< Amosi 7 >
1 Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha. Tazama, aliumba kundi kubwa la nzige wakati wa kuchipuka kwa mmea, na, tazama, ulikuwa ni mmea wa mwisho baada ya mavuno ya mfalme.
Thus he showed me [the] Lord Yahweh and there! [he was] forming locusts at [the] beginning of [the] coming up of the spring-crop and there! a spring-crop after [the] mowings of the king.
2 Wakati walipomaliza kula mbogamboga za nchi, kisha nikasema, “Bwana Yahwe, tafadhali nisamehe; Je Yakobo ataishije? kwa kuwa yeye ni mdogo sana.”
And it will be if it had finished to eat [the] vegetation of the land and I said O Lord Yahweh forgive please who? will he stand Jacob for [is] small he.
3 Yahwe akapunguza hasira kuhusu hili. “Haitatokea,” akasema.
He relented Yahweh on this not it will be he said Yahweh.
4 Hivi ndivyo ambavyo Bwana Yahwe alivyonionyesha: Tazama, Bwana Yahwe aliita juu ya moto kuhukumu. Nao ukakausha sana, kilindi chini ya dunia na kutaka kuitekeza nchi, pia.
Thus he showed me [the] Lord Yahweh and there! [was] calling for conducting a case by fire [the] Lord Yahweh and it consumed [the] deep great and it consumed the portion of land.
5 Lakini nikasema, “Bwana Yahwe, acha tafadhali; Yakobo ataishije? Kwa kuwa yeye ni mdigo sana.”
And I said O Lord Yahweh cease please who? will he stand Jacob for [is] small he.
6 Yahwe akagairi kuhusiana na hili, “Hili halitajitokeza pia,” asema Bwana Yahwe.
He relented Yahweh on this also it not it will be he said [the] Lord Yahweh.
7 Hivi ndivyo ambavyo Yahwe alivyo nionyesha: Tazama, Bwana amesimama karibu na ukuta, pamoja na uzi wa timiza kwenye mkono wake.
Thus he showed me and there! [the] Lord [was] standing on a wall of tin and [was] in hand his tin.
8 Yahwe akanambia, “Amosi, unaona nini?” nikasema, “Uzi wa timazi.” Kisha Bwana akasema, “Tazama, nitaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli. Sintowaharibu tena.
And he said Yahweh to me what? [are] you seeing O Amos and I said tin and he said [the] Lord here I [am] about to put tin in [the] midst of people my Israel not I will repeat again to pass by it.
9 Mahala pa juu pa Isaka pataharibiwa, patakatifu pa Israeli pataangamia, na nitainuka juu ya nyumba ya Yeroboamu kwa upanga.”
And they will be made desolate [the] high places of Isaac and [the] sanctuaries of Israel they will be waste and I will arise on [the] house of Jeroboam with the sword.
10 Kisha Amazia, yule kuhani wa Betheli, akatuma ujumbe kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli: “amosi amefanya njama dhidi yako katikati ya nyumba ya Israeli. Nchi haiwezi kubeba maneno yote haya.
And he sent Amaziah [the] priest of Beth-el to Jeroboam [the] king of Israel saying he has conspired on you Amos in [the] midst of [the] house of Israel not it is able the land to endure all words his.
11 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Amosi, 'Yeroboamu atakufa kwa upanga, na hakika Israeli itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'
For thus he has said Amos by the sword he will die Jeroboam and Israel certainly it will go into exile from on land its.
12 Amazia akamwambia Amosi, “Mwonaji, nenda, kimbia irudie nchi ya Yuda, na hapo ule mkate na kutabiri.
And he said Amaziah to Amos O seer go flee yourself to [the] land of Judah and eat there bread and there you will prophesy.
13 Lakini usitabiri tena hapa katika Betheli, kwa kuwa ni patakatifu pa mfalme na nyumba ya kifalme.”
And Beth-el not you must repeat again to prophesy for [is] a sanctuary of a king it and [is] a house of kingdom it.
14 Kisha Amosi akamwambia Amazia, “Mimi sio nabii wala mwana wa nabii. Mimi ni mchungaji wa mifugo, na mtunza mikuyu.
And he answered Amos and he said to Amaziah not [am] a prophet I and not [am] a son of a prophet I for [was] a herdsman I and a fig picker of sycamores.
15 Lakini Yahwe akanichukua kutoka kuchunga mifugo na kunambia, 'Nenda, katabiri kwa watu wangu Israeli.'
And he took me Yahweh from after the flock and he said to me Yahweh go prophesy to people my Israel.
16 Sasa sikia neno la Yahwe. Wewe usemaye, 'Usitabiri juu ya Israeli, na usiongee juu ya nyumba ya Isaka.
And therefore hear [the] word of Yahweh you [are] saying not you must prophesy on Israel and not you must prophesy on [the] house of Isaac.
17 Kwa hiyo hivi ndivyo Yahwe asemavyo, 'Mke wako atakuwa kahaba katika mji; wana wako waume na binti zako wataanguka kwa upanga; nchi yako itapimwa na kugawanywa; utakufa katika nchi najisi, na Israeli hakika itakwenda utumwani kutoka nchi yake.”'
Therefore thus he says Yahweh wife your in the city she will be a prostitute and sons your and daughters your by the sword they will fall and land your with measuring-line it will be divided and you on ground unclean you will die and Israel certainly it will go into exile from on land its.