< Wagalatia 1 >

1 Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Paul, an apostle—not from men nor through a man, but through Jesus Christ and God the Father, who raised Him from the dead—
2 Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
and all the brothers with me, to the congregations in Galatia:
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
Grace to you and peace from God the Father and our Lord Jesus Christ,
4 aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
who gave Himself for our sins, so that He might deliver us out of this present malignant age, according to the will of our God and Father, (aiōn g165)
5 Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
to whom be the glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
6 Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
I am sadly surprised that you are turning away so quickly from the one who called you by the grace of Christ, to a different gospel
7 Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
—it is not a mere variation, but certain people are unsettling you and wanting to distort the Gospel of the Christ.
8 Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
Now even if we, or an angel out of heaven, should preach any other gospel to you than what we have preached to you, let him be accursed!
9 Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
As we have just said, I here emphatically repeat: If anyone preaches any other gospel to you than what you have received, let him be accursed!
10 Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
Am I just now appealing to men, or to God? Or am I trying to please men? You see, if I were still pleasing men I would not be a slave of Christ.
11 Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
Now I want you to know, brothers, that the Gospel preached by me is not according to man;
12 Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
because I did not receive it from any man, nor was I taught it; rather it came through a revelation from Christ.
13 Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
You have heard of my former conduct while in Judaism, how I was rabid in my persecution of God's Church and tried to annihilate it;
14 Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
indeed I was advancing in Judaism beyond many Jews of my own age, being far more zealous for the traditions of my forefathers.
15 Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
But when God—who set me apart from my mother's womb and called me through His grace—resolved
16 kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
to reveal His Son in me so that I might proclaim Him among the nations/Gentiles, I did not start by consulting with flesh and blood,
17 na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
nor did I go up to Jerusalem to those who were apostles before I was; rather I went off into Arabia, and then returned to Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
Subsequently, after three years, I went up to Jerusalem to compare notes with Peter, and stayed with him fifteen days.
19 Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
(I saw none of the other apostles except James, the Lord's brother.
20 Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
Really, before God, I am not lying in what I write to you.)
21 Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
Then I went into the regions of Syria and Cilicia.
22 Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
So I remained unknown by face to the congregations of Judea (those in Christ)
23 lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
—they just kept hearing that “He who once persecuted us now proclaims the faith he formerly tried to destroy.”
24 Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.
And they glorified God about me.

< Wagalatia 1 >