< Danieli 1 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja Yerusalemu na kuuzunguka mji ili kuzuia mahitaji yake yote.
In year three of [the] reign of Jehoiakim [the] king of Judah he came Nebuchadnezzar [the] king of Babylon Jerusalem and he laid siege on it.
2 Bwana alimpa Nebukadneza ushindi dhidi ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, na alimpatia vitu vitakatifu kutoka nyumba ya Mungu. Alivipeleka vitu hivyo mpaka katika nchi ya Babeli, kwa nyumba ya mungu wake, na aliviweka vitu vitakatifu katika hazina ya mungu wake.
And he gave [the] Lord in hand his Jehoiakim [the] king of Judah and some of [the] end of [the] vessels of [the] house of God and he brought them [the] land of Shinar [the] house of god his and the vessels he brought [the] house of [the] treasury of god his.
3 Mfalme akamwambia Ashipenazi, afisa wake mkuu, awalete baadhi ya watu wa Israeli, wa familia ya kifalme na za kiungwana -
And he said the king to Ashpenaz [the] chief of officials his to bring some of [the] people of Israel and some of [the] offspring of royalty and some of the nobles.
4 vijana wasio na hila, wenye mwonekano wa kuvutia, wenye ujuzi katika hekima yote, wenye kujawa na ufahamu na weledi, na wenye sifa za kutumika katika ikulu ya mfalme. Alitakiwa kuwafundisha maandiko na lugha ya Babeli.
Youths whom not [was] in them any (blemish *Q(K)*) and good of appearance and having insight in all wisdom and knowing knowledge and understanding knowledge and whom ability [was] in them to stand in [the] palace of the king and to teach them [the] writing and [the] tongue of [the] Chaldeans.
5 Mfalme aliwatengea kwa ajili yao fungu kutoka katika chakula chake kizuri kwa kila siku na katika divai aliyokunywa. Vijana hawa walitakiwa kufunzwa kwa miaka mitatu, na baada ya hapo, wangeweza kumtumikia mfalme.
And he assigned to them the king [the] matter of a day in day its some of [the] deli-caci[es] of the king and some of [the] wine of drink his and to bring up them years three and from [the] end their they will stand before the king.
6 Miongoni mwao walikuwa ni Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria, baadhi ya watu wa Yuda.
And he was among them from [the] people of Judah Daniel Hananiah Mishael and Azariah.
7 Afisa mkuu aliwapa majina: Danieli alimwita Belteshaza, Hanania alimwita Shadraka, Mishaeli alimwita Meshaki, na Azaria alimwita Abedinego.
And he assigned to them [the] chief of the officials names and he assigned to Daniel Belteshazzar and to Hananiah Shadrach and to Mishael Meshach and to Azariah Abed-nego.
8 Lakini Danieli alinuia katika akili yake kuwa asingejitia ujanisi mwenyewe kwa chakula kizuri cha mfalme wala kwa divai ambayo alikunywa.
And he set Daniel on heart his that not he defiled himself with [the] delicaci[es] of the king and with [the] wine of drink his and he requested from [the] chief of the officials that not he will defile himself.
9 Basi, aliomba ruhusa kutoka kwa afisa mkuu ili kwamba asije akajitia uchafu yeye mwenyewe. Hivyo, Mungu alimpa Danieli kibali na huruma kupitia katika heshima ambayo afisa mkuu alikuwa nayo kwake.
And he gave God Daniel favor and compassion before [the] chief of the officials.
10 Afisa mkuu alimwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme. Ameagiza aina ya chakula na vinywaji mnavyotakiwa kutumia. Kwa nini awaone ninyi mkiwa mnaonekana vibaya kuliko vijana wengine wa umri wenu? Mfalme aweza kukitwaa kichwa changu kwa sababu yenu.
And he said [the] chief of the officials to Daniel [am] fearing I master my the king who he has assigned food your and drink your that why? will he see faces your looking thin more than the youths who [are] about age your and you will endanger head my to the king.
11 Kisha Daniel akamwambia msimamizi ambaye afisa mkuu alikuwa amemweka juu ya Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria.
And he said Daniel to the guardian whom he had assigned [the] chief of the officials over Daniel Hananiah Mishael and Azariah.
12 Alisema, “Tafadhari tujaribuni, sisi watumishi wako kwa siku kumi. Tupatieni tu mboga mboga za kula na maji ya kunywa.
Put to [the] test please servants your days ten so let people give to us some of the vegetables so we may eat and water so we may drink.
13 Kisha ulinganishe mwonekano wetu na mwonekano wa vijana wanaokula vyakula vya mfalme, na mtutendee, sisi watu wako kulingana na kile unachokiona.”'
And they may appear before you appearance our and [the] appearance of the youths who are eating [the] delicaci[es] of the king and just as you will see deal with servants your.
14 Hivyo msimamizi alikubaliana naye kufanya hivi, na aliwajaribu kwa siku kumi.
And he listened to them to the thing this and he put to [the] test them days ten.
15 Katika mwisho wa siku kumi mwonekano wao ulikuwa ni wenye afya nzuri kuliko wa wale vijana waliokula vyakula vya kifalme.
And from [the] end of days ten it appeared appearance their good and fat of flesh more than all the youths who were eating [the] delicaci[es] of the king.
16 Basi, msimamizi aliliondoa fungu lao la chakula na vivywaji vyao na walipewa mboga mboga tu.
And he was the guardian taking away delicaci[es] their and [the] wine of drink their and giving to them vegetables.
17 Na kuhusu vijana hawa nne Mungu aliwapa uelewa na ufahamu katika maandiko yote na hekima, na Danieli aliweza kupambanua aina zote za maono na ndoto.
And the youths these [the] four of them he gave to them God knowledge and insight in all writing and wisdom and Daniel he understood every vision and dreams.
18 Katika mwisho wa muda uliokuwa umepangwa na mfalme kuwaleta ndani, afisa mkuu aliwaleta mbele ya Nebukadneza.
And from [the] end of the days which he had said the king to bring them and he brought them [the] chief of the officials before Nebuchadnezzar.
19 Mfalme aliongea nao, na miongoni mwa kundi lote hapo hapakuwa na wa kuwalinganisha na akina Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria. Walisimama mbele ya mfalme, wakiwa tayari kumtumikia.
And he spoke with them the king and not he was found any of all of them like Daniel Hananiah Mishael and Azariah and they stood before the king.
20 Katika kila swali la hekima na ufahamu ambalo mfalme aliwauliza, aliwakuta wakiwa na uwezo mara kumi kuliko waganga wote na wale waliojidai kusema na wafu, waliokuwa katika ufalme wake wote.
And every matter of wisdom of understanding which he sought from them the king and he found them ten hands above all the soothsayer-priests the conjurers who [were] in all kingdom his.
21 Danieli alikuwa hapo mpaka mwaka wa kwanza wa Mfalme Koreshi.
And he was Daniel until year one of Cyrus the king.

< Danieli 1 >