4 Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
with reference to which, when you read, you can understand my insight into Christ's secret),
5 Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
which in different generations was not made known to the sons of men, as it has now been revealed by Spirit to His holy apostles and prophets:
6 Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
that the Gentiles are joint-heirs, of the same body, and fellow partakers of His promise in the Christ through the Gospel,
7 Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
of which I became a servant according to the gift of God's grace, the gift given to me according to the outworking of His power.
8 Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
To me, the very least of all saints, was this grace given, to preach among the Gentiles the unsearchable riches of Christ,
9 inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn )
and to enlighten all as to the program of the secret that from the beginning of the ages has been hidden by the God who created all things through Jesus Christ; (aiōn )
10 Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
to the intent that now, through the Church, the manifold wisdom of God might be made known to the rulers and the authorities in the heavenly realms,
11 Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
according to the eternal purpose that He accomplished by Christ Jesus our Lord, (aiōn )
12 Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
in whom we have the boldness and the access with confidence through faith in Him.
13 Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
Therefore I ask that you not lose heart at my afflictions on your behalf, which is your glory.
14 Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
For this reason I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
15 ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
from whom every family in heaven and on earth receives its name,
16 Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
that He[F] may grant you, according to the riches of His glory: 1) to be strengthened with power by His Spirit in the inner man;
17 Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
2) Christ to dwell in your hearts through the Faith, having been rooted and established in love
18 Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
so that you may be fully able to grasp (with all saints) what is the breadth and length and depth and height;
19 Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
and 3) to know the love of Christ that surpasses knowledge—so that you may be fulfilled into all the fullness of God.
20 Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
Now to Him who is able to do immeasurably more than all we ask or imagine, according to the power that is working in us,
21 kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn )
to Him be the glory in the Church in Christ Jesus, to all generations, forever and ever. Amen. (aiōn )