< Ezekieli 20 >

1 Ikawa ikaja katika mwaka wa saba, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wa Israeli wakaja kumuuliza Yahwe na kuketi mbele yangu.
And it was - in the year seventh in the fifth [month] on the ten of the month they came men from [the] elders of Israel to consult Yahweh and they sat down before me.
2 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
3 “mwanadamu, tangaza kwa wazee wa Israeli na uwaambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Mmekuja kuniuliza swali? Kama niishivyo, sitaulizwa swali na ninyi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
O son of humankind speak with [the] elders of Israel and you will say to them thus he says [the] Lord Yahweh ¿ to consult me [are] you coming [by] [the] life of me if I will let myself be consulted by you [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
4 Je! Utawahukumu? Utamuhukumu, mwanadamu? Wajulishe kuhusu machukizo ya baba zao.
¿ Will you judge them ¿ will you judge O son of humankind [the] abominations of ancestors their make known to them.
5 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyoichagua Israeli na kuinua mkono wangu kuapa kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo, na kufanya kujulikana mimi mwenyewe kwao katika nchi ya Misri, wakati nilipoinua mkono wangu kuapa kiapo kwao. Nalisema, “Mimi ni Yahwe Mungu wenu”-
And you will say to them thus he says [the] Lord Yahweh on [the] day chose I Israel and I lifted up hand my to [the] offspring of [the] house of Jacob and I made myself known to them in [the] land of Egypt and I lifted up hand my to them saying I [am] Yahweh God your.
6 siku hiyo niliinua mkono wangu kuapa kiapo kwa ajili yao kwamba nitawatoa kutoka nchi ya Misri kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimeichagua kwa umakini kwa ajili yao. Ilikuwa ikitiririka maziwa na asali; ilikuwa nzuri sana utukufu miongoni mwa nchi mbali mbali.
On the day that I lifted up hand my to them to bring out them from [the] land of Egypt to a land which I had selected for them flowing of milk and honey [is] beauty it to all the lands.
7 Nikawaambia, “Kila mtu atupilie mabli mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake na sanamu za Misri. Msijitie unajisi; mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
And I said to them everyone [the] detestable things of eyes his throw away and by [the] idols of Egypt may not you make yourselves unclean I [am] Yahweh God your.
8 Lakini wameasi juu yangu hawakuwa tayari kunisikiliza. Kila mtu hakutupilia mbali mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake wala kwa ajili ya sanamu za Misri, hivyo nikaona nimwage ghadhabu yangu juu yao kukamilisha hasira yangu miongoni mwao katikati ya nchi ya Misri.
And they rebelled against me and not they were willing to listen to me anyone [the] detestable things of eyes their not they threw away and [the] idols of Egypt not they forsook and I said to pour out rage my on them to complete anger my on them in [the] midst of [the] land of Egypt.
9 Nilifanya kwa ajili ya jina langu ili lisinajisiwe katika macho ya mataifa ambao walikaa pamoja nao. Nilijifanya mwenyewe kujulikana kwao, katika macho yao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.
And I acted for [the] sake of name my to not to be profaned to [the] eyes of the nations which they [were] in midst of them which I had made myself known to them to eyes their by bringing out them from [the] land of Egypt.
10 Basi nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta kwenye jangwa.
And I brought out them from [the] land of Egypt and I brought them into the wilderness.
11 Kisha nikawapa amri zangu na kufanya maagizo yangu kujulikana kwao, kwa kila mwanadamu atakayezishika ataishi.
And I gave to them statutes my and judgments my I made known to them which he will do them the person and he will live by them.
12 Pia nikawapatia Sabato zangu kama ishara kati yangu na wao, ili wajue kwamba mimi ni Yahwe niwafanyao wawe watakatifu.
And also sabbaths my I gave to them to become a sign between me and between them to know that I [am] Yahweh [who] sanctified them.
13 Lakini nyumba ya Israeli imeasi dhidi yangu jangwani. Hawakuenenda katika amri zangu; badala yake, wameyakataa maagizo yangu, ambayo mwanadamu ataishi kama akiyatii. Wamezinajisi Sabato zangu sana, basi nikasema nitamwaga hasira yangu juu yao jangwani ili kuwamalliza.
And they rebelled against me [the] house of Israel in the wilderness in statutes my not they walked and judgments my they rejected which he will do them the person and he will live by them and sabbaths my they profaned exceedingly and I said to pour out rage my on them in the wilderness to make an end of them.
14 Lakini nilifanya kwa ajili ya jina langu hivyo lisinajisiwe katika macho ya mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao kutoka Misri.
And I acted for [the] sake of name my to not to be profaned to [the] eyes of the nations which I had brought out them to eyes their.
15 Basi mimi mwenyewe pia nimeinua mkono wangu kuapa kiapo kwao jangwani sitawarudisha kwenye nchi ile niliyokuwa naenda kuwapatia, nchi inayotiririkayo maziwa na asali, ambayo ilikuwa nzuri sana ambayo ni nzuri kati ya nchi zote.
And also I I lifted up hand my to them in the wilderness to not to bring them into the land which I had given flowing of milk and honey [is] beauty it to all the lands.
16 Nimeapa hivi kwa sababu walikataa maagizo yangu na kutotembea katika amri zangu, na wazikufuru Sabato zangu.
Because judgments my they had rejected and statutes my not they had walked in them and sabbaths my they had profaned for after idols their heart their [was] walking.
17 Lakini jicho langu likawahurumia kutokana na uharibifu na sikuwaangamiza jangwani.
And it looked with compassion eye my on them from destroying them and not I made them complete destruction in the wilderness.
18 Nikawaambia watoto wao jangwani, “Msitembee kutokana na amri za wazazi wenu; msiweke maagizo yao au kujinajisi wenyewe kwa sanamu.
And I said to children their in the wilderness in [the] statutes of ancestors your may not you walk and judgments their may not you keep and by idols their may not you make yourselves unclean.
19 Mimi ni Yahwe Mungu wenu, tembeeni katika amri zangu; tunzeni maagizo yangu na kuyatii.
I [am] Yahweh God your in statutes my walk and judgments my keep and do them.
20 Zitunzeni Sabato zangu takatifu ili kwamba zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, hivyo basi mtajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
And sabbaths my keep holy and they will become a sign between me and between you to know that I [am] Yahweh God your.
21 Lakini watoto wao waliniasi. Hawakutembea kwenye sheria zangu au kushika maagizo yangu, ambazo mwanadamu ataishi kama akizitii. Wamezinajisi Sabato zangu, hivyo nimeamua kumwaga ghadhabu yangu juu yao kutimiza ghadhabu yangu dhidi yao katika jangwa.
And they rebelled against me the children in statutes my not they walked and judgments my not they kept to observe them which he will do them the person and he will live by them sabbaths my they profaned and I said to pour out rage my on them to complete anger my on them in the wilderness.
22 Lakini niliurudisha mkono wangu na kutenda kwa ajili ya jina langu, hivyo lisitiwe unajisi katika macho ya mataifa ambao mbele ya macho yao niliwatoa Waisraeli.
And I turned back hand my and I acted for [the] sake of name my to not to be profaned to [the] eyes of the nations which I brought out them to eyes their.
23 Mimi mwenyewe pia nimeuinua mkono wangu kuapa juu yao jangwani, kwamba nitawatawanya kati ya maifa na kuwatawanya miongoni mwa nchi mabali mbali.
Also I I lifted up hand my to them in the wilderness to scatter them among the nations and to disperse them among the lands.
24 Nimeamua kufanya hivi kwa kuwa hawakuzitii amri zangu, na tangu walipo zikataa sheria zangu na kuzinajisi Sabato zangu. Macho yao yalizitamani sanamu za baba zao.
Because judgments my not they had done and statutes my they had rejected and sabbaths my they had profaned and after [the] idols of parents their they had been eyes their.
25 Kisha niliwapa amri ambazo hazikuwa nzuri, na maagizo ambayo hawakuweza kuishi kwayo.
And also I I gave to them statutes not good and judgments [which] not they will live by them.
26 Nikawafanya unajisi kwa zawadi zao wakati walipofanya dhabihu za kila limbuko la tumbo la uzazi na kutupa kwenye moto. Nalifanya hivi ili kuwaogofya hivyo wangeweza kujua kwamba mimi ni Yahwe!'
And I made unclean them by gifts their when made pass through every firstborn of a womb so that I may make appalled them so that this they may know that I [am] Yahweh.
27 Kwa hiyo, mwanadamu, waambie nyumba ya Israeli na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika hili pia baba zenu walinikufuru wakati walipokuwa sio waaminifu kwangu.
Therefore speak to [the] house of Israel O son of humankind and you will say to them thus he says [the] Lord Yahweh again this they blasphemed me ancestors your when acted unfaithfully they against me unfaithfulness.
28 Wakati nilipowaleta kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimewaapia kuwapatia, na kisha popote walipoona jiwe lolote refu na mti wenye majani, walitoa sadaka zao, walinikasirisha kwa sadaka zao, na huko pia walichoma ubani wao wa kunukia na kumwaga sadaka zao za kinywaji.
And I brought them into the land which I had lifted up hand my to give it to them and they saw every hill high and every tree leafy and they sacrificed there sacrifices their and they presented there [the] provocation of offering their and they made there [the] odor of soothing their and they poured out there drink offerings their.
29 Kisha nikawaambia, “Nini maana ya mahali palipoinuka ambapo mmeleta sadaka huko?” Hivyo jina lake linaitwa Bana hata leo.'
And I said to them what? [is] the high place where you [are] the [ones who] go there and it has been called name its Bamah until the day this.
30 Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Kwa nini unajinajisi mwenyewe kwa njia za baba zako? Kwahiyo kwa nini unatenda kama makahaba, kutafuta kwa ajili ya mambo ya machukizo?
Therefore say - to [the] house of Israel thus he says [the] Lord Yahweh ¿ in [the] way? of ancestors your [are] you making yourselves unclean and after detestable things their [are] you? acting as prostitutes.
31 Kwa kuwa wakati mtoapo zawadi zenu na kuwaweka watoto wenu kwenye moto, siku hii mnajitia unajisi pamoja na sanamu zenu zote. Kwa hiyo kwa nini niwaache mniulize mimi, nyumba ya Israeli? Kama niishivyo-Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Sitawaacha mniulize swali.
And when lift up gifts your when make pass children your in the fire you [are] making yourselves unclean to all idols your until this day and I will I let myself be consulted? by you O house of Israel [by] [the] life of me [the] utterance of [the] Lord Yahweh if I will let myself be consulted by you.
32 Mawazo yanayoumbika kwenye moyo wako hayatatokea kamwe. Mmesema, “Ngoja tuwe kama mataifa mengine, kama koo za nchi nyingine waabuduo mti na jiwe.”
And the [thing which] comes up on spirit your certainly not it will happen [that] which - you [are] saying we will be like the nations like [the] clans of the lands to serve wood and stone.
33 Kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Nitatawala hakika juu yenu kwa mkono wenye nguvu, mkono ulionyooshwa, na ghadhabu itakayomwagwa juu yenu.
[by] [the] life Of me [the] utterance of [the] Lord Yahweh if not by a hand strong and by an arm outstretched and with rage poured out I will reign over you.
34 Nitawatoa kutoka kwa watu wengine na kuwakusanya kutoka kwenye nchi mlizotawanyika ndani mwao. Nitafanya hivi kwa mkono hodari na kwa ghadhabu iliyomwagika.
And I will bring out you from the peoples and I will gather you from the lands which you have been scattered among them by a hand strong and by an arm outstretched and with rage poured out.
35 Kisha nitawaleta kwenye jangwa la watu, na huko nitawahukumu uso kwa uso.
And I will bring you into [the] wilderness of the peoples and I will enter into judgment with you there face to face.
36 Kama nilivyo wahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, hivyo pia nitawahukumu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Just as I entered into judgment with ancestors your in [the] wilderness of [the] land of Egypt so I will enter into judgment with you [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
37 Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, na nitawafanya kutii maagizo yangu ya agano.
And I will make pass you under the rod and I will bring you in [the] bond of the covenant.
38 Nitawasafisha kutoka miongoni mwenu maasi na wale ambao walionichukiza. Nitawatoa kutoka nchi ambayo wanayoishi kama wageni, lakini hawataingia kwenye nchi ya Israeli. Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I will purge from you those [who] rebel and those [who] transgress against me from [the] land of sojournings their I will bring out them and into [the] land of Israel not he will go and you will know that I [am] Yahweh.
39 Basi kwenu, nyumba ya Israeli, Bwana Yahwe asema hivi: Kila mmoja wenu ataenda kwa sanamu zake mwenyewe. Muwaabudu kama mtakataa kunisikiliza, lakini hamtalikufuru tena jina langu takatifu kwa zawadi zenu na sanamu zenu.
And you O house of Israel thus he says - [the] Lord Yahweh everyone idols his go serve and after if not you [will be] listening to me and [the] name of holiness my not you will profane again by gifts your and by idols your.
40 Kwa kuwa juu ya mlima wangu mtakatifu, juu ya kilele cha mlima wa Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-wote wa nyumba ya Israeli mtaniabudu huko katika nchi. Nitabarikiwa kwa kutaka sadaka zenu huko, na pia malimbuko yenu ya shukrani pamoja na vitu vyenu vyote vitakatifu.
For on [the] mountain of holiness my on [the] mountain of - [the] height of Israel [the] utterance of [the] Lord Yahweh there they will serve me all [the] house of Israel all of it in the land there I will accept them and there I will seek contributions your and [the] choicest of gifts your with all holy things your.
41 Nitawapokea kama harufu nzuri ya ubani wakati nitakapowatoa kutoka wale watu na kuwakusanya toka nchi ambazo mlizotawanyika. Nitajifunua mimi mwenyewe kama mtakatifu ndani yenu kwa ajili ya mataifa waone.
An odor of soothing I will accept you when bring out I you from the peoples and I will gather you from the lands which you have been scattered among them and I will show myself holy among you to [the] eyes of the nations.
42 Kisha, wakati nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, kwenye nchi ambayo niliuinulia mkono wangu kuapa kuwapatia baba zenu, mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And you will know that I [am] Yahweh when bring I you into [the] land of Israel into the land which I lifted up hand my to give it to ancestors your.
43 Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya huko, na matendo yenu yote machafu mliyoyafanya wenyewe, na mtajichukia wenyewe katika macho yenu kwa matendo yenu yote maovu mliyoyafanya.
And you will remember there ways your and all practices your which you have made yourselves unclean by them and you will loathe faces your for all wicked deeds your which you have done.
44 Hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe nifanyapo haya kwenu kwa ajili ya jina langu, sio kwa njia zenu mbaya au matendo yenu mabovu, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
And you will know that I [am] Yahweh when do I with you for [the] sake of name my not according to ways your wicked and according to practices your corrupt O house of Israel [the] utterance of [the] Lord Yahweh.
45 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
46 “Mwanadamu, weka uso wako kuelekea nchi za kusini, na kuongea juu ya kusini; tabiri juu ya msitu wa Negebu.
O son of humankind set face your [the] direction south-ward and prophesy against [the] south and prophesy against [the] forest of the field [the] south.
47 Uuambie msitu wa Negebu, 'Hivi ndivyo Yahwe asemavyo-Bwana Yahwe asema hivi: Tazama, nitaweka moto ndani yako. Utakula kila mti mbichi na kila mti mkavu ndani yako. Miali ya moto haitazimika; na kila uso utokao kusini hata kaskazini utateketezwa kwa moto.
And you will say to [the] forest of the south hear [the] word of Yahweh thus he says [the] Lord Yahweh here I [am] about to kindle in you - a fire and it will consume in you every tree moist and every tree dry not it will be extinguished [the] flame of flame and they will be scorched by it all faces from [the] south [the] north towards.
48 Kisha watu wote wenye mwili watajua yakwamba mimi ni Yahwe nimeuwasha moto, na hautazimika.”'
And they will see all flesh that I Yahweh I have kindled it not it will be extinguished.
49 Kisha nimesema, Ee! Bwana Yahwe, Wananisema mimi, 'Je! yeye sio mwenye kusema mafumbo?”'
And I said alas! O Lord Yahweh they [are] saying of me ¿ not making a parable parables [is] he.

< Ezekieli 20 >