< Danieli 6 >

1 Ilimpendeza Dario kuchagua juu ya ufalme magavana wa majimbo 120 ambao wangetawala juu ya ufalme wote.
It seemed good before Darius and he appointed over kingdom the satraps the one hundred and twenty who they will be over all kingdom the.
2 Juu yao kulikuwa na watawala wakuu watatu, na Daniel alikuwa mmoja wao. Hawa watawala waliwekwa ili waweze kuwasimamia magavana wa majimbo, ili kwamba mfalme asipate hasara.
And above more than them overseers three whom Daniel [was] one of them whom they will be satraps the these giving to them report the and king the not he will be suffering injury.
3 Danieli alipambanuliwa juu ya watawala wakuu na juu ya magavana wa majimbo kwasababu alikuwa na roho isiyo ya kawaida. Mfalme alikuwa akipanga kumweka juu ya ufalme wote.
Then Daniel this he was distinguishing himself over overseers the and satraps the as to because that a spirit extraordinary [was] in him and king the [was] planning to appoint him over all kingdom the.
4 Basi watawala wakuu wengine na magavana wa majimbo walitafuta makosa katika kazi ambazo Danieli alizifanya kwa ufalme, lakini hawakuweza kuona ufisadi au kushindwa katika majukumu yake kwasababu alikuwa mwaminifu. Hakuna kosa au uzembe uliopatikana ndani yake.
Then overseers the and satraps the they were seeking an occasion to find to Daniel from [the] side of kingdom the and any occasion and corruption not [they were] able to find as to because that [was] trustworthy he and any negligence and corruption not it was found concerning him.
5 Kisha watu hawa wakasema, “Hatukuweza kupata sababu yoyote ya kumshitaki huyu Danieli isipokuwa tukitafuta kitu fulani dhidi yake kuhusiana na sheria za Mungu wake.'”
Then men the these [were] saying that not we will find to Daniel this any occasion except we have found concerning him in [the] law of God his.
6 Ndipo watawala hawa na magavana walileta mpango mbele ya mfalme. Walimwambia, “Mfalme Dario, uishi milele!
Then overseers the and satraps the these they came as a crowd to king the and as follows [they were] saying to him O Darius king the for ever live!
7 Watawala wote wakuu wa ufalme, magavana wa mikoa, na magavana wa majimbo, washauri, na magavana wameshauriana kwa pamoja na kuamua kuwa wewe, mfalme, unapaswa kupitisha amri na kuitekeleza, ili kwamba mtu yeyote anayefanya dua kwa mungu yeyote au mtu kwa siku thelathini, isipokuwa wewe mfalme, mtu huyo lazima atupwe katika tundu la simba.
They took counsel together all - [the] overseers of kingdom the prefects the and satraps the counselors the and governors the to establish [the] statute of king the and to make stringent a prohibition that every [one] who he will ask a petition from any god and person until days thirty except from you king O he will be thrown to [the] den of lions the.
8 Sasa mfalme, litoe agizo na utie saini nyaraka ili kwamba isije ikabadilika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi, hivyo haiweze ikabatilishwa.
Now king O you will establish prohibition the so you may sign writing the which not to change according to [the] law of [the] Medes and [the] Persians which not it will pass away.
9 Basi, mfalme Dario alitia saini nyaraka kwa kuifanya amri kuwa sheria.
As to because this king the Darius he signed writing the and prohibition the.
10 Danieli alipojua kuwa nyaraka imekwisha kusainiwa kuwa sheria, alienda ndani ya nyumba yake (madirisha yake katika chumba cha juu yalikuwa wazi kuelekea Yerusalemu), na alipiga magoti yake, kama alivyokuwa akifanya mara tatu kwa siku, na aliomba na kushukuru mbele ya Mungu wake, kama alivyofanya hapo kabla.
And Daniel as that he knew that it was signed writing the he went in to house his and windows [were] opened to it in upper room his facing Jerusalem and times three in day the he - [was] kneeling on knees his and [was] praying and [was] praising before God his as to because that he was doing from [the] former time of this.
11 Kisha watu hawa walikuwa wameunda hila kwa pamoja walimwona Danieli akiomba na kutafuta msaada kutoka kwa Mungu.
Then men the these they came as a crowd and they found Daniel asking and imploring favor before God his.
12 Ndipo walipomwendea mfalme na kuongea naye kuhusiana na amri yake: “Je haukuweka amri kwamba mtu yeyote akayefanya maombi kwa mungu mwingine au kwa binadamu ndani ya siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, mfalme, lazima mtu huyo atupwe katika tundu la simba? Mfalme akajibu, “Jambo hili ni la hakika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi; ambazo haziwezi zikabatilishwa.”
Then they approached and [were] saying before king the concerning [the] prohibition of king the ¿ not a prohibition did you sign that every person who he will ask from any god and person until days thirty except from you king O he will be thrown to [the] den of lions the [was] replying king the and saying [is] certain word the according to [the] law of [the] Medes and [the] Persians which not it will pass away.
13 Kisha wakamjibu mfalme, “Mtu yule Daniel, ambaye ni mmoja wa watu wa mateka kutoka Yuda, hakutii wewe, mfalme wala maagizo yako uliyoyasaini. Yeye humwomba Mungu wake mara tatu kwa siku.”
Then they replied and [were] saying before king the that Daniel who [is] one of [the] sons of exile the of Judah not he has set (to you *Q(k)*) king O discretion and to prohibition the which you signed and times three in day the [he is] asking petition his.
14 Mfalme aliposikia haya, alisikitishwa sana, alitumia akili jinsi ya kumwokoa kutoka katika utawala huu. Alisumbuka sana mpaka wakati wa kuzama kwa jua akijaribu kumwokoa Danieli.
Then king the as that word the he heard exceedingly it was displeasing to him and concerning Daniel he set mind to deliver him and until [the] goings in of sun the he was striving to rescue him.
15 Kisha watu hawa waliokuwa wamepanga njama walikusanyika kwa pamoja na mfalme, na wakamwambia, “Ujue mfalme kwamba ni sheria ya Wamedi na Waajemi kwamba hakuna amri au sanamu ambayo mfalme anaipitisha yaweza kubadilishwa.”
Then men the these they came as a crowd to king the and [were] saying to king the know king O that [the] law of [the] Medes and [the] Persians that any prohibition and statute which king the he will establish not to change.
16 Ndipo mfalme alitoa agizo, na walimleta ndani Danieli, na kisha wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako, ambaye unamtumikia daima, na akuokoe.''
Then king the he said and they brought Daniel and they threw [him] to den the of lions the [was] replying king the and [was] saying to Daniel God your whom (you *Q(k)*) [are] paying reverence to him in continuance he may he deliver you.
17 Jiwe lililetwa katika mlango wa tundu, na mfalme alilitia muhuri wa pete yake mwenyewe na pamoja na muhuri wa wakuu wake ili kwamba chochote kisiweze kubadilishwa kuhusiana na Danieli.
And it was brought a stone one and it was set over [the] mouth of den the and he sealed it king the with signet-ring his and with [the] signet-rings of nobles his that not it will change anything with Daniel.
18 Basi mfalme alienda kwenye ikulu yake na usiku ule alikuwa na mfungo. Hakuna starehe yoyote iliyoletwa mbele yake, nao usingizi ulimkimbia.
Then he went king the to palace his and he passed [the] night fasting and thrusting [women] not he brought in before him and sleep his it fled on him.
19 Kisha katika mapambazuko mfalme aliamka na kwa haraka alienda kwenye tundu la simba.
Then king the at dawn he arose at daylight the and in haste to den the of lions the he went.
20 Na alipokaribia kwenye tundu, alimwita Danieli kwa sauti ya huzuni, akimwambia Danieli, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je Mungu wako ambaye anamtumkia daima ameweza kukuokoa kutoka katika simba?
And just as approached he to den the to Daniel with a voice pained he cried out [was] replying king the and [was] saying to Daniel O Daniel [the] servant of God the living God your whom (you *Q(k)*) [are] paying reverence to him in continuance ¿ was he able to deliver you from lions the.
21 Ndipo Danieli akamwambia mfalme, “Mfalme, uishi milele!
Then Daniel with king the he spoke king O for ever live!
22 Mungu wangu amemtuma mjumbe na amevifunga vinywa vya simba, na hazijaweza kunidhuru. Kwa kuwa sikuwa na hatia yoyote mbele yake na pia mbele yako, ewe mfalme, na sijakufanyia jambo lolote la kukudhuru.”
God my he sent angel his and he closed [the] mouth of lions the and not they harmed me as to because that before him innocence it was found to me and also (before you *Q(k)*) king O a hurtful act not I have done.
23 Basi mfalme alikuwa na furaha sana. Alitoa agizo kwamba wanatakiwa wamtoe Danieli nje ya tundu. Hivyo Danieli aliondolewa kutoka katika tundu. Hakuna dhara lolote lililoonekana kwake, kwa kuwa alikuwa amemtumainia Mungu wake.
Then king the exceedingly it was good to him and Daniel he said to take up from den the and he was taken up Daniel from den the and any hurt not it was found on him that he had trusted in God his.
24 Mfalme alitoa agizo, waletwe wale watu waliomshitaki Danieli na kisha akawatupa wao katika tundu la simba - wao, na watoto wao, na wake zao. Kabla hawajafika sakafuni, simba waliwararua na kuvunjavunja mifupa yao vipande vipande.
And he said king the and they brought men the these who they had eaten pieces his of Daniel and to [the] den of lions the they threw they sons their and wives their and not they reached to [the] bottom of den the until that they assaulted them lions the and all bones their they shattered.
25 Kisha mfalme Dario aliandika ujumbe kwa watu wote, mataifa na lugha ambazo ziliishi katika dunia yote: “Amani na iongezeke kwenu.
Then Darius king the he wrote to all peoples the nations the and languages the which ([were] dwelling *Q(k)*) in all earth the peace your may it increase.
26 Ninaagiza kwamba katika utawala wote wa ufalme wangu watu watetemeka na kumcha mbele ya Mungu wa Danieli, kwa kuwa ni Mungu aliye hai na huishi milele, na ufalme wake hauwezi kuharibiwa; utawala wake utakuwepo hadi mwisho.
From before me it is made a decree that - in all [the] dominion of kingdom my they will be (trembling *Q(k)*) and fearing from before God his of Daniel that he - [is] God the living and enduring for ever and kingdom his which not it will be destroyed and dominion his [is] to end the.
27 Yeye anatuhifadhi salama na kutuokoa, na anafanya ishara na maajabu mbinguni na duniani; amemhifadhi Danieli salama dhidi ya uwezo wa simba.”
[he is] delivering And [he is] rescuing and [he is] doing signs and wonders in heavens the and on earth the who he has delivered Daniel from [the] hand of lions the.
28 Na hivyo basi, Danieli alifanikiwa katika utawala wa Dario na katika utawala wa Koreshi Mwajemi.
And Daniel this he prospered in [the] reign of Darius and in [the] reign of Cyrus (Persian the. *Q(k)*)

< Danieli 6 >